Sito kwamba yeye alikuwa mkweli bali alikuwa mkweli na muaminifu na hili pia walilishuhudia maadui zake. Sasa utaona lipi zito halo kati ya kujishuhudia mwenyewe au wale walio kupiga vita wakakiri ya kuwa weww ni mkweli na muaminifu.Swali lipo palepale weka andiko Muhammad akisema yeye ni kweli na uhai embu jibu kama huna jibu kiri tuendelee na mengine
Koran 22:62. Hayo ni kwa kuwa Mwenyezi Mungu ndiye Wa Kweli,....
John 14: 6Yesu akamjibu, “Mimi ni njia, na ukweli na uhai.
Naanzia hapa :
Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alipapanda juu ya jabali Swafaa akawaita watu wake na kuwaambia: "Enyi Maquraysh (na riwaayah nyingine enyi Banuu Manaaf, Enyi Banuu fulani na fulani). Je, ikiwa nitawaambieni kuwa wapanda farasi wapo nyuma ya jabali hili wakijitayarisha kukushambulieni, mtanisadiki?" Wote kwa pamoja wakamjibu:
"Bila shaka tutakusadiki, kwa sababu hatujapata kusikia kutoka kwako isipokuwa maneno ya kweli." Akasema: "Basi mimi ni mwonyaji kwenu juu ya adhabu kali iliyo mbele yenu. Okoeni nafsi zenu kutokana na moto…" [Al-Bukhaariy, Muslim na wengineo kwa riwaayah tofauti]
Kisha naendela na hapa :
Hii ni kauli ya Abu Jahl, huyu alikuwa akimpinga Mtume, lakini alikiri juu ya ukweli na uaminifu wa Mtume.
“Wa-Allaahi mimi najua vilivyo kuwa yeye ni Mkweli….Tulikuwa tukimwita katika ujana wake Asw-Swaadiq Al-Amiyn.” (Mkweli Mwaminifu). [Tafsiyr Al-Qurtwubiy]
Kisha narudi hapa :
Na yule aliyekuja na ukweli na wakausadikisha - hao ndio wenye taqwa. [Az-Zumar: 33]
Amesema Mujaahid na Qataadah na wengineo kuhusu: “Na yule aliyekuja na ukweli” “Huyo ni Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam)” [Tafsiyr Ibn Kathiyr]
Misho wa kunukuu.
Nakukumbusha maswali yangu :
1. Yesu ni njia, je ni njia ya kuelekea wapi ?
2. Mwanga wa Yesu ni upi ?
3. Kwanimi Yesukila jambo alikuwa analielekeza kwa Mola muumba ?