Naombeni ushauri kuhusu tabia ya dada yangu

Naombeni ushauri kuhusu tabia ya dada yangu

ana tatizo la kiakili huyo + wivu wa kichawi, pia anapepo mbaya mean hata baada ya ndoa hali itazidi kuwa tete zaidi,plz baada ya ndoa yako kaa nae mbali sana,pia jaribu kumweleza jamaa yako nina dada yangu ambaye anatatizo la kiakili kidogo! ili ajijenge nalo kisaikolojia,ili litakapo waka asistaajabu!apuuze

ninakushukuru sana kwa ushauri mzuri ngoja nilifanyie kazi. asante sana
 
Huyo dada yako ana roho mbaya sana,anakuonea wivu kwakuwa hajaolewa,bora msimwambie baada ya harusi wekeni kikao cha familia kumueleza ukweli wa mambo anayoyafanya asije kukuhalibia ndoa.

jana kaniuliza jamani mdogo wangu mbona huolewi nina hamu ya kucheza harusi, nikamjibu nitapata wapi mwanaume mpya? kwa kuwa wote umeshatembea nao? akanyamaza sana then akacheka akajibu ukiyafuatilia hayo utazeekea nyumbani. hapo ndipo nilipoamini watu wanavyosema ana jini mahaba, sasa jana sijui alimtoka kidogo. inatisha
 
Nimempenda ghafla dada yako.

Hahahahaah

haya bwana yuko hapo open anafanya degree yake ya pili naweza kuku direct ukamuona utampenda zaidi, ila akikustukia tuu kama unaenda kumchoresha jiandae kwa kupigwa mawe
 
Pole
Fuata ushauri wa baba zako wadogo

Ingawa nao nawashangaa, kama wanajua tabia ya dada yako, kwa. Nini walimsikiliza????

Pia hiyo dada yako ni wa kumuepuka inaelekea ana roho mbaya na wivu si wa kumshirikisha kwenye mambo yako yote


Sent from my iPhone using JamiiForums
mara ya kwanza walijua ni ukweli na ndiyo maana walikuwa wanamsikiliza sikuwa na uhuru hata wa kujitetea, na pia kwa kuwa sijakulia hapa sana ikaonekana kweli mimi nimevamia mwanaume wake, sasa ilivyojirudia mara tatu ndiyo wamestuka kuona ni uongo ina maana kila anayeletwa ni wake, na kwanini wakiwa nae wasitangaze ndoa mpaka kwangu, hivyo sasa akili zimewarudia
 
Kuna maisha baada ya lunch yenu mweleze mwenzako aelewe ampuuze akileta upuuz

ni kweli asante sana, mpaka sasa kila mtu humu amenishauri kuwa nimweleze mchumba wangu na kwa kuwa tupo watu tofauti na nilihitaji ushauri wenu, sina budi kuuchukua na kuufanyia kazi haraka, asanteni na nimefarijika sana moyoni
 
Dah. Umeshashauriwa. Ila tunao ndugu hata ukinunua gari ama kiwanja, ukipata kazi ama kufungua biashara huthubutu kumuambia. Mie naomba leo nijitolee kuwa dada yako wa hiari. Nikusaidie kumnyoosha huyu dada yako na kumuweka mahali pake. Yaani unampandishia vioo, afu tinted ya maana na unamuachia vumbi. Watu wa hivi huwa wanatia hasira sana aisee.

if you are game, send me a pm.

bestito Kiranga, njoo tafadhali. Huyu first client but in our baddest way!
 
Last edited by a moderator:
Dah. Umeshashauriwa. Ila tunao ndugu hata ukinunua gari ama kiwanja, ukipata kazi ama kufungua biashara huthubutu kumuambia. Mie naomba leo nijitolee kuwa dada yako wa hiari. Nikusaidie kumnyoosha huyu dada yako na kumuweka mahali pake. Yaani unampandishia vioo, afu tinted ya maana na unamuachia vumbi. Watu wa hivi huwa wanatia hasira sana aisee.

if you are game, send me a pm.

bestito Kiranga, njoo tafadhali. Huyu first client but in our baddest way!

wow! nashukuru sana kupata dada wa hiari, ni kweli nimeshapata ushauri mwingi na nimefarijika sana
 
Kwanza kabisa unatakiwa umuombe sana Munguuu kwa ajilii ya harusi yako na pili mueleze mchumba wako ujue kuwa muwazi kwa mwanaume unaetaka kfunga nae ndoa
Kila la kherii
 
Back
Top Bottom