Namchukia sana Mama yangu

Namchukia sana Mama yangu

Of course hapo ndio shida ilipoanzia. Mleta mada hajatwambia mazingira yalikuwaje, ila kwa namna alivyoelezea ni kama vile palikuwa na kikao ambacho na yeye alishiriki (au labda alisikia mazungumzo yao).

Rejection inauma, na inaumiza sana akili. So kinachomuumiza jamaa yetu ni hiyo rejection na kukosekana kwa bond kati yao.

Sema Baba wa kambo naye ni cherema(akili mgando) au ni ile sampuli ya wanaume makatili na wabinafsi.
Wale wanaume waropokaji na watumiaji.

Mwanaume aliyetimamu hawezi kuongea maneno ya hovyo mbele ya watoto hata wasio wake.

Ongea na mkeo chumbani, eleza hofu yako, eleza suluhisho kisha toa maamuzi.
Kisha mama atekeleze sehemu yake kwa kuongea na kijana bila kuleta matàtizo.
 
kumbe alikupeleka kwa bibi na bibi alikupokea vizuri.... naona bado hujakuwa huwezi kuelewa kitu...
Pia hajajua kama bibi na mamaake waliongea na wakakubaliana juu ya maisha yake, hivii anamchukiaje mama kwa kumpeleka kuishi kwa bibi!!
 
Watu watamuona mtoa mada anakosea lakini ukija kwenye suala la ukweli na haki unamkûta yuko sahihi.

Kwanza hakupaswa kujua kuwa babaake wa kambo na mama wamepeana uchaguzi mgumu kama huo. Yeye alikuwa mtoto. Walimfangia ukatili mkubwa.
Fikiria mtoto anasikia Mamaake akimkana kisa mtu mwingine.

Mama kamsaliti mtoto kisa mume(baba wa kambo)
Ndio ile mtoto wa kiume anamfukuza Mamaake kisa Mkewe. Sio pouwa hiyo. Hakuna tofauti hapo.

Lazima chuki kali iwepo.

Hayo maelezo sijui hakumtunza ni Geresha. Ila ishu ni upendo.
Yeah ni kweli.., Sometimes watoto hatutakiwi kujua hata kama wazazi wanagombanaga..
That’s why namshukuru Mungu kwajili ya wazazi wangu siku zote
 
Pia hajajua kama bibi na mamaake waliongea na wakakubaliana juu ya maisha yake, hivii anamchukiaje mama kwa kumpeleka kuishi kwa bibi!!
bibi upande wa baba unahis waliongea nn..In short bibi alichukua jukumu baada ya kuona hatuna mbele wa nyuma
 
WanaJF

Mimi namchukia sana mama hata nsipowasiliana nae mwaka najiona sawa.

To sum up..
Mimi nmelelewa na bibi baada ya wazazi kuachana na mama akaolewa. Hivyo mimi nikiwa mtoto wa pili na mwisho ilibidi nikaishi na mama kulingana na umri wangu.

Baba wa kambo alitamka kauli moja anahitaji kubaki na mtu mmoja kama mama anaondoka mim nibaki na kama mimi naondoka mama abaki.

Maamuzi ya mwsho yaliamuliwa niondoke nikaenda kuishi na bibi huku mzee akiwa karibu na sisi tangu darasa la kwanza hadi tunamliza chuo.

Huwa naona mtandaoni watu wakiwasifia mama zao jins wanavowapenda ila kwangu imekuwa tofauti.

Nampenda sana bibi yaani sana hata nikiwa na kidogo bora apate bibi ila sio mama..Mama namuona kama. Sina maelezo mazuri ya kuelezea ila namchukia.

Nataman nimpende kama mzazi nifanyaje
Una childhood trauma sabbai ya tukio lililo tokea, mama aka aka ignore hilo tatizo limekuwa, umueleze why na nini kisababishi then safari ya ku heal ianzia hapo
 
Hiyo hali iliwahi kunipata nikiwa na umri kati ya miaka 14-18 hadi baba yangu alihisi kuwa nipo kwenye hali hiyo.
Licha ya kuwa yeye na mama hawakua na mawasiliano mazuri sana lakini alinieleza maneno haya "Lucha mwanangu yule ni mama yako , mama hakosei dunia hiii huwezi kumpata mama mwingine mpende sana mama yako pepo yako ipo chini ya nyayo za mama yako(kwa mujibu wa imani ya dini yetu tunaamini hivyo)"

Hiyo kauli ilinitoa machozi nilimtafuta mama yangu kwa simu nikawasiliana nae, lakini nasikitika hadi leo ule upendo wangu niliokua nao kwake kipindi nikiwa mdogo bado haujarudi kwa kiasi kile, siku moja nilimwambia mama kama una shida nieleze mimi ni mtoto wako mimi sina mama mwingine mama yangu alitoa machozi mbele yangu kwa mara ya kwanza mbele yangu.

Alhamdulillah kwa sasa ile chuki imeondoka kabisa duniani tunapitia mitihani mingi sana lakini amepata hasara yule ambae mama yake /baba yake ataondoka katika dunia hii hali yakua hana mahusiano nae mazuri Majuto huja wakati ambao huwezi kufanya nae suluhu au kuombana msamaha.

Nakusihi ndugu yangu msamehe mama yako na umpende sana maisha ni mara moja tu.
 
Kumchukia MTU ni tatizo kubwa Sana na linaweza kukutesa hasa pale utakapojua maisha ni UPENDO na vitu havina nguvu kumzidi MTU

Hasara za chuki
Utachelewa kuwa yule unayetaka kuwa
Utakuwa unafanya mambo kwa msukumo na sio kwa hiari yako.


Ikiwa Alifanya makosa usimchukie msamehe na umpende na kumjali ili utume ujumbe katika universe kuwa Love always win .


Mandela alisema hivi

"Kumchukia MTU ni kuamua kunywa sumu huku ukiamini itamuua unayemchukia"
Dr siku hizi umekua na busara sana kuna vimaneno unaviandika navipenda.... Naomba kuja pm 😊
 
WanaJF

Mimi namchukia sana mama hata nsipowasiliana nae mwaka najiona sawa.

To sum up..
Mimi nmelelewa na bibi baada ya wazazi kuachana na mama akaolewa. Hivyo mimi nikiwa mtoto wa pili na mwisho ilibidi nikaishi na mama kulingana na umri wangu.

Baba wa kambo alitamka kauli moja anahitaji kubaki na mtu mmoja kama mama anaondoka mim nibaki na kama mimi naondoka mama abaki.

Maamuzi ya mwsho yaliamuliwa niondoke nikaenda kuishi na bibi huku mzee akiwa karibu na sisi tangu darasa la kwanza hadi tunamliza chuo.

Huwa naona mtandaoni watu wakiwasifia mama zao jins wanavowapenda ila kwangu imekuwa tofauti.

Nampenda sana bibi yaani sana hata nikiwa na kidogo bora apate bibi ila sio mama..Mama namuona kama. Sina maelezo mazuri ya kuelezea ila namchukia.

Nataman nimpende kama mzazi nifanyaje
Msamehe, msamehe Mungu akutendee. Usilipe ubaya, msamehe
 
WanaJF

Mimi namchukia sana mama hata nsipowasiliana nae mwaka najiona sawa.

To sum up..
Mimi nmelelewa na bibi baada ya wazazi kuachana na mama akaolewa. Hivyo mimi nikiwa mtoto wa pili na mwisho ilibidi nikaishi na mama kulingana na umri wangu.

Baba wa kambo alitamka kauli moja anahitaji kubaki na mtu mmoja kama mama anaondoka mim nibaki na kama mimi naondoka mama abaki.

Maamuzi ya mwsho yaliamuliwa niondoke nikaenda kuishi na bibi huku mzee akiwa karibu na sisi tangu darasa la kwanza hadi tunamliza chuo.

Huwa naona mtandaoni watu wakiwasifia mama zao jins wanavowapenda ila kwangu imekuwa tofauti.

Nampenda sana bibi yaani sana hata nikiwa na kidogo bora apate bibi ila sio mama..Mama namuona kama. Sina maelezo mazuri ya kuelezea ila namchukia.

Nataman nimpende kama mzazi nifanyaje
Mzazi ata akosee vip atabaki kuwa mzazi.
 
Hakuna bond kati yenu, ndio maana unafeel hivyo.

Kwa choices alizopewa, ilikuwa ni wazi wewe ndio wakuondoka. Unaweza kumlaumu ila jaribu kumuelewa. Usikae na kinyongo, jaribu kuflash ili maisha yaendelee.
Amen
 
Nimevaa viatu vyako nikajua unavyojisikia, pole sana ila bi mkubwa alizingua kinyama! Nyakati na majira vitakuponya. Vidonda vitapona yatabaki makovu na yenyewe yatapotea utasahau. Songa mbele hayo yameshapita.
 
Hiyo hali iliwahi kunipata nikiwa na umri kati ya miaka 14-18 hadi baba yangu alihisi kuwa nipo kwenye hali hiyo.
Licha ya kuwa yeye na mama hawakua na mawasiliano mazuri sana lakini alinieleza maneno haya "Lucha mwanangu yule ni mama yako , mama hakosei dunia hiii huwezi kumpata mama mwingine mpende sana mama yako pepo yako ipo chini ya nyayo za mama yako(kwa mujibu wa imani ya dini yetu tunaamini hivyo)"

Hiyo kauli ilinitoa machozi nilimtafuta mama yangu kwa simu nikawasiliana nae, lakini nasikitika hadi leo ule upendo wangu niliokua nao kwake kipindi nikiwa mdogo bado haujarudi kwa kiasi kile, siku moja nilimwambia mama kama una shida nieleze mimi ni mtoto wako mimi sina mama mwingine mama yangu alitoa machozi mbele yangu kwa mara ya kwanza mbele yangu.

Alhamdulillah kwa sasa ile chuki imeondoka kabisa duniani tunapitia mitihani mingi sana lakini amepata hasara yule ambae mama yake /baba yake ataondoka katika dunia hii hali yakua hana mahusiano nae mazuri Majuto huja wakati ambao huwezi kufanya nae suluhu au kuombana msamaha.

Nakusihi ndugu yangu msamehe mama yako na umpende sana maisha ni mara moja tu.
Nimeipenda sana hii

Katika mafundisho ya kiislamu mama ana nafasi tatu ya nne ndio baba hii inaonyesha ni kiasi gani mama ana uzito mkubwa, na mafundisho yanasema ikitokea baba na mama wote wanakuita kwa wakati mmoja basi Muitikie mama kwanza

Ewe ndugu yangu hata mama yako aliumia pia alipokuacha uondoke lkn hakuwa na namna, kwahiyo ilibidi iwe hivyo,, ondoa hiyo dhana akilini mwako labda alimchagua mwanaume dhidi yako laa,,, ila ilitokea tu nawe aweze kuwa na mwenza.

Mpende mama yako kwa ajili ya Kutaka radhi za Mwenyezi Mungu

Ni swala la mda ukianza kumthamini kama mama utaona mapenzi yako kwake yanaongeza.

All the best chief
 
Pole sana kwa uliyo pitia, Mama ako sidhani kama alifanya ivo, kwa kukusudia ila naweza sema Ali fanya ivo kulinda maisha yake uhuenda alikua haoni future yake ingekuaje bila kua na mtu.

Kama umekua sasa fanya kujenga ukaribu nae kabla hujaja kujutia mama ni mama, hakuna kama mama
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom