GoldDhahabu
JF-Expert Member
- Apr 29, 2023
- 4,695
- 6,398
Umepanga kutembelea nchi ngapi katika kipindi cha miaka 5 ijayo?
Binafsi, ninapenda sana kusafiri, lakini kwa sababu ya kiwango cha kipato, bado sijazimaliza hata nchi za Afrika Mashariki.
Mpaka sasa, nchi nilizokwishatia miguu yangu ni Kenya, Uganda na Burundi.
Ikimpendeza Mungu, mwishoni mwa mwaka huu nitaenda Rwanda na South Africa.
Kwa sababu safari ya South Africa itakuwa kwa basi, nitaweza kupitia nchi kadhaa, labda Zambia, Zimbabwe, n.k. Bado sijaamua route, lakini huenda nikaenda kwa basi nikarudi kwa ndege, au vinginevyo.
Kwa hiyo, nimeziengua Rwanda na S. A kwenye nchi za kuzitembelea katika miaka mitano ijayo. Ninahesabu nimeshazitembelea.
Hizi ndizo nchi nitakazozitembelea katika kipindi cha miaka mitano kuanzia 2024:
1. Misri
2. Nigeria
3. Dubai - ( UAE)
4. Israel
5. Ugiriki
6. Uturuki
7. China
8. Uingereza
9. Marekani
10. Canada.
Natamani kwamba ifikapo Disemba 2028, niwe nimeshazitembelea nchi zote hizo hapo juu, na zaidi, ikiwezekana.
Wewe umepanga kutembelea nchi zipi?
Binafsi, ninapenda sana kusafiri, lakini kwa sababu ya kiwango cha kipato, bado sijazimaliza hata nchi za Afrika Mashariki.
Mpaka sasa, nchi nilizokwishatia miguu yangu ni Kenya, Uganda na Burundi.
Ikimpendeza Mungu, mwishoni mwa mwaka huu nitaenda Rwanda na South Africa.
Kwa sababu safari ya South Africa itakuwa kwa basi, nitaweza kupitia nchi kadhaa, labda Zambia, Zimbabwe, n.k. Bado sijaamua route, lakini huenda nikaenda kwa basi nikarudi kwa ndege, au vinginevyo.
Kwa hiyo, nimeziengua Rwanda na S. A kwenye nchi za kuzitembelea katika miaka mitano ijayo. Ninahesabu nimeshazitembelea.
Hizi ndizo nchi nitakazozitembelea katika kipindi cha miaka mitano kuanzia 2024:
1. Misri
2. Nigeria
3. Dubai - ( UAE)
4. Israel
5. Ugiriki
6. Uturuki
7. China
8. Uingereza
9. Marekani
10. Canada.
Natamani kwamba ifikapo Disemba 2028, niwe nimeshazitembelea nchi zote hizo hapo juu, na zaidi, ikiwezekana.
Wewe umepanga kutembelea nchi zipi?