Naombeni ushauri kuhusu tabia ya dada yangu

Naombeni ushauri kuhusu tabia ya dada yangu

Hapo atake asitake unaolewa mie na dada yangu kuna vuguvu linaendelea kama lako anadai had aolewe yeye ndio na mim nifuate.

sasa naona miaka inazid kwenda mie nicje poteza bahati now nimepata mtoto lakn bado anagubu na mim na kuniita mal. ya. akiambiwa apeleke mchumba hapeleki ni gubu 2.

hampendi mwanangu had nyumba naiona chungu. na hv kapata taarfa ndoa mwakan yan anataman aniloge.

Mungu akusaidie dada angu tena mwombe mungu sana hawakawii kuloga hata kama 2mezaliwa pamoja lakn kila mtu na tabia zake. kila la kheri best
 
Dunia ina mambo.
Ni ngumu sana kuamini kuwa wewe na dada yako mmezaliwa tumbo moja.
Mnatofautiana sana hasa katika mamboa ambayo ilibidi mfanane au mrandane
 
asante sana, tena ukimuona yeye ni mzuri sana wa sura na umbo kuliko mimi ila ndiyo hivyo tuu

Anaweza kuambiwa lakini usimuonyeshe ni nani. Mwambie kuna siku utamleta home amuone. Wakati akisubiria umlete home, anakuja kushangaa kuambiwa dada wiku ijayo nafunga ndoa na yule mchumba wangu. Akikuuliza vipi unamwambia sorry, umeamua kuharakusha coz kuna mambo mengine unataka kufanya. ..
 
asante sana, tena ukimuona yeye ni mzuri sana wa sura na umbo kuliko mimi ila ndiyo hivyo tuu

Embu tuma picha yake tumtafutie mchumba anayewezana nae..kuna wababe huku kitaa..but pole xna
 
Hapo atake asitake unaolewa mie na dada yangu kuna vuguvu linaendelea kama lako anadai had aolewe yeye ndio na mim nifuate.

sasa naona miaka inazid kwenda mie nicje poteza bahati now nimepata mtoto lakn bado anagubu na mim na kuniita mal. ya. akiambiwa apeleke mchumba hapeleki ni gubu 2.

hampendi mwanangu had nyumba naiona chungu. na hv kapata taarfa ndoa mwakan yan anataman aniloge.

Mungu akusaidie dada angu tena mwombe mungu sana hawakawii kuloga hata kama 2mezaliwa pamoja lakn kila mtu na tabia zake. kila la kheri best

Duh!! Nimethibitisha kweli wanawake hampendani na kuoneana wivu..kama ndugu yako wa damu anaolewa si ni furaha kuwa kapata mume sasa wivu wa nin..but angalieni msitoane roho
 
Wapendwa samahani sana kwa usumbufu,

Nina kitu ambacho kwa kweli kinaniumiza moyo wangu sana, sisi kwetu tumezaliwa wawili na wote ni wasichana, dada yangu ni mkubwa kwangu kwa miaka saba hajaolewa na kwa kweli sijawahi kuona yuko na mwanaume ambaye wanadumu kwa muda hata kwa wiki mbili.

Akiwa na mtu yeye ni mtu wa kumfokea mwanaume na kumtukana hivyo ni dada mwenye kazi nuzri msomi kiasi ila tatizo lake ni hilo.

Shida yangu kubwa iliyonifanya niilete hapa kila nikipata mchumba akija nyumbani kujitambulisha dada yangu anadai ni mpenzi wake wa zamani na maneno hayo anawaeleza wazazi hivyo yule mwanaume hawezi kukubaliwa kuendelea na mimi.

Mara ya kwanza nilijua kweli huyo kaka hakulalamika akaondoka zake ni muda mrefu sana, nikapata mwingine dada akadai hivyo nina amini kwa kuwa tanzania kubwa.

Cha kushangaza nikapata mwanaume wa nchi nyingine nimemleta Tanzania kwa ajili ya kujitambulisha dada yangu baada ya muda akadai yule baba atembea nae kipindi hiki nilichokuja nae Tanzania.Kiukweli niliumia sana.

Yule Mjapan akatuona sisi washenzi akaondoka zake yamebaki mawasiliano ya kawaida tuu. Mungu kanikumbuka tena nimepata jamaa mwingine, baba akashauri tupange tarehe ambayo dada hayupo, na kweli kila kitu kilienda sawa.

Harusi yangu inakaribia sana na mpaka sasa dada yangu hawajawahi kuonana na mchumba wangu huyu mpya na hajapata uhakika kama kweli nina mchumba kwani hata pete ya uchumba sivai kwa kumuogopa yeye.

Naomba ushauri je! nimweleze ukweli dada kuwa nina mchumba ila tamuona siku ya harusi?

Au nimweleze mchumba tabia za dada ili hata likitokea awe anajua?

Baba zangu wadogo wanashauri asiambiwe kitu na siku ya harusi astukizwe tuu kwani hakutakuwa na sherehe kubwa ni lunch tuu na vinywaji.

Asanteni nina imani mmenielewa.

Nisaidieni

piga buyu cya.
 
Wapendwa samahani sana kwa usumbufu,

Nina kitu ambacho kwa kweli kinaniumiza moyo wangu sana, sisi kwetu tumezaliwa wawili na wote ni wasichana, dada yangu ni mkubwa kwangu kwa miaka saba hajaolewa na kwa kweli sijawahi kuona yuko na mwanaume ambaye wanadumu kwa muda hata kwa wiki mbili.

Akiwa na mtu yeye ni mtu wa kumfokea mwanaume na kumtukana hivyo ni dada mwenye kazi nuzri msomi kiasi ila tatizo lake ni hilo.

Shida yangu kubwa iliyonifanya niilete hapa kila nikipata mchumba akija nyumbani kujitambulisha dada yangu anadai ni mpenzi wake wa zamani na maneno hayo anawaeleza wazazi hivyo yule mwanaume hawezi kukubaliwa kuendelea na mimi.

Mara ya kwanza nilijua kweli huyo kaka hakulalamika akaondoka zake ni muda mrefu sana, nikapata mwingine dada akadai hivyo nina amini kwa kuwa tanzania kubwa.

Cha kushangaza nikapata mwanaume wa nchi nyingine nimemleta Tanzania kwa ajili ya kujitambulisha dada yangu baada ya muda akadai yule baba atembea nae kipindi hiki nilichokuja nae Tanzania.Kiukweli niliumia sana.

Yule Mjapan akatuona sisi washenzi akaondoka zake yamebaki mawasiliano ya kawaida tuu. Mungu kanikumbuka tena nimepata jamaa mwingine, baba akashauri tupange tarehe ambayo dada hayupo, na kweli kila kitu kilienda sawa.

Harusi yangu inakaribia sana na mpaka sasa dada yangu hawajawahi kuonana na mchumba wangu huyu mpya na hajapata uhakika kama kweli nina mchumba kwani hata pete ya uchumba sivai kwa kumuogopa yeye.

Naomba ushauri je! nimweleze ukweli dada kuwa nina mchumba ila tamuona siku ya harusi?

Au nimweleze mchumba tabia za dada ili hata likitokea awe anajua?

Baba zangu wadogo wanashauri asiambiwe kitu na siku ya harusi astukizwe tuu kwani hakutakuwa na sherehe kubwa ni lunch tuu na vinywaji.

Asanteni nina imani mmenielewa.

Nisaidieni
pole dada yako ana wivu. jealous is disability. Je huyu wa sasa kama ni mtu muelewa atakuwa by your side. BUT U ALSO NEED TO STAND UP ON UR OWN. DADAKO UBAKI UNDUGU ILA MAMBO YAKO USIMSHIRIKISHE SIO MTU Mzuri. Najua atakununia ila chunga sana. usikubali awe na mawasiliano ama mazungumzo yeyote na mumeo mtarajiwa. she is a bichywitchy. lol
 
Huyo dada kiboko,nisichoelewa ni kwa nini familia yenu inampa nguvu ya kufanya atakalo.
 
pole dada yako ana wivu. jealous is disability. Je huyu wa sasa kama ni mtu muelewa atakuwa by your side. BUT U ALSO NEED TO STAND UP ON UR OWN. DADAKO UBAKI UNDUGU ILA MAMBO YAKO USIMSHIRIKISHE SIO MTU Mzuri. Najua atakununia ila chunga sana. usikubali awe na mawasiliano ama mazungumzo yeyote na mumeo mtarajiwa. she is a bichywitchy. lol

nina mshukuru Mungu nimetoka kuongea nae leo muda si mrefu na mpaka sasa niko kwake, amenielewa sana .
 
Huyo dada kiboko,nisichoelewa ni kwa nini familia yenu inampa nguvu ya kufanya atakalo.

mwanzo walimuamini sana haikuwa rahisi kumzuia kwa maneno yake na wazazi walikuwa upande wake sana, ila sasa mambo yamebadilika, kwa kifupi leo jumapili nimemwambia mchumba wangu kuhusu dada yangu, kwanza ameshangaa sana ila amenishukuru na tatu amenilaumu kwanini sikumwambia mapema kwa kuwa dada anahitaji maombi na ushauri kutoka kwa wataalamu wa akili, hivyo amenielwa sana na kunipa pole kwa yote.
 
Anaweza kuambiwa lakini usimuonyeshe ni nani. Mwambie kuna siku utamleta home amuone. Wakati akisubiria umlete home, anakuja kushangaa kuambiwa dada wiku ijayo nafunga ndoa na yule mchumba wangu. Akikuuliza vipi unamwambia sorry, umeamua kuharakusha coz kuna mambo mengine unataka kufanya. ..

huwezi kuamini vitu vingi nafanya kimya kimya tuu ila kama nilivyosema ni mtu wa machale, leo nimeongea na mchumba wangu kanielewa sana nashukuruni sana kwa ushauri wenu
 
Dunia ina mambo.
Ni ngumu sana kuamini kuwa wewe na dada yako mmezaliwa tumbo moja.
Mnatofautiana sana hasa katika mamboa ambayo ilibidi mfanane au mrandane

tumbo moja yeye wa kwanza baada ya miaka saba nikapatikana mimi
 
Hapo atake asitake unaolewa mie na dada yangu kuna vuguvu linaendelea kama lako anadai had aolewe yeye ndio na mim nifuate.

sasa naona miaka inazid kwenda mie nicje poteza bahati now nimepata mtoto lakn bado anagubu na mim na kuniita mal. ya. akiambiwa apeleke mchumba hapeleki ni gubu 2.

hampendi mwanangu had nyumba naiona chungu. na hv kapata taarfa ndoa mwakan yan anataman aniloge.

Mungu akusaidie dada angu tena mwombe mungu sana hawakawii kuloga hata kama 2mezaliwa pamoja lakn kila mtu na tabia zake. kila la kheri best

asante sana kwa ushauri, Mungu atakupigania mwenzangu na hongera sana kwa mtoto, yaani aliyewaloga hawa wadada sijui ni nani
 
Back
Top Bottom