Namuacha mpenzi wangu kisa DP WORLD

The only

JF-Expert Member
May 19, 2011
10,435
13,421
Habari waungwana!

Baada ya familia kunikomalia nioe nikaona nianze msako ,dada yangu mmoja ni lecturer akanilengeshea kwa ka mwalimu ka sekondali (jina kapuni) Basi baada ya kutumiwa picha akaomba tuonane .
Vigezo alivonivutia

1.Mwanadada ni muwazi kupitiliza sijui umuulize nini ajibu uongo hata kama kitamuharibia yy,mfano nlitonywa kuna mwamba ambae ni mtu mbad shule ya jirani yuko naye ,kumuuliza sio tu alikubali bali alinifungulia chat zao zote ,mpaka mwamba kuniponda sana kuwa nakula hadi ambiance ,nikaamua kuwa muwazi pia nkamwambia ukweli mm sifai ila naomba nipime.

2.Nikaanza mtambulisha kwa washikaji na ndugu kwa kweli kwenda kwa dadangu mkubwa (ndo kanilea ) alijipatia baraka hadi dada akangangania alale pale mm nisepe

3.Kukomaa na kupima ngwengwe (hapa nusu nitoke nduki ila nimetoboa) mtoto namzidi 7 yrs maana ana 27 ila kiwango cha maturity hadi naogopa kabisaa,ameshanishauri sana hadi biashara zangu ashaenda hadi duka langu moro na kukagua akakuta madudu kibao .

4.Kitandani ni tatizo kuu la kimkakati mtoto anamwaga miuno kama yondo sister ,alikuwa hajawahi fika mitaa ya katelelo pale bukoba nimempeleka kachanganyikiwa

KASORO KUU NA KUU SANA

Muda wote huu nilikuwa nashukuru muumba nimekumbukwa mpaka nkaacha kwenda maeneo ya kihuni ,siku moja akaniambia nimpitie karimjee wanamkutano na wenzie tuende lala kwake .LOOOOHH nusu nizimie ,kumbe sikujua dada ni mwnachama wa ChiChieMu ,Si katoka na majezi yao ya kijani ile midela na kikundi cha wenzie wakiimba '' ....mbele kwa mbeleeee'' nilimchukua hadi hoteli ya karibu na kumuuliza swali moja tuu '' NINI MSIMAMO WAKO JUU YA ISHU YA BANDARI '' Asee aliitetea balaa hajui muda huo nilikuwa nikishukuru muumba kwa kuniondolea huu msiba.

Hapa leo siku ya pili sipokei simu yake sitaki hata kumuona shetani mkubwa huyu.
 
Back
Top Bottom