gfsonwin
JF-Expert Member
- Apr 12, 2012
- 18,272
- 20,714
- Thread starter
- #81
Mnajuana wenyewe bana, maana siku hizi shetani anajiinua sana hata kama mtu ana kakidumu kakumliwaza hawezi kushindwa kuandika haya...samahani lakini. Hii imenikumbusha nikiwa chuo somewhere kuna dada nilikuwa nimejitambulisha mpaka kwao for marriage. Alikuwa ananiandikia E-mails hizo mpaka sasa nime-zi save na kibaya zaidi mpaka rafiki zangu walikuwa wanamuonea huruma jinsi anavyopata taabu kutokuwa karibu nami, lakini baadaye nikaja ku-porve beyond reasonable doubt kwamba ananiibia.
Dah Mwalimu gfsonwin kwanza hongera sana kwa kufikisha huu umri mrefu wa ndoa yako na bado ukaendelea kutamani kuendelea kuwepo kwenye ndoa yako. Ni wengi ambao wapo ndani ya ndoa ila ukiwauliza ni nini wanachotamani wangeweza kukuambia ni kuvunjika kwa ndoa zao kila mmoja ashike njia yake ila kwako hongera sana kwa kuwa bado una ule upendo wako wa kwanza wa siku za uchumba na siku za mwanzo wa ndoa yako. Hongera sana sana
Natamani tulio kwenye ndoa tungekuw ana ujasiri kama huo kusema wazi namna tulivyowamiss wapendwa wetu namna umbali uliopo kati yetu na wao unavyotuumiza na namna tunavyowapenda. Nahisi huko waliko wanajisikia vyema sana wakiambiwa kuwa wanapendwa na kuna mtu anawamiss sana.
Nichukue nafasi hii kukupongeza kwa kufikisha umri huu wa ndoa yako na naamini Mungu atazidi kuwajalia baraka zake na rehema zake katika kufanikisha mengi ya ndoa yenu na ikawe ya heri na baraka.
(off topic hata mimi nammiss sana my wife wangu popote alipo muda huu na namwambia nampenda sana)
Hongera sister kwa miaka 11 ya mafanikio.
Kuna wenzako wengine sasa hivi wanawaza kucheat jioni hii, au kuondoka kwenye ndoa
Ama kutafuta buzi ili aendeshe Vogue!
Ila nahisi haka kamsimu ka mvua kamechangia kwenye kumbukumbu yako hii. No no vidole vimeteleza
Kompyuta ya mchina hii.
Kwahiyo wewe uliolewa siku ya Jumapili??maana hiyo siku nakumbuka ndiyo siku yakwanza kuitwa Baba fulani!baada ya kuzaliwa mtoto wangu wa kwanza(ELLEN) alizaliwa siku hiyo asubuhi ya saa tano kasoro(010:45hrs) pale Hospitali ya Muhimbili kwa kufanyiwa Operation Marehemu mke wangu Mungu aiweke roho yake mahali pema Peponi Amina!!Nilikupenda na nitaendelea kukupenda japo kimwili haupo na mimi ila kiroho tupo pamoja!. gfsonwin kumbuka leo nitukio la pili kufanana katika maisha yako!
kidogo umejibu, ila ukubwa wa umri haihusiani kabisa na mihemko na ukifika umri wa ukubwani mihamu ndo inaongezeka sa we unawezaje kuhimili mikiki ya mihemko na mitongozo klein mtoe kabisa,na kuna zile siku zote yaaan hata kama yuko mbali utatamani umfate je umefanikiwaje kuzikabili au una njia mbadala?.
hahahahhhaha! babu nimeskype lakin bado.
kiu yangu nimuone nimguse, aniguse,
tukae mezani tule sote, tulale pamoja,
niwajibike kike juu yake like kumuandalia nguo kumtandikia kitanda
yaani utu tuvitu utu ndo nliotumiss kuvifanya juu yake.
huwaga vinaleta raha fulan, hebu pata picha bibi asbh anahangaika kukubrashia kiatu uvae na nguo kanyoosha unafkiri haskii raha??
nakwambia hivi vina raha kuliko hata ya mpera wenyewe.
Sorry ngoja niongezee......Wakati nikiwa mdogo my dady alikuwa ananitajia makundi ya wasomi wa kuoa na katika makundi yooote alikuwa anabaki saaana kwa waalimu na wauguzi....sijasema wengine sio wake la hasha haya yalikuwa masomo ya baba yangu mpendwa...to be in this group umenionyesha ni kitu gani baba alikuwa ananiambia....Nashukuru sikuteleza sana......Siku ya kutimiza miaka 11 usisahau kunijulisha ili nikutumie Card.thanks bro..........
Hahahahaahhahahah,
Wewe ni balaa Mr Rocky..!
Nimecheka sana..... kumbe kuna coincidence hata kwenye kumiss wake/waume....lol!!:yo:
Hii kwangu ndiyo aina ya great thinking...
Cheers bro platozoom
Hili linahitaji msaada wa Mungu na roho mtakatifu kulimeza mkuu .. KakaKiiza...
But, the Lord is a great and your only shepherd, will never let you alone.....Amen!
Hapa kuna maswali ya kiutu uzima .. ummu kulthum,
Labda tumwombe teacher gfsonwin atafute muda baada ya stress kupungua atudadavulie...
Ukisema hivi bwana unawaacha watoto wanaelea hewani....
Kwa zaidi ya muongo mmoja, teacher gfsonwin huwezi kusema umekosa kalufundi ka kukusaidia kumalizana na hayo ma-tention...
Ngoja niwaite wakubwa wenzangu hapa tusaidiane.....
Cc.. Bishanga, Asprin, Nyamayao, @FP, snowhite....
Babu DC!!
babu nimepigwa biti mimi!nimekaatu kimya!nimemuudhi sana leo kungwi wangu
kwanza kwa kuandikahapa tu tayari kashanuna!
ila mwali nisamehe tu japo wiki tu niruhusu!
Kwanza kabisa gfsonwin nikupe hongera kwa kumudu miaka 11 ndani ya ndoa na bado uko na matumaini makubwa juu ya mumeo jambo ambalo ni jema sana kwa ustawi wa familia yenu na fundisho kwa akina dada wengine wanaovamia ndoa baada ya siku mbili akikutana na changamoto anaanza kutafuta namna ya kusepa.
Pili nikutie moyo kwamba upweke ulionao ni wa kitambo kidogo tu kwakuwa wewe na mumeo mnatambua sababu ya kuwa mbali kwa muda huu na bila shaka panapo wakati muafaka atarudi na kujumuika nawe pamoja na wanenu.
Tatu, kama utaweza next time ikitokea siku kama hii imefika na haamko pamoja na mumeo jitahidini mmoja amfuate mwenzake alipo ili mnapokumbuka tukio adhimu la kuwaunganisha kuwa mwili mmoja mpate kuwa pamoja na kuunganika tena siku hiyo na kuwa mwili mmoja kama ishara ya kutumaini kuendelea kuwa pamoja hadi ukamilifu wa dahari
Bora na wewe umeona....
Hivi tulipowambia wababa kuwa ni marufuku kulia lia mbele za watu.....wadau wa upande wa pili tuliwambiaje??
Naomba unikumbushe.......
Kwa dizaini hii...wale wa miezi hadi mwaka watakuwa ICU....
Kweli ni mabadiliko ya tabia nchi yamemfikisha hapa mzee mwenzetu....??
Wapi FP na Kaizer??
Babu DC!!
Dah, safi sana!
Sikujua kama mwanamke anaweza akammis mwanaume kwa kiasi hiki (mpaka kusema mbele ya watu) as kila mwanamke anatongozwa tena kwa dizaini ya gfsonwin inakuwa maradufu!
Inavutia kujua wako wa aina hii, na si kila saa wanaume tuwe tunawafikiria vibaya wake zetu
Safi sana and Big up! Kwa kummis mwenzi wako