Kwa hili, namsaidiaje binti yangu?

Kwa hili, namsaidiaje binti yangu?

min -me

JF-Expert Member
Joined
Jul 20, 2022
Posts
58,066
Reaction score
166,581
Niseme tu mimi ni single father wa binti mmoja , japo nilisha sema nawakiume mkubwa ila ni stori ndefu mpaka kufanya maamuzi ya kubaki na binti yangu tu.

Binti yangu nilianza kukaa nae alipo timiza miaka miwili baada ya kuvutana na mama yake mno.

Ila mama yake alipo pata mtu mwingine wa kumuoa ndoa kabisa, baada ya mimi kupeana nae talaka , ikawa rahisi sana kunipa binti yangu .

Nilimlea binafsi , alipo kua alienda kwa bibi yake na sasa yupo shule ya kulala anaendelea vyema.

Shida inakuja , baada ya binti ya kuwa mkubwa kiasi , naona kama hana bond na mama yake , wala hana hisia nae kabisa 🥲 , sikupenda hii hali ijitokeze kabisa , yani hata ukimwambia wewe unafanana na mama yako vitu fulani analia kabisa 🤔

Wakionana hauwezi fikiri ni mtu na mtoto wake , hii hali siipendi kwa sababu sijawahi kumsaigia kunguni mama watoto wangu kwa mwanae kabisa , tunaelewana kama wazazi na hata yeye ana shiriki matunzo ya mwenetu.

Hii hali imekaaje wadau , na nina weza fanya vipi nikaweka ukaribu wa binti yangu na mama yake 🤔.
 
bwashee, kwa ninavyoona Binti yako amejawa na chuki ya kuona mama yake alimtelekeza na kumuacha, hivyo hapo ni kuzidi kuwapa muda wa kuonana, kuzoeana zaidi ili hatimaye Binti yako apate nafasi ya kumkubali mama yake kwa mara nyingine, itachukua muda lakini italipa
 
Binti yupo shule ya "kulala"? Okay.Binti hana mapenzi na mamaye yawezekana sababu ni umbali/kutokuishi pamoja,mazoea au dokezo hasi kuhusu huyo mama kutoka kwa mtu mwingine.Unahitaji kumpanga kwa akili nyingi ili uwaunganishe wapatane.Au,tumia wataalamu wa saikolojia wamuweke relini.
ANGALIZO;Usilazimishe upendo umuingie mtoto kama roho mtakatifu na vilevile chunga usiharibu ndoa ya mzazi mwenzio kwa kung'ang'aniza upendo kwa binti yenu.
 
Binti yupo shule ya "kulala"? Okay.Binti hana mapenzi na mamaye yawezekana sababu ni umbali/kutokuishi pamoja,mazoea au dokezo hasi kuhusu huyo mama kutoka kwa mtu mwingine.Unahitaji kumpanga kwa akili nyingi ili uwaunganishe wapatane.Au,tumia wataalamu wa saikolojia wamuweke relini.
ANGALIZO;Usilazimishe upendo umuingie mtoto kama roho mtakatifu na vilevile chunga usiharibu ndoa ya mzazi mwenzio kwa kung'ang'aniza upendo kwa binti yenu.
Shida ya binti ni mbishi na ukizingatia mama yake ana watoto wengine wawili wa kike , hapa naona kama hataki kuelewa
 
Niseme tu mimi ni single father wa binti mmoja , japo nilisha sema nawakiume mkubwa ila ni stori ndefu mpaka kufanya maamuzi ya kubaki na binti yangu tu.

Binti yangu nilianza kukaa nae alipo timiza miaka miwili baada ya kuvutana na mama yake mno.

Ila mama yake alipo pata mtu mwingine wa kumuoa ndoa kabisa, baada ya mimi kupeana nae talaka , ikawa rahisi sana kunipa binti yangu .

Nilimlea binafsi , alipo kua alienda kwa bibi yake na sasa yupo shule ya kulala anaendelea vyema.

Shida inakuja , baada ya binti ya kuwa mkubwa kiasi , naona kama hana bond na mama yake , wala hana hisia nae kabisa 🥲 , sikupenda hii hali ijitokeze kabisa , yani hata ukimwambia wewe unafanana na mama yako vitu fulani analia kabisa 🤔

Wakionana hauwezi fikiri ni mtu na mtoto wake , hii hali siipendi kwa sababu sijawahi kumsaigia kunguni mama watoto wangu kwa mwanae kabisa , tunaelewana kama wazazi na hata yeye ana shiriki matunzo ya mwenetu.

Hii hali imekaaje wadau , na nina weza fanya vipi nikaweka ukaribu wa binti yangu na mama yake 🤔.

Ipe muda hii hali.

Ila kwa sasa Mama mtoto ashiriki kwa ukaribu (hata akiwa mbali) kwenye mambo/shughuli zinazomuhusu binti yenu ambazo zinaonekana mko sambamba mfano ( birthdays, kula Christmas pamoja, kwenda visiting day ww na Mama mtoto, pia Mama mtoto ampigie Binti kumuelekeza mambo ya Hedhi nk).

Binti huwa ni kipenz cha Baba.
Ila malezi mazuri anapata kwa Mama.
 
bwashee, kwa ninavyoona Binti yako amejawa na chuki ya kuona mama yake alimtelekeza na kumuacha, hivyo hapo ni kuzidi kuwapa muda wa kuonana, kuzoeana zaidi ili hatimaye Binti yako apate nafasi ya kumkubali mama yake kwa mara nyingine, itachukua muda lakini italipa
Hakumteleza mkuu, alivyopata ndoa , mimi ndio nikaona niupenyo wa kumchukua binti yangu na yeye akakubali ,ila pia hakuacha kushiriki kwenye malezi japo alibanwa na ndoa yake
 
Ipe muda hii hali.

Mama mtoto ashiriki kwa ukaribu (hata akiwa mbali) kwenye shughuli zinazomuhusu binti yenu( birthdays, kula Christmas pamoja, kwenda visiting day ww na Mama mtoto, pia Mama mtoto ampigie Binti kumuelekeza mambo ya Hedhi nk).

Binti huwa ni kipenz cha Baba.
Ila malezi mazuri anapata kwa Mama.
Mambo ya hedhi awaulize shangazi zake
 
Binti yako hana emotion connection na Mama yake coz hakuishi nae toka akiwa mdogo,hilo ni jambo la kawaida kabisa,

Ndio maana hua nasema humu,kuna tofauti kati ya kuhudumia na kulea,wapo wazazi hua wanahudumia ila hawana muda wa kukaa na watoto wao ili kujenga ile bond,

Mtoto humkumbuka au hua na emotion connection na mtu aliyekua nae kwenye makuzi yake,Angalia hata Lamine Yamal,alikataa kusign contract na Barcelona mpaka Bibi yake awepo kushuhudia,coz kwa kiasi kikubwa,yeye ndiye aliyemlea,

Huyo binti yako hata kama atarudisha mapenzi kwa Mama yake baada ya yeye kua mkubwa au kujitambua,basi mapenzi hayo hayawezi kua ni mapenzi ya dhati toka moyoni bali atafanya tu kisa ni Mama yake ila hatakua na hisia nae
 
Ipe muda hii hali.

Mama mtoto ashiriki kwa ukaribu (hata akiwa mbali) kwenye shughuli zinazomuhusu binti yenu( birthdays, kula Christmas pamoja, kwenda visiting day ww na Mama mtoto, pia Mama mtoto ampigie Binti kumuelekeza mambo ya Hedhi nk).

Binti huwa ni kipenz cha Baba.
Ila malezi mazuri anapata kwa Mama.
Mama yake anashiriki kila kitu hata leo kanitumia rangi ya gauni la mtoto kwa birthday yake mwezi wa tisa, ila kuna bond ya mama nahisi anaikosa, kwenye familia ya mtu kuweka hii bond kwa mtoto ambae yupo na bond na mimi naona ni ngumu sana 🤔
 
Back
Top Bottom