Naombeni ushauri kuhusu tabia ya dada yangu

Naombeni ushauri kuhusu tabia ya dada yangu

Viumbe wazito ndo dadako....
Mueleze mchumba wako tabia ya Dada ako kwa maana anaweza kuharibu na ukabaki na Pete yako mkononi
 
Na watafuta madada wa hizo tabia huyu tunaendana kabisa ,ni pm nimtulize kabla huja funga ndoa
 
Kweli msumulie mchumba au atakutia aibu mbele yake na ndugu zake.

Yeye akijua atajua cha kuwaambia ndugu zake bila kuharibu yeye kukukimbia akidhani anaingia kwenye familia ya ajabu.

Huyo dada nyamaza apate mmshtuko ni wivu tu, sasa mweleze wako na sema dada huyo hayupo hapo mjini danganya yupo mkoa mwingine ili asikushangae na usiseme yote ya mliopanga na familia yako kumficha atawashangaa sana na kuogopa.

Mweleze tu tabia ya dada na matukio labda mawili na sema mila na desturi zikafanya iwe hivyo usikubaliwe kuolewa. Usiongeee sanaaaaaaaa labda mbeleni mkishaoana eeehhh

Na ukiolewa usimkaribishe dada kulala kwako akija aje na wazazi au sema haupo akitaja kuja kukutembelea. Mchawi wako huyo hatakuachia kwa kutaka kulipizia kuwa ulimgundua akashindwa kukuzuia tena. Kaa nae mbali maishani mwako na ndoa yako kabisa au utakoma vituko atakavyofanya huyo.
 
Hiki kisa ni cha kweli? Basi lawama kwa dada ondoa. Kila unachokisema kuhusu yeye kinaonyesha ana tatizo la akili. Mna mgonjwa. Sasa kwa kuwa umeshaona tabia yake, wadau hapa wameshakutabiria ya mbele. Si ajabu akatia viwembe au moto gauni lako siku ya harusi ukaishia kuvaa batiki!! Hata kama utafanikiwa kufunga ndoa huyu atakuandama tu na si ajabu akaja kumsingizia mumeo hata ubakaji ilimradi akunyime raha. We mweleze huyo shemeji ukweli kuhusu shida ya dada yako (sema ukweli unaohusika hapo tu, kweli zingine ni baina yako na Mungu mpaka uingie nazo kaburini). Mkiweza kuishi nae mbali kijiografia itakuwa vyema pia.
 
Usije kuzimia siku ya harusi dada yako akiibua zengwe kanisani kuwa ana mimba ya huyu mchumba wako! Muhimu kwenye kamati ya maandalizi msisahau kuweka budget ya kuwalipa FFU ili wakae standby dada yako akileta za kuleta wamvurumishie mabomu ya machozi maana anaonekana ni hatari kwa usalama wa ndoa yako! Halafu kaa chini na mama yako umuulize vizuri akuambie kama kweli dada yako ni mtoto wa baba kweli maana haiwezekani awe na tabia za broiler wakati yeye ni wa kienyeji!
 
Kuna maisha baada ya lunch yenu mweleze mwenzako aelewe ampuuze akileta upuuz
 
muombee dada yako ana stress za kumis mambo, inatakiwa akutane na mimi nimpe dawa alafu atasahau list yake yote.
 
Pole
Fuata ushauri wa baba zako wadogo

Ingawa nao nawashangaa, kama wanajua tabia ya dada yako, kwa. Nini walimsikiliza????

Pia hiyo dada yako ni wa kumuepuka inaelekea ana roho mbaya na wivu si wa kumshirikisha kwenye mambo yako yote


Sent from my iPhone using JamiiForums
 
Nimempenda ghafla dada yako.

Hahahahaah
 
Huyo dada yako ana roho mbaya sana,anakuonea wivu kwakuwa hajaolewa,bora msimwambie baada ya harusi wekeni kikao cha familia kumueleza ukweli wa mambo anayoyafanya asije kukuhalibia ndoa.
 
Umemdekeza sana huyo dada yko ni kumpa makavu kwenda front,no kulea lea ujinga.
 
ana tatizo la kiakili huyo + wivu wa kichawi, pia anapepo mbaya mean hata baada ya ndoa hali itazidi kuwa tete zaidi,plz baada ya ndoa yako kaa nae mbali sana,pia jaribu kumweleza jamaa yako nina dada yangu ambaye anatatizo la kiakili kidogo! ili ajijenge nalo kisaikolojia,ili litakapo waka asistaajabu!apuuze
 
msikate tamaa kuhusu maombezi. kuna matatizo mengine kama hayo yatatoka kwa kufunga na kuomba kwa imani, wala msimuhukumu aminini sio yeye ni pepo linamuendesha, hakuna binadamu anayependa aishi katika mfumo huo. Mungu awasaidie, jaribu kupeleka picha

kiukweli ana matatizo mengi sana nikieleza hapa kila mtu atamuonea huruma, mimi nahisi kichwani na hayo madude, nashukuru sana kwa ushauri
 
Back
Top Bottom