LadyAJ, kwa lugha uliyotumia, hapo juu, ni dhahiri wewe ni mtata. Umejaza pekepeke na shutuma tu, na siyo ushauri.
Hakuna ugonjwa unaoua wanaume sana, kimawazo na kimwili, kama hiyo lugha uliyotumia kuwasilisha hisia zako.
Mwanaume anahitaji kuheshimiwa na kubembelezwa hata kama kafanya kosa dhahiri. Pekepeke na shutuma za mwanamke, kama zako, ni adui mkubwa wa mahusiano katika ndoa.
mshana jr, kawasilisha hoja mwafaka kwa upande wa akina baba, akiwatahadharisha matokeo hasi ya nyumba ndogo. Kwa falsafa, anawahasa akina mama ndoani, kuwa makini na ndoa zao.
LadyAJ, mpira uko uwanjani kwako.