Aunt ake kwa hiyo mtu akisema hachepuki ni anajifanya mtakatifu? Unafikiri kila mwanaume duniani anaendekeza kuchepuka?
1. Kuna watu wanaomuheshimu na kumcha Mungu, so cheating haipo kwenye mawazo yao. "Aonavyo mtu nafsini mwake ndivyo alivyo"
2. Kuna watu wameamua tu kutokucheat as wanaona haina faida kwao. Yes, cheating is a choice. Some people will cheat no matter how good it is, and others won't cheat no matter how bad it is.
Kwa nini hawa watu tusiwatie moyo, instead of kuwakatisha tamaa sijui wanajiona watakatifu mara wanafiki na maneno mengine ya kuwadiscourage? Kwa nini tunapromote sana "uchepukaji" na kuufanya ni kitu cha lazima?, yani tunahalalisha dhambi kwa kiasi hiki khaa! !!. Wanatuumiza mioyo ndo tunawakumbatia kweli na kuwapa moyo wazidi kutuuumiza.
Hayo magroup mawili niliyoyataja, hata mtu ikitokea amechepuka, (no one has immunity to cheating), ni wepesi wa kujuta na kurudi kwenye mstari, ni kitu ambacho kitamuumiza yeye mwenyewe sana na atarepent na kustruggle kurudisha ile trust ilovunjika. Ila wale wanaoona kucheat ni kawaida, hata umfume leo live, atazuga siku 2 ya tatu ana mchepuko mpya. He is unrepentant serial cheater
Hivyo kuchepuka ni heshima? Maana me siilewagi huo msemo wenu "eti achepuke ila amuheshimu mkewe" mmh????????. Kuonesha utupu wake huko nje na kuvunja kiapo chake cha ndoa ndo heshima? Afu usisahau haba na haba hujaza kibaba. Leo utasema it's ok achepuke tu ila aniheshimu sijui, akishanogewa umsahau. Hao wanaohama nyumba zao leo na kuhamia kwa michepuko, hata na wenyewe walianzia na kuchepuka kidogo huku "wakiheshimu" wake zao, ila dhambi ikishakomaa huzaa mauti. So ataendelea kuchepuka hadi ndoa yenu ipate mauti. Hivi kweli tunahalalisha waume kuumiza wake zao wa ndoa au ndo tumeamua tu kuishi kwenye denial???? Hawa wake hawana mioyo au? Afu hakuna kitu kinachoumiza kama emotional abuse, majeraha yake hayaonekani kwa macho ila yana madhara makubwa sana. Wanandoa na waheshimu ndoa zao jamani. Ndoa ni wawili, watatu ni ibilisi, sasa kama kuna ibilisi anayejenga ndoa, haya tutaonaga.