Namchukia sana Mama yangu

Namchukia sana Mama yangu

WanaJF

Mimi namchukia sana mama hata nsipowasiliana nae mwaka najiona sawa.

To sum up..
Mimi nmelelewa na bibi baada ya wazazi kuachana na mama akaolewa. Hivyo mimi nikiwa mtoto wa pili na mwisho ilibidi nikaishi na mama kulingana na umri wangu.

Baba wa kambo alitamka kauli moja anahitaji kubaki na mtu mmoja kama mama anaondoka mim nibaki na kama mimi naondoka mama abaki.

Maamuzi ya mwsho yaliamuliwa niondoke nikaenda kuishi na bibi huku mzee akiwa karibu na sisi tangu darasa la kwanza hadi tunamliza chuo.

Huwa naona mtandaoni watu wakiwasifia mama zao jins wanavowapenda ila kwangu imekuwa tofauti.

Nampenda sana bibi yaani sana hata nikiwa na kidogo bora apate bibi ila sio mama..Mama namuona kama. Sina maelezo mazuri ya kuelezea ila namchukia.

Nataman nimpende kama mzazi nifanyaje
Pole sana, fanya tu kile kilicho moyoni.
 
Hamna bond mkuu.

Na sijui ni kwanini wanawake hasa single maza wakiolewa na kama mwanaume hataki kuishi na huyo mtoto basi wengi huwatelekeza.

Mtoto asipopata malezi bora au upendo toka huko alipopelekwa lazima amlaumu na kumchukia mama/baba yake ila mhanga hapa huwa ni mama.

Huna haja ya kumchukia mkuu, utajiumiza bure. Si ajabu hata yeye anatamani sana aongee na wewe ila anakuogopa, kina mama wana tendency ya kuogopa vijana wao wa kiume hasa kama wewe ambae hajakulea kabisa.

Bado ni mama yako, wewe ni mwanae, ni mdogo kwake.
Anza kujenga nae ukaribu, trust me utapata faraja mno, utaiona furaha halisi ya mama yako pamoja na ukubwa wako huo utadeka upya.
 
"Baba wa kambo alitamka kauli moja anahitaji kubaki na mtu mmoja kama mama anaondoka mim nibaki na kama mimi naondoka mama abaki." Hii inatia mashaka sana. Baba wa kambo anataka ubaki wewe au mama yako?
Wewe na baba wa kambo mgefanya nini ikiwa mama yako hayupo?
 
Nilisema wapi?
Mim watoto wangu kwanza kama hupendi watoto wangu hata sura yangu au harufu yangu hutoisikia
sikuwa na maana ya wewe in person, ila humu kwenye mijadala vijana wanaimba kabisa kwamba hawataki kushughulikia wazee wao wawachwe na maisha yao
 
sikuwa na maana ya wewe in person, ila humu kwenye mijadala vijana wanaimba kabisa kwamba hawataki kushughulikia wazee wao wawachwe na maisha yao
Kama wazazi hawajakulea unategemea Nin?
 
WanaJF

Mimi namchukia sana mama hata nsipowasiliana nae mwaka najiona sawa.

To sum up..
Mimi nmelelewa na bibi baada ya wazazi kuachana na mama akaolewa. Hivyo mimi nikiwa mtoto wa pili na mwisho ilibidi nikaishi na mama kulingana na umri wangu.

Baba wa kambo alitamka kauli moja anahitaji kubaki na mtu mmoja kama mama anaondoka mim nibaki na kama mimi naondoka mama abaki.

Maamuzi ya mwsho yaliamuliwa niondoke nikaenda kuishi na bibi huku mzee akiwa karibu na sisi tangu darasa la kwanza hadi tunamliza chuo.

Huwa naona mtandaoni watu wakiwasifia mama zao jins wanavowapenda ila kwangu imekuwa tofauti.

Nampenda sana bibi yaani sana hata nikiwa na kidogo bora apate bibi ila sio mama..Mama namuona kama. Sina maelezo mazuri ya kuelezea ila namchukia.

Nataman nimpende kama mzazi nifanyaje

Mama anakosa gani? Hata huyo step Baba na hana kosa? Achana na huo ujinga usio wa maana.
 
Mpendee mama yako tu kakuzaa hajakutupa , baba yako alikutelekeza so hakuwa na jinsi
Wwe una kisonono cha kuchukia wanaume bila sababu ya msingi! Sasa hapo ni wapi mleta maada kasema baba yake alimtelekeza!? Wakati hadi ada za shule alikua analipa baba.yao japokua alikua anaishi kwa bibi yake!!
 
Mwanao atatakiwa na uliyezaa naye tu.
Na ndiyo maana wanawake wengi hupenda kusingizia mimba wanaume, maana wanajua kua akisema ukweli kua hii siyo mimba yako hakuna mwanaume atakubali kulea mimba au mtoto wa mwanaume mwenzie!!
 
Wako wengi sana kama Wewe lakini wamefaulu kusamehe, it is a process, na hapo ulipofikia uko pazuri umeanza kujiuliza maswali mazuri haujaufunga moyo kutafuta majibu.

Namna nzuri ni kuvivaa viatu vyake, angalia hali yake ya umri alivyokuwa naye mpimie leo na umri vs maamuzi ya mtu wa umri wake, pima changamoto zake alizokuwa nazo, na uelewa pamoja na fursa alizokuwa nazo. Utamuelewa kwamba mwanadamu huwa ana deal na changamoto zake kulingana na uwezo upeo na wingi wa knowledge alionao kwa wakati huo.
Kwa kesi kama hiyo hiyo yako Kuna waliowapa watoto sumu wakafa, kuna waliotelekeza kwa kuwatupa au kuwaacha mahali wao wakatoweka.
Kuna waliokataa kuitwa mama wakaitwa dada.

Jambo la kumshukuru Mungu ulipata grand parents wazuri hawakukutesa, kuna walioteswa na walezi mateso na manyanyaso makubwa sana.

Msamehe mama,pateni muda wa kuongeza huwa inasaidia sana kuongeza yaliyotokea kuliko kuyazika moyoni. All the best.
 
Wwe una kisonono cha kuchukia wanaume bila sababu ya msingi! Sasa hapo ni wapi mleta maada kasema baba yake alimtelekeza!? Wakati hadi ada za shule alikua analipa baba.yao japokua alikua anaishi kwa bibi yake!!
Haya kwanini hawapo together kama familia mnapenda sana kuchukuia wanawake
 
Kwahiyo ulitaka asiolewe abaki kwa wazazi wako anyanyaswe na wazazi wake au ulitaka achague ubaki wewe pale kwa baba wa kambo aondoke yeye?
Si kwamba hakupendi bali alikutana na jambo lililozidi uwezo wake
 
Ukikua utaelewa Mama asingeweza kumuacha mumewe kikubwa alikupeleka kwa Bibi na ukapata malezi bora, angalau mshukuru kwa kukuzaa.
Ashukuru Sana hajaolewa na Bab wa kambo yeye analeta pigo za ajabu
 
Mijitu humu sijui itaacha lini kukurupuka.
Mtoa mada keshaandika kuhusu baba lakini bado kuna mamburula yanakazana tuu kumlaumu baba.
Mnakosa umakini
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom