Aaron Ramsey
Member
- Jan 2, 2014
- 44
- 6
Aiseee, pole sana kijana!
Binafsi sijaona kosa lako, na umefanya vizuri tu kusema. Nadhani walioharibu huu uzi ni wachangiaji badala ya ku stick kwenye kutoa ushauri wame-base kwenye ubashiri na kufukunyua mengine.
Kwa kuongea na kusema yalio moyoni mwako umejipa uhuru wa akili na kuondoa hasira zako kifuani, ushayatoa ya moyoni relax endelea na maisha yako tu. Usiangalie ulipotoaka, angalia unapo elekea ndio iko na umuhimu kwa sasa.
Insinuation na speculation zetu sisi wachangiaji tuziache. Sidhani kama kuna faida sana kumjua mhusika wa pili. Japo najua alipo sasa atakuwa kajawa na hasira manake kwa mleta mada kusema ya moyoni kajiondolea tatizo, sasa huyo binti atakuwa na hasira za kuletwa hapa nae atafute pa kusemea ya moyoni awe huru kiakili na kuondoa hizi stress.
Kucheza na hisia ni mbaya sana, seriously na hivi inakuwaje kutongozana mitandaoni? Mbona social na public centre ziko mob tu mnafanya meeting na ku-date! Hizi cheap relationship za mitandaoni ndio cost yake hii.
Ma phyico na serial killer wanatengenezwa hivi hivi kwa visa vya ki.pu.mbavu kuumizana kwenye mapenzi bila sababu za msingi. Hata kama mtu haja meet yo standard au hajafikia criteria zako kuna better way ya kum-push back!
Poleni sana...wote msichana na mvulana. Wote mko kwenye majanga ya kimapenzi. Tafuteni pa kusemea muondoe hasira na muwe na akili huru za kuweza kupenda na kuamini kwenye mapenzi ya kweli.
Sent from my WhiteBerry using JamiiForums
Safi sana kwa mchango wako