Nani aliyemuumba Mungu?

Nani aliyemuumba Mungu?

Tumia akili japo kidogo kufikiri kwamba mtu anadai kuwa kitu fulani hakipo, sasa tutawezaje kujua kuwa anachosema ni kweli?
Mfano umekuja kwangu halafu haujanikuta .. Kisha umerudi kwako mkeo akakuuliza hearly yupo ukamjibu hayupo halafu yeye akakuambia kuwa nipo ...unadhani ni nani kati yenu atakaye paswa kuthibitisha kuwa nipo ni wewe ambaye umekuja kwangu halafu umekuta sipo au yeye anaye ng'ang'ania kuwa nipo?

Kitu ambacho hakipo kinathibitishwa vipi kuwa hakipo ??

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Uthibitisho pekee ni kutokuonekana kwa mungu,kutokujulikana kwa mwanzo na mwisho wake na kutokujulikana muonekano wala umbo lake,lakini kama angekuwa anajulikana katika hayo basi asingekuwa Mungu tena.
Kwanini una amini kutokuonekana na kutojulikana kwake ndio uthibitisho?
 
Mwanzo kabisa niliandika allah ni pepo ambalo limeumbwa na Othman.

Sikubahatisha, kwanza Othman ndiye kaitengeneza hiyo koran unayoitumia sasa tatu katengeneza hizo blunder mbili kwanza ziko tatu moja nimeiweka kiporo.

Mungu aliyehai hawezi kufanya hizo blunder ni jini pekee.
Wewe unaamini cha kwanza kuumbwa ni kalamu? Unaamini Mungu anakaa kwenye wingu? Rubbish!
.
Nikijadili kama GT sasa allah ni pepo tu na pepo always huwa ni muharibifu hajengi anabomoa.
Imani yako imeanza na kubomoa kilichokuwepo na kuleta kitu kipya hiyo ni sifa ya pepo.
Swali rahisi sana, labda kama una matatizi ya akili. THIBITISHA UNAYO YAANDIKA, UNASHINDWA.
 
Wewe umeweka hadithi au aya gani ya Qur'an inayosema kwamba Mtu YEYOTE anayehoji kuumbwa kwa Mungu ni Muongo na tapeli??

Unanitaka mimi nioe aya kwani mimi ndio nitoaye hayo madai??? -- wewe ndiye unayetakiwa kwanza kuthibitisha madai yako kwa aya na hadithi sahihi za Alrasulullah (saw) mbora wa manabii.


Namsubiri huyo teacher wako umlete hapa aje kujibu kwani haya ni maji marefu kwako.
Ina maana hujui unacho egemea sio ?

Mbona una yumba sana, hivi punde ulodai unamcheki mwalimu wangu tena umekuja unataka nikuletee mwalimu wangu.

Jana nimekuelezea jambo hili kwa wepesi sana, lakini ukaamua kuukataa ukweli na kujidao unaweza kujibu hoja zangu lakini mpaka muda huu hujajijibu, nikakwambia kosoa hoja unalalama.

Ndio maana nasema hivi, weka hoja sio unalia lia.
 
Kudai uthibitisho wa kitu ni kudai definition ya hicho kitu?!!
Ina maana mwenye kutaka uthibitisho wa kitu ni kwamba hakijui hicho kitu ni nini?
1. Inawezekana hakijui, na hapo definition ni sehemu ya uthibitisho, maana unaweza kuanza kuelezea kitu bila kuki define ikawa huja make sense.

2. Inawezekana anakijua, lakini anavyokijua yeye na unavyokijua wewe ni tofauti. Na hapo ni muhimu definition iwekwe vizuri ili kuondoa mapishano. Mfano, kama wote mnajua rangi nyekundu na blu ni ipi, lakini unayoita wewe nyekundu, mwenzako anaita bluu, na unayoita wewe bluu, mwenzako anaita nyekundu, mnaweza kuwa mnataja kitu kile kile, lakini kwa majina tofauti, au mnaweza kuwa mnataja vitu tofauti, kwa jina lile lile.

Hapo definition ni muhimu.

Chukulia mfano, mnafanya litmus paper test kuangalia acidity na alkalinity. Halafu wewe unachoita nyekundu, mimi naita bluu, na mimi ninachoita bluu, wewe unaita nyekundu.

Hapo tutabishana hata kama tunaona rangi ile ile. Wewe utaiita nyekundu, mimi nitaiita bluu.

Kwa nini? Kwa sababu hatuja define na kukubaliana nyekundu ni nini na bluu ni nini.

define Mungu ni nini, kisha, thibitisha Mungu yupo.

Unaweza kum define Mungu wako ni ng'ombe kama wahindi, au ni gravity.

Ukimdefine Mungu wako hivyo, siwezi kukubishia kwamba yupo, katika muktadha huo.

Kwa sababu ng'ombe yupo, na gravity ipo.

Ili mjadala uwe na maana, inabidi u define Mungu ni nini kwanza. Halafu uthibitishe yupo.

Bila hayo, utakuwa unaendekeza ubishi usio msingi.
 
kosoa hoja unalalama.


Nitakosoa hoja mara ngapi??---

Nitarudia, Hoja ya msingi ni hii; sio sawa kumuita Muongo, Tapeli nk, Mtu YEYOTE anayeuliza; je Mungu kaumbwa??.

Kujua uongo au utapeli nk, wa mtu anayeuliza swali hilo ni kitu kilichojificha na Yule anayeweza kujua mambo yaliyomo katika nafsi ya mtu ni Alghuyyub yaani ni Allah pekee.

Anapotokea mtu na akajipachika hicho cheo cha Mungu huyo ni Mshirikina, anajifanya yeye ni Mungu, ameshirikiana na Mungu kwa uongo sifa isiyomuhusu na isiyomtosha.

Hakuna dhambi kubwa kuliko zote zaidi ya Ushirikina, mtu asipotubu dhambi ya ushirikina hapa duniani siku ya akhera Mungu anaweza kusamehe dhambi zingine ila kamwe hasamehi dhambi ya ushirikina, ni lazima atakuadhibu tu.

Upo hapo???, mwambie huyo mwalimu wako uliyemficha aache Ushirikina.
 
Nitakosoa hoja mara ngapi??---

Nitarudia, Hoja ya msingi ni hii; sio sawa kumuita Muongo, Tapeli nk, Mtu YEYOTE anayeuliza; je Mungu kaumbwa??.

Kujua uongo au utapeli nk, wa mtu anayeuliza swali hilo ni kitu kilichojificha na Yule anayeweza kujua mambo yaliyomo katika nafsi ya mtu ni Alghuyyub yaani ni Allah pekee.

Anapotokea mtu na akajipachika hicho cheo cha Mungu huyo ni Mshirikina, anajifanya yeye ni Mungu, ameshirikiana na Mungu kwa uongo sifa isiyomuhusu na isiyomtosha.

Hakuna dhambi kubwa kuliko zote zaidi ya Ushirikina, mtu asipotubu dhambi ya ushirikina hapa duniani siku ya akhera Mungu anaweza kusamehe dhambi zingine ila kamwe hasamehi dhambi ya ushirikina, ni lazima atakuadhibu tu.

Upo hapo???, mwambie huyo mwalimu wako uliyemficha aache Ushirikina.
Hujakosoa hata sehemu moja na huna uwezo huo.

Simchezo, naona una rula rula ulianza kwenye kupewa kiswahili cha Sophist, ukaja kwenye bida'a nao a umeamua kuja kwenye Ushirikina, ambao huwezi kuthibitisha hilo. Ushirikina wake uko wapi ? Nimekuuliza hili swali,najua huwezi kulijibu ila naonyesha ujinga wako ulipo.

Nakuacha na swali hili, USHIRIKINA ni nini ?

Huna hona, umeamua kuwazulia watu UONGO sasa.

Nipo...
 
Sasa muda wote ulikuwa unajadili nini humu ikiwa uzi unahusu Mungu na wewe hujui kabisa Mungu ni kitu gani hujawahi kusikia hilo neno?

Yani kwahiyo kumbe muda wote ulikuwa unajadili kitu ambacho hukijui kabisa.
 
Mfano umekuja kwangu halafu haujanikuta .. Kisha umerudi kwako mkeo akakuuliza hearly yupo ukamjibu hayupo halafu yeye akamuambia kuwa yupo ...unadhani ni nani kati yenu atakaye paswa kuthibitisha kuwa nipo ni wewe ambaye umekuja kwangu halafu umekuta sipo au yeye anaye ng'ang'ania kuwa nipo ??

Kitu ambacho hakipo kinathibitishwa vipi kuwa hakipo ??

Sent using Jamii Forums mobile app
Mie sijauliza ni nani anayetakiwa kuthibitisha kati ya anayesema kipo na anayesema hakipo, nimeuliza kuwa tunawezaje kujua ukweli wa madai ya mtu anayesema kitu fulani hakipo?

Mfano mie niseme nimetoka kwa hearly kwake sikumkuta hayupo, je watu watawezaje kujua kuwa nachosema ni kweli? Au kwamba itakuwa nachosema kinakuwa ni kweli hadi itokee mtu wa kupinga?
 
Sasa muda wote ulikuwa unajadili nini humu ikiwa uzi unahusu Mungu na wewe hujui kabisa Mungu ni kitu gani hujawahi kusikia hilo neno?

Yani kwahiyo kumbe muda wote ulikuwa unajadili kitu ambacho hukijui kabisa.
Kuna mtu nlimuazima simu Nimekuta jamaa alikuwa anatumia id yangu.
Anyways acha chenga za pele
Mungu ni nini?
 
Mungu yupo hakuumbwa bali yeye ndie muumbaji wa kila kitu kile tunachokijua na tusichokijua.
Hana mwanzo wala mwisho,hana mfano wa kitu chochote,hajulikana umbo wala muonekano wake.
Mungu yupi huyo hajulikani umbo?
Mungu wa wahindu ni ng'ombe
Mungu wa waarabu ana mguu mmoja na mikono miwili upande mmoja
 
Kuna mtu nlimuazima simu Nimekuta jamaa alikuwa anatumia id yangu.
Anyways acha chenga za pele
Mungu ni nini?
Huwa sipendi maswali yasiyo na msingi na ndiyo hizi mada huwa hazina mafanikio kila siku tunarudia palepale, haiwezekani wewe uanze kujadili mada toka huko mwanzo halafu et sasa ndio useme hujui maana ya kitu unachokijadili. Bora ungekuwa na shida na definition ya Mungu maana wakati mwengine watu hutofautiana kwenye definition za maneno ila wewe unasema hujui kabisa hilo neno na ndio mara yako ya kwanza kusikia
 
Hujakosoa hata sehemu moja na huna uwezo huo.

Simchezo, naona una rula rula ulianza kwenye kupewa kiswahili cha Sophist, ukaja kwenye bida'a nao a umeamua kuja kwenye Ushirikina, ambao huwezi kuthibitisha hilo. Ushirikina wake uko wapi ? Nimekuuliza hili swali,najua huwezi kulijibu ila naonyesha ujinga wako ulipo.

Nakuacha na swali hili, USHIRIKINA ni nini ?

Huna hona, umeamua kuwazulia watu UONGO sasa.

Nipo...



Hapa ndipo hupawezi kabisa, elimu yako ni ya; Muulizaji anakuwa tapeli na muongo nk, na elimu ya majini- mbwa na majini--paka shume.

Na usitake kubadilisha mada kijanja, tupo hapo hapo kwa nyie mnojifanya Miungu kujua yaliyomo ndani za nafsi za kila YEYOTE aulizaye kuhusu kuumbwa kwa Mungu eti, ni lazima awe muongo, tapeli nk!!!🤣

Mnataka watu wasiwe wanahoji kama jinsi nyinyi akili zenu zilivyokuwa dormant kwa kutokuhoji mnataka na za wengine ziwe hivyohivyo!!

Sasa bila kuhoji na kutafakari akili itafanya kazi gani??-- Allah mara kadhaa anauliza; A falaa ta'akiluun?? Yaani; je hamtumii akili??--- sasa kuuliza kutaanza vipi bila kutumia akili??, na unapouliza au kujiuliza ndipo unakwenda mbele zaidi kwenye tafakur.

Nyie ni watu wa ajabu kweli, mnataka watu wawe mabubusa kama nyie.
 
Back
Top Bottom