GoldDhahabu
JF-Expert Member
- Apr 29, 2023
- 4,695
- 6,397
Tafadhali naomba mchango wako wa mawazo!
Nimekuwa nikitamani sana kuzitembelea baadhi ya nchi za Afrika ambazo bado sijafika. Ninatarajia kutimiza sehemu ya hiyo hiyo ndoto hapo baadaye mwaka huu.
Ninatarajia kutembelea alau nchi nne, kama bajeti itaruhusu, nazo ni AFRIKA KUSINI, BOTSWANA, LESOTHO na NAMIBIA. Safari yangu itakuwa ya wiki moja.
Dhumuni kuu la kusafiri ni "kuosha macho", yaani, kuona jinsi maisha yalivyo katika nchi za wenzetu, n.k. Kwa kifupi, ni safari ya kitalii.
Bajeti yangu ni shilingi milioni mbili. Itagharamia mahitaji yote isipokuwa passport. Usafiri ni wa basi, na kwa upande wa malazi, nitafikia lodge za bei rahisi. Muhimu ziwe sehemu salama.
Naomba kufahamu yafuatayo:
1. Kwa bajeti hiyo, nitaweza kuzifikia nchi zote 4 au nitalazimika kuzipunguza? Hata kama nikilazikika kutumia siku moja tu katika nchi husika, itatosha. Na kama nikiona bajeti haitatosha, nitaondoa Lesotho na Namibia kwenye orodha ya nchi nitakazozitembelea.
2. Unanishauri nitembelee maeneo/ miji gani kwa kila nchi?
3. Katika hizo nchi tajwa, kuna inayohitaji visa kwa Mtanzania?
4. Wapi pa kupandia basi kwa mtu anayeanzia safari Mwanza? Lazima kwenda hadi Dar?
5. Mabasi gani yanatoa huduma husika?
6. Sina pasi ya kusafiria. Travel document itatosha? Najua yenyewe haichukui muda mrefu kupatikana.
7. Lodge zipi za bei rahisi lakini zilizopo maeneo salama?
8. Nini cha kuzingatia sana nikiwa
katika nchi husika na wakati wa safari kwa ujumla?
Natanguliza shukrani zangu za dhati kwa ushirikiano wako chanya. Asante sana.
Nimekuwa nikitamani sana kuzitembelea baadhi ya nchi za Afrika ambazo bado sijafika. Ninatarajia kutimiza sehemu ya hiyo hiyo ndoto hapo baadaye mwaka huu.
Ninatarajia kutembelea alau nchi nne, kama bajeti itaruhusu, nazo ni AFRIKA KUSINI, BOTSWANA, LESOTHO na NAMIBIA. Safari yangu itakuwa ya wiki moja.
Dhumuni kuu la kusafiri ni "kuosha macho", yaani, kuona jinsi maisha yalivyo katika nchi za wenzetu, n.k. Kwa kifupi, ni safari ya kitalii.
Bajeti yangu ni shilingi milioni mbili. Itagharamia mahitaji yote isipokuwa passport. Usafiri ni wa basi, na kwa upande wa malazi, nitafikia lodge za bei rahisi. Muhimu ziwe sehemu salama.
Naomba kufahamu yafuatayo:
1. Kwa bajeti hiyo, nitaweza kuzifikia nchi zote 4 au nitalazimika kuzipunguza? Hata kama nikilazikika kutumia siku moja tu katika nchi husika, itatosha. Na kama nikiona bajeti haitatosha, nitaondoa Lesotho na Namibia kwenye orodha ya nchi nitakazozitembelea.
2. Unanishauri nitembelee maeneo/ miji gani kwa kila nchi?
3. Katika hizo nchi tajwa, kuna inayohitaji visa kwa Mtanzania?
4. Wapi pa kupandia basi kwa mtu anayeanzia safari Mwanza? Lazima kwenda hadi Dar?
5. Mabasi gani yanatoa huduma husika?
6. Sina pasi ya kusafiria. Travel document itatosha? Najua yenyewe haichukui muda mrefu kupatikana.
7. Lodge zipi za bei rahisi lakini zilizopo maeneo salama?
8. Nini cha kuzingatia sana nikiwa
katika nchi husika na wakati wa safari kwa ujumla?
Natanguliza shukrani zangu za dhati kwa ushirikiano wako chanya. Asante sana.