Nani anaiongoza CCM?

Zamani kulikuwa na chama cha mapinduzi; uongozi wake ulikuwa hauna utata, maamuzi yake yalikuwa yanaeleweka (hata kama hayapendwi), na mwelekeo wake kiitikadi ulikuwa wazi kabisa. Chama hicho cha zamani hakikuona haya au aibu kusema kuwa ni chama cha kimapinduzi chenye kutaka kujenga taifa la "watu walio huru na sawa".

Ndani yake kulikuwa na nidhamu ambayo ilitokana na kuelewa kuwa uongozi wake hauna utata na kama chama hawakuweza kuona haya kumchukulia mtu yeyote ambaye alikuwa ni tatizo kwa Taifa au kwa chama. Hivyo tangu enzi za TANU maamuzi magumu yalifikiwa na mengine yaliwagusa watu ambao waliaminika kuwa wana nguvu.

Ilipotishiwa uhaini hakukuwa na utata hata marafiki walishukiwa!

Ilipotishiwa Muungano hawakuwa na utata hata Makamu wa Rais na Rais wa Zanzibar na baadaye Waziri Kiongozi wote hawakuonewa haya.

Ilipotishiwa uhujumu wa uchumi hakukuwa na utata wa nini kifanyike (japo baadaye baadhi ya kesi ziligeuzwa na mchakato kuboreshwa). Hakukuwa na utata hata hivyo wa nani atachkua hatua!

Chama kweli kilikuwa kimeshika hatamu ya uongozi. Leo hii chama hiki kipya kilichoko madarakani, hakina mwelekeo, hakina itikadi, hakina maono ya mafanikio na kimebakia kama picha ya zamani iliyojawa na vumbi la ufisadi. Kimebakia kuwa chama cha kuangaliana, kukodoleana, kubezena, kutukanana, na sasa imefika mahali kuwa chama cha kusakamana!

Hakina tena hatamu za uongozi isipokuwa utamu; hakina kujitegemea bali kimebaki na kujimegea, hakina ujamaa tena bali kimebakia na utamaa! Ndiyo CCM hii siyo ile ile, zimebakia rangi za kijani, njano na nyeusi! Uongozi wake butu, mwelekeo wake hupo, na malengo yake yamebakia vitabuni!

Ndiyo, CCM haina uongozi tena unaoongoza, bali kinaongozwa na viiongozi wanaoongozwa na matukio! CCM hii haijui nchi yetu ni nchi ya mrengo gani na tunataka kujenga taifa la namna gani! SAsa hivi chini ya CCM hii ninachoshuhudia ni mambo kwenda mrama!

Taifa liko mashakani, hatima ya watu wetu matatani, na kwa hakika toka mbali kama kwenye ukungu hivi naweza kuona mahali ambapo ule unabii niliondika habari zake miaka mitatu uliyopita unazidi kutimia kwa haraka zaidi. Na wanaoutimiza ni wana CCM wenyewe!

CCM pole pole inaanza kusimamishwa kizimbani! Kizimba cha maoni na fikra za watu! Je itakutwa na hatia? Na ni nani anaiongoza! Je Kikwete ameishindwa?

Je, ipo haja ya haraka kwa Rais Kikwete kuitisha MKUTANO MAALUM WA HALMASHAURI KUU YA TAIFA?

MKJJ You nailed it,na ndio maana wengine tunapata shida kumtetea Mwakyembe moja kwa moja kutokana na hilo,Mwakyembe na wazalendo wengine inabidi wawe makini sana kwasabab wanaweza kuwapa mafisadi nguvu zaidi kwani ufisadi ndio nguvu ya ccm na wakibadilisha direction means tutapata maendeleo hilo halina siri,tatizo ni kama wako addicted sasa na ufisadi kwasababu wananchi hawawawajibishi wanasiasa mafisadi...Kama MK anaelewa hilo na anajua hawezi kuibadilisha ccm,then whats next?
 
F. Kuweka utaratibu wa kuwa na serikali ya mseto.

N.k

This is best MKJJ

Lakini kwa CCM! wasivyowaza uzalendo, hii kitu wakiweza kufanya, siku hiyo hiyo mitume wote watafufuka na tutawaona Tanzania!, achilia mbali kumwona Nyerere na Sokoine wakikatiza mitaa ya kariakoo! Usiseme kuhusu wanyama mbalimbali kubehave differently, na nature kushtuka kutokana na mtikisiko wa mapinduzi!
 
Mkuu MMKJ, ningekuwa mwanasisiemu, ningekutunza kwa jinsi unavyoipigia chapuo kuhakikisha nyumba inakaa sawa kabla ya 2010. Kwa vile pia siyo mwanachama wa chama chochote, nitaunga mkono chama chochote kitakachopigania ustawi wa taifa. Kazi elekezi unayokifanyia chama. Thanks.

CCM unayoizungumza wewe, ni CCM ya enzi za chama kushika hatamu, 'party supremacy'. Mfumo wa vyama vingi ulipoanza, tumekuja kupata 'the executive supremacy' sasa tuko katika safari
Ya kuelekea Bunge kushika hatamu 'legistlature supremacy' which is one step short of the real power which is 'peoples power'
'Vox Populi is vox Dei'. Party is nothing where we go. Ila katiba yetu kandamizi inayokwenda kinyume cha Azimio la Haki za Binaadamu kwa kusisitiza kipengele cha vyama.

Inavyoshauri CCM ijirekebishe ni dalili ya wazi kwamba, there is no altenative, ndio maana huko nyuma nimewahi kusema, CCM imekuwa ikishinda kwa kishindo na itaendelea kushinda kwa vishindo sio kwasababu ni mzuri sana, ama inapendwa sana, bali
watu wanaipigia kura kwa sababu hawaoni mbadala, nashukuru hilo nawe umeliona na ndio maana unawasaidia kuweka nyumba safi kabla mgeni '2010' hajafika, na akishaondoka, ni kuendelezwa kwa uchafu ule ule kumsubiria mgeni mwingine '2015.

Na mwisho kumbukumbu yangu sio nzuri sana, ila ninachokumbuka yale maneno 'Tanzania ni nchi ya Kijamaa yaliwekwa mpaka kwenye katiba, hivyo ni above party politics. Kama yaliondolewa, then I support you CCM wayaondoe ili mzimu wa Baba wa Taifa uwashukie na lile neno lake la upinzani wa kweli litimie, na watu wapate altenative.

Mungu ibariki Tanzania.
 
Na mwisho kumbukumbu yangu sio nzuri sana, ila ninachokumbuka yale maneno 'Tanzania ni nchi ya Kijamaa yaliwekwa mpaka kwenye katiba, hivyo ni above party politics. Kama yaliondolewa, then I support you CCM wayaondoe ili mzimu wa Baba wa Taifa uwashukie na lile neno lake la upinzani wa kweli litimie, na watu wapate altenative.

Mungu ibariki Tanzania.

Kumbukumbu yako iko sahihi.. "Tanzania ni nchi ya kijamaa" inatamka Katiba...
 
Mimi si mwanachama wa CCM wala chama chochote bali ni mwanachama wa ''jamiiforums''.

Ila ninaona kwamba CCM haina aneiongoza kwa maana kwamba katiba ambayo nde kiongozi wa chama hicho haijakaa sawa kwa kuzingatia umri na mabadiliko ya kidunia kwa sasa.

Lakini wakati huohuo katiba hiyo katika sura yake ya sita ibara ya pili ina SEKRETARIETI YA MAADILI YA VIONGOZI WA UMMA ambayo siku nyingi ingeweza kushughulikia suala la MAFISADI na wahujumu wengine wa uchumi.

Sasa njia pekee ni mkutano mkuu wa dharura wa halmashauri kuu ya taifa utakaoto azimio la kuifanyia marekebisho katiba.
 
- CCM haina kiongozi? Sasa tumeshindaje ubunge Mbeya bila ya kua na kiongozi? Eti huko upinzani mna viongozi? Nani Zitto na Lipumba? Au Mrema na Mtikila? Kwa viongozi kama hawa CCM tunahitaji viongozi? Wa nini hasa?

- Wakuu CCM tuko sawa, tunajua malumbano ya kidemokrasia huwa ni adimu sana kwetu Tanzania, kwa hiyo naona we are reading too much katika demokrasia inayoendelea sasa hivi ndani ya CCM.

- Tuna matatizo ya kuwa na baadhi ya viongozi wabovu na sasa malumbano haya ndio wmazo wa kuwafikia, regardless ya who is talking too much soon tutakaa chini na viongozi wabovu wataumbuliwa, kama vile tulivyomuumbua Mbunge wa wetu wa zamani Nyimbo, tunao utaratibu wa ku-deal na uovu ingwa tumekuwa very slow sometimes,

- Otherwise, we are just fine, sijui huko upande wa pili kuna nini hasa Sangara au Dowans? Wakuu tuongee alternative sio majungu majungu, maana wananchi sio wajinga tena, kwenye haya malumbano ukweli unajiweka kando na tunauona wazi and very clear, nani ni nani,

- Wa-Tanzania sio mabwege tena! Tusipojua kuheshimu vyama vya wengine vya siasa tutaheshimu vipi vya kwetu? Tusipojua kuheshimu viongozi wenzetu wa chama kimoja tutajiheshimu vipi sisi wenyewe na wananchi? Tusipoheshimu maagizo ya vyama vyetu vya siasa, tutaheshimu vipi maagizo ya wananchi na taifa lao?

We are all together int his boat, kusema CCM haina viongozi ni matusi kwetu wanachama wa CCM na it is unacceptable! Tunaweza kujadili matatizo ya vyama vyetu vya siasa yanajadilika, lakini sio matusi kama haya kwamba eti CCM hakuna kiongozi, tusichanganye heshima na uoga ni vitu viwili tofauti sana!

Respect!

Wazee wa sauti ya umeme FMEs!
 
CCM haina uongozi! kama hili ni tusi basi nalirudia kwa furaha. CCM haina uongozi kama iliyowahi kuwanao. sasa hivi wamebaki kuburuzana. Wapinzania na wenyewe wana matatizo yao na ya uongozi ni mojawapo tu. Hata hivyo, wapinzani hawanisumbui kichwa changu kwani hawaongozi nchi na hatima ya Taifa haiko mikononi mwao. CCM ndiyo wahusika wakuu.

CCM wamebakia kuwa na SIUONGOZI!
 
- CCM we are fine, kwa sababu hakuna upinzani, mpaka siku utakpopatikana upinzani wa kweli then CCM tutajirekebisha, not now kwa sababu ni clear kwamba sisi wananchi tumeshindwa kujenga upinzani, tunasubiri somebody aje atujengee huku tukilaumu tu bila kufanya anything serious, angalau hata Mrema asiyekuwa na elimu kubwa alijitahidi, sisi wenye elimu kubwa ndio haya!

- Wakuu tukazane tuingie wenyewe huko ndani, hakuna tena wa kutufanyia tukabadilishe wenyewe!

FMES!
 
JK na wana-mtandao wenzake waliitumia CCM kuingia madarakani,na hawana muda na hilo dude (CCM) hata likimomonyoka kesho.Wameshachuma vya kutosha,na hata ikitokea 2010 wakashindwa kumnadi JK kwa fedha zao za kifisadi basi wana uhakika wa kuishi maisha ya kipeponi kama Mkapa.

CCM itaendelea kufanya madudu kadri inavyotaka simply because inafahamu kuwa Watanzania bado hawajaamka (with exception ya fraction ndogo inayojitahidi kupiga kelele).Mpaka hapo watawaliwa watakapoamua kuonyesha (sio kusema tu) kuwa enough is enough (kama Madagascar) tusitegemee chochote kutoka kwa CCM.
 
- CCM haina kiongozi? Sasa tumeshindaje ubunge Mbeya bila ya kua na kiongozi? Eti huko upinzani mna viongozi? Nani Zitto na Lipumba? Au Mrema na Mtikila? Kwa viongozi kama hawa CCM tunahitaji viongozi? Wa nini hasa?

- Wakuu CCM tuko sawa, tunajua malumbano ya kidemokrasia huwa ni adimu sana kwetu Tanzania, kwa hiyo naona we are reading too much katika demokrasia inayoendelea sasa hivi ndani ya CCM.

- Tuna matatizo ya kuwa na baadhi ya viongozi wabovu na sasa malumbano haya ndio wmazo wa kuwafikia, regardless ya who is talking too much soon tutakaa chini na viongozi wabovu wataumbuliwa, kama vile tulivyomuumbua Mbunge wa wetu wa zamani Nyimbo, tunao utaratibu wa ku-deal na uovu ingwa tumekuwa very slow sometimes,

- Otherwise, we are just fine, sijui huko upande wa pili kuna nini hasa Sangara au Dowans? Wakuu tuongee alternative sio majungu majungu, maana wananchi sio wajinga tena, kwenye haya malumbano ukweli unajiweka kando na tunauona wazi and very clear, nani ni nani,

- Wa-Tanzania sio mabwege tena! Tusipojua kuheshimu vyama vya wengine vya siasa tutaheshimu vipi vya kwetu? Tusipojua kuheshimu viongozi wenzetu wa chama kimoja tutajiheshimu vipi sisi wenyewe na wananchi? Tusipoheshimu maagizo ya vyama vyetu vya siasa, tutaheshimu vipi maagizo ya wananchi na taifa lao?

We are all together int his boat, kusema CCM haina viongozi ni matusi kwetu wanachama wa CCM na it is unacceptable! Tunaweza kujadili matatizo ya vyama vyetu vya siasa yanajadilika, lakini sio matusi kama haya kwamba eti CCM hakuna kiongozi, tusichanganye heshima na uoga ni vitu viwili tofauti sana!

Respect!

Wazee wa sauti ya umeme FMEs!

Wazee wa Sauti ya Umeme FMEs! Respet mkuu na Taratiiiiiiiiiiibu ndiyo mwendo tunakaribia kufika.

Swali la Msingi ambalo hoja ya Mwanakijiji imejikita ni 'Nani anaiongoza CCM'?
Sidhani kama MMM alikuwa akimaanisha CCM haina Viongozi, ina Mwenyekiti, ina Katibu Mkuu, in Katibu Mwenezi ina Makamu Mwenyekiti na Viongozi wengine.

asante
 
Wazee wa Sauti ya Umeme FMEs! Respet mkuu na Taratiiiiiiiiiiibu ndiyo mwendo tunakaribia kufika.

Swali la Msingi ambalo hoja ya Mwanakijiji imejikita ni 'Nani anaiongoza CCM'?
Sidhani kama MMM alikuwa akimaanisha CCM haina Viongozi, ina Mwenyekiti, ina Katibu Mkuu, in Katibu Mwenezi ina Makamu Mwenyekiti na Viongozi wengine.

asante

- Then angesema kwanza Upinzani unaongozwa na nani, alinganishe na CCM ili kuipa hoja nguvu ya kielimu, badala ya maneno ya mtaani. Kwa sababu CCM tunao viongozi wetu tuliowachagua tena kwa kura.

FMES!
 
- CCM we are fine, kwa sababu hakuna upinzani, mpaka siku utakpopatikana upinzani wa kweli then CCM tutajirekebisha, not now kwa sababu ni clear kwamba sisi wananchi tumeshindwa kujenga upinzani, tunasubiri somebody aje atujengee huku tukilaumu tu bila kufanya anything serious, angalau hata Mrema asiyekuwa na elimu kubwa alijitahidi, sisi wenye elimu kubwa ndio haya!

- Wakuu tukazane tuingie wenyewe huko ndani, hakuna tena wa kutufanyia tukabadilishe wenyewe!

FMES!
2010 mkuu una kura yangu usinisahau kwenye ukurugenzi.....
 
Wazee wa Sauti ya Umeme FMEs! Respet mkuu na Taratiiiiiiiiiiibu ndiyo mwendo tunakaribia kufika.

Swali la Msingi ambalo hoja ya Mwanakijiji imejikita ni 'Nani anaiongoza CCM'?
Sidhani kama MMM alikuwa akimaanisha CCM haina Viongozi
, ina Mwenyekiti, ina Katibu Mkuu, in Katibu Mwenezi ina Makamu Mwenyekiti na Viongozi wengine.

asante
Hoja hujibiwa kwa hoja

- Then angesema kwanza Upinzani unaongozwa na nani, alinganishe na CCM ili kuipa hoja nguvu ya kielimu, badala ya maneno ya mtaani. Kwa sababu CCM tunao viongozi wetu tuliowachagua tena kwa kura.

FMES!
 
CCM haina uongozi! kama hili ni tusi basi nalirudia kwa furaha. CCM haina uongozi kama iliyowahi kuwanao. sasa hivi wamebaki kuburuzana. Wapinzania na wenyewe wana matatizo yao na ya uongozi ni mojawapo tu. Hata hivyo, wapinzani hawanisumbui kichwa changu kwani hawaongozi nchi na hatima ya Taifa haiko mikononi mwao. CCM ndiyo wahusika wakuu.

CCM wamebakia kuwa na SIUONGOZI!

I always admire boldness yako on things you belive, ila pia kuelekea 2010, jihadhari sana na malumbano na ma opportunists watakaoimba nyimbo za shangwe na mapambio kuhusu CCM kwa sababu maalum, ila naamini ukweli wanaujua.
 
..CCM ukiwa mpinzani na wakijua ni tishio kwao,basi watatumia serikali yao ya kifisadi na vyombo vyake kukunyasa,kukusingizia kuanzia kodi mpaka uhaini na kukuweka ndani...yaani hakuna haki kabisa na hawa wapuuzi ndio maana nchi inazidi kuwa maskini tuu kila siku,dawa yao ni kuwamaliza mafisadi ndani ya chama chao na kukivunja vunja kama KANU,naanza kuamini upinzani wa kweli lazima uanzie ndani ya CCM au lazima wapinzani wawe na strategy za kukamata maeneo fulani kwanza kabla ya nchi nzima,najua wapinzani wakicheza kadi zao vizuri sehemu za Dar,Mwanza,Arusha,Mbeya,Kigoma na Mara CCM najua wanaweza kupigwa nje kirahisi sana
 
Koba mkuu, signature yako nimeiona... kwikwikwiiii!
Hata mimi nimechoka na CCM kuimba wimbo huohuo eti wapinzani hawana uongozi lakini ukiwaambia Dr Slaa atawajadili kesho hadharani utasikia wanavyohaha kutaka kujua kama wamo! Waache walale! Maana wana dharau Operesheni Sangara lakini matokeo yake watakiona. Kwani hawajaona Kikwete alivyopopolewa mawe Mbeya? Wanafikiri ni dalili ya nini? Rais wa nchi anapopolewa mawe? Wananchi wamesha-loose all respect for them. Narudia tena, let them sleep!
 
..CCM ukiwa mpinzani na wakijua ni tishio kwao,basi watatumia serikali yao ya kifisadi na vyombo vyake kukunyasa,kukusingizia kuanzia kodi mpaka uhaini na kukuweka ndani...yaani hakuna haki kabisa na hawa wapuuzi ndio maana nchi inazidi kuwa maskini tuu kila siku,dawa yao ni kuwamaliza mafisadi ndani ya chama chao na kukivunja vunja kama KANU,naanza kuamini upinzani wa kweli lazima uanzie ndani ya CCM au lazima wapinzani wawe na strategy za kukamata maeneo fulani kwanza kabla ya nchi nzima,najua wapinzani wakicheza kadi zao vizuri sehemu za Dar,Mwanza,Arusha,Mbeya,Kigoma na Mara CCM najua wanaweza kupigwa nje kirahisi sana

Muongo wewe....
 
Back
Top Bottom