Kuna mwalimu wangu aliwahi kujenga hoja yake kuhusu utatu akasema.
" Ujue ni rahisi kumuelewezsha mtoto kuwa Mungu I mmoja, kuliko kumwambia Mungu amegawanyika mara tatu,"
Nilipouona huu mfano wako ndio Nimekumbuka hii, yaani najiuliza kama sisi watu wazima umeona huwenda hatuja uelewa huo mfano wako, sijui watoto wenu huwa mnawaelewesha vipi?
Hivi unajua tofauti ya sifa na dhati?
Gari - dhati
Linakimbia, jeusi - sifa
Tangu nianze kutumia Jf sijawahi kumuona mkristo akifafanua utatu akaeleweka.
ngoja nijaribu kuelezea utatu.
Kwanza ili uelewe utatu lazima ujue utofauti huu
a)1+1+1=3
b)1×1×1= 1
Katika mfano ' b' hapo juu ndio utatu wenyewe .
Ni hivi , baada ya wanadamu kuasi katika kanuni za kiroho ilipaswa lazima uhai utoke ndio wanadamu wapate kusamehewa dhambi zao.
Kumbuka Mungu hajikani neno lake, mshahara wa dhambi ni mauti na yeyote aliyetaka kuondolewa dhambi mauti iliyotokana na kuchinja mnyama au wanyama na kutoa sadaka( utaona kwenye agano la kale ) ilihusika.
Sasa kwa kuwa Mungu ana upendo, na ili asilikane neno lake na sheria yake mwenyewe ilibidi ashuke mwenyewe na itolewe sadaka takatifu ambayo itakomboa watu wote na utumwa wa dhambi ambao uliwahitaji wao kutoa sadaka niliyotaja hapo juu.
Sasa Mungu anashukaje, hapa ndio utatu unaeleweka sasa , Mungu akashuka kwa njia ya mwanadamu ( kumbuka yesu hakuwa mbegu ya mwanadamu ) kama wanadamu wengine, na hakuna mwanadamu wa kawaida ambaye anatokea katika mbegu ambazo sio za mwanadamu.
Mungu huyo huyo akashuka in form of a human kwaajili ya ukombozi wa watu.
Sasa kuna watu huwa wanauliza swali la kijinga kama Mungu alishuka duniani , mbinguni alibaki nani ( watakaouliza hivi na wenyewe tuwaulize Mungu anawezaje kusikia mtu aliyepo singida , mwingine austaralia , Mwingine india?) hivyo basi jibu Mungu ni muweza wa yote na anaweza kuwa kote muda wote. Tusiulimit uwezo wa Mungu kwa uwezo mwanadamu wa kuwepo eneo moja kwa wakati mmoja.
Yesu alipomaliza mission yake akaondoka, alipoondoka akasema Roho mtakatifu atachukua hatamu.
Roho mtakatifu ni roho wa Mungu, anatufundisha na anatuongoza hapa duniani baada ya Mungu kuondoka inform of a human.
Yesu= Mungu alipokuja kama mwanadamu na ndio neno la Mungu
Roho mtakatifu= Roho wa Mungu/Jehovah ambaye hata hapa duniani ukiamua kusali utamsikia kabisa akikuongoza katika mambo mbalimbali
Mungu Baba= Jehovah/Yahweh
hivyo utatu ni simple kuelewa.... 1×1×1=1