Namchukia sana Mama yangu

Nilipiga chini mtu kisa tu aliuliza mwanangu ataishi wapi, vi vema akae kwa mama yake au bibi yake.
Nikaona hii ni kenge maji.
Yaan hongera ulijiongeza mapema,,, ungelazimisha angemtesa sana mwanao
 

Unadhani mama yako alifanya vile kwa kupenda? mama yako ni mama yako huna mwingine.Fika mahali uachilie tuu.Unaweza usijue,inawezekana maisha uliyoyapata kwa bibi ni mama yako alikiwa anasupprt.
 
Ongea na mkeo chumbani, eleza hofu yako, eleza suluhisho kisha toa maamuzi.
Kisha mama atekeleze sehemu yake kwa kuongea na kijana bila kuleta matàtizo.
Ili eneo ndio jamaa hajatufafanulia vizuri. Je hayo maneno aliyasikia akiwa wapi? Inawezekana wazazi walikuwa wanaongelea chumbani, ila mtoto akawa anawasikiliza.
 
Kuna wamama huchagua wanaume kuliko watoto wao unalalaje na mtu hamtaki mwanao khaa
kuna wengine huchagua mali/vitu kuliko watoto wao, imagine mwanaume kasafiri kwenda kutafuta. huku nyuma mke kauza kila kitu cha ndani na kuwaacha watoto kwa jirani akiwemwo mtoto wa mwaka na miezi miwili.
 
Hiyo ndio duniani kila mtu anajali maslahi yake ,hapo mother wako kajali ndoa yake ila baadae akizeeka atakuja kudai umsaidie wakati alienda mbio.

Kila mtu anaangalia maslahi yake kwa wakati husika hata kuvunja ndoa wazazi watapata mbadala yule atao mwingine ataolewa,kimbembe kwa watoto ndio watapata tabu ila wazazi washatuliza nafsi zao.

Ukichunguza sana wazazi ni wanafiki sana tena watu wanaozaa kwa maslahi ,wakishazeeka basi mzigo unao haijalishi walikulea au lah...Hapo sasa kila mzazi anakaa kwake utoe msaada kwa wote wewe mmoja.
 
Mimi mwanzoni nilidhani mama ndiyo Kila kitu lakini nilivyoanza kuyaona maisha na kukaa sana na Mzee na kuchanganya akili zangu za kikubwa nikagundua kuwa kumbe mama nilikuwa nampa vyeo vingi sana hivyo basi nikaamua kuwa baba na mama nawapa wote vyeo sawa, yani 50/50 wote wawili.
 
Kutokukufinya ukiwa tumboni ama uzaliwapo ni dhahiri mama yako anakupenda,nani kama mama?
 
Hakuna bond kati yenu, ndio maana unafeel hivyo.

Kwa choices alizopewa, ilikuwa ni wazi wewe ndio wakuondoka. Unaweza kumlaumu ila jaribu kumuelewa. Usikae na kinyongo, jaribu kuflash ili maisha yaendelee.
Kabisa chief,
 
Hakuna mwanaume anaekubali kulea mtoto wa mwanaume mwenzie,, mshukuru bibi amekulea makosa uliopitia kwa wazazi wako hakikisha wewe unarekebisha. Hakikisha unachagua mtu sasa utakayeweza alie tayari kuhudumia na kulea wanao.
 
Hayo ni matumizi mabaya ya chuki.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…