Nakiri kwamba naendelea kujifunza siasa za Tanzania

Umeongea vizuri sana mkongwe. Ila umesahau jambo moja. Shida kwenye nchi yetu ilianza pale Nyerere alipokataa mawazo ya watu waliokuwa wanaona mbele kuliko yeye hasa Kambona.

Kwa jinsi Nyerere alivyomfanyia Kambona ndo laana ya hii nchi ilipoanzia. Kama hatujatubu ile dhambi, maendeleo ya kweli tuyasahau milele.

Kambona alipinga sana siasa za kukieneza zaidi Chama cha Mapindizi kuliko Serikali na huduma zake. Wakamuona mzandiki hafai, Kambona alipinga nchi kujiingiza kwenye siasa za ujamaa wakamuona chizi wakamfanya hadi akimbie nchi.

Ukitizama kwa makini mambo aliyopinga Kambona hadi kukorofishana na Nyerere ndo msingi na chanzo kikuu cha matatizo yanayotukabili hii leo.
Nakubaliana kabisa na wewe kabisa, mchango wa Oscar Kambona kwa hili taifa ni mkubwa mno, tena mkubwa sana. Nadhani hakustahili kufanyiwa vile na kina Mzee Nyerere. Nadhani njia sahihi ilikuwa kumuweka pembeni kuliko kumchafua vile mtu aluetoa mchango mkubwa kwa taifa:​
  1. Kambona alivyoingia TANU ndani ya mwaka mmoja alikusanya wanachama 10000.​
  2. Ndiye aliyeunda mifumo ya usalama hapa nchini akishauri kwamba vijana wa TYL ndiyo waingizwe kwenye idara mpya ya usalama wa taifa. Yeye ndiye aliyeenda kwa waisraeli ili watoe mafunzo kwa watanzania.​
  3. Ndiye aliyezima uasi wa kijeshi wa KAR mwaka 1964 wakati Mzee Nyerere na Rashidi Kawawa wakiwa wamefichwa. Angekuwa ni mtu mbaya basi baadhi ya wanajeshi walipomwambia ajitangaze kuwa Raisi alikataa mzee wa watu.​
  4. Kambona ndiye ARCHITECH wa FOREIGN POLICY ya Tanzania, alichokuwa anakizungumza Kambona miaka ya 60's mwanzoni ndicho ambacho Mzee Nyerere alikuwa akikizungumza miaka yote ya utawala wake.​
Kambona was forced into the Dark-Side. Mambo mabaya aliyofanyiwa ndiyo yalipelekea Kambona aje kuwa na moyo mgumu vile. Mzee Nyerere alimwogopa Kambona hadi mwisho kwasababu yeye ni mmoja kati ya watu waliokuwa wanamfahamu Nyerere kiundani (Hulka na Madhaifu yake), jambo ambalo Nyerere hakulipenda ukizingatia alishajitengenezea A CULT OF PERSONALITY.​
 
Ndugu yangu umefafanua kwa kina, kitaalam na umefanya analysis nzuri sana.

Na hakika, baya likiingizwa kwenye mfumo wa utawala, kuliondoa ni mpaka kwa sululu, na hasa kama baya hilo lina watu linaowanufaisha.

Leo msingi mkubwa wa CCM ni uovu. CCM inajitambulidha kwa watu kimatendo kuwa ni chama kinachosimamia na kujivunia ushetani/uovu. Leo CCM, mtu akiwa mwovu kupindukia, kama alivyo Makonda, anaonekana ndiye shujaa wa chama. Yaani kwa sasa shujaa wa CCM ni yule anayeweza kudhulumu watu, vyama na makundi ya baadhi ya watu ili CCM au watu fulani ndani ya CCM wafanye uovu wao bila kubughudhiwa.

Yaani yale mambo ambayo yalitakiwa kuonewa aibu, ndiyo CCM kwayo inajivunia na kuyaonea fahari.

Kwa tunavyoenda, hata kama siyo leo au kesho, kusipokuwa na mabadiliko ya kweli na ya haraka, lazima nchi hii itumbukie kwenye njia ile ile ambayo mataifa mengi ya Afrika yamepitia. Na tkiingia tu kwenye njia hiyo, nayo itajenga mfumo na fikra mpya, ambayo nayo nchi itaishi nayo kwa miaka mingi. Na hilo kutokea wala haitachukua muda mrefu.
Wazungu husema hivi "When children grow up, they always realize a parent who was a problem"​
 
Nakubaliana kabisa na wewe kabisa, mchango wa Oscar Kambona kwa hili taifa ni mkubwa mno, tena mkubwa sana. Nadhani hakustahili kufanyiwa vile na kina Mzee Nyerere. Nadhani njia sahihi ilikuwa kumuweka pembeni kuliko kumchafua vile mtu aluetoa mchango mkubwa kwa taifa:​
  1. Kambona alivyoingia TANU ndani ya mwaka mmoja alikusanya wanachama 10000.​
  2. Ndiye aliyeunda mifumo ya usalama hapa nchini akishauri kwamba vijana wa TYL ndiyo waingizwe kwenye idara mpya ya usalama wa taifa. Yeye ndiye aliyeenda kwa waisraeli ili watoe mafunzo kwa watanzania.​
  3. Ndiye aliyezima uasi wa kijeshi wa KAR mwaka 1964 wakati Mzee Nyerere na Rashidi Kawawa wakiwa wamefichwa. Angekuwa ni mtu mbaya basi baadhi ya wanajeshi walipomwambia ajitangaze kuwa Raisi alikataa mzee wa watu.​
  4. Kambona ndiye ARCHITECH wa FOREIGN POLICY ya Tanzania, alichokuwa anakizungumza Kambona miaka ya 60's mwanzoni ndicho ambacho Mzee Nyerere alikuwa akikizungumza miaka yote ya utawala wake.​
Kambona was forced into the Dark-Side. Mambo mabaya aliyofanyiwa ndiyo yalipelekea Kambona aje kuwa na moyo mgumu vile. Mzee Nyerere alimwogopa Kambona hadi mwisho kwasababu yeye ni mmoja kati ya watu waliokuwa wanamfahamu Nyerere kiundani (Hulka na Madhaifu yake), jambo ambalo Nyerere hakulipenda ukizingatia alishajitengenezea A CULT OF PERSONALITY.​
Kikubwa zaidi Kambona alipinga Chama kuonekana kama a symbol of pride huku kikienezwa nchi nzima hadi vijijini badala ya Serikali kujikita katika kueneza huduma muhimi kama Barabara, Hospitali na Mashule.

No wonder leo kuna maeneo mengi nchini watu wanaenda kwa viongozi wa chama kutatuliwa matatizo yao badala ya kufuata mifumo sahihi ya kiserikali! Rejea ziara za Makonda na watu kwenda kwake.

Kambona alisema tusianzishe vijiji vya ujamaa badala yake tujikite katika katika mfumo tuliokuwa nao before 1967. Ukifuatilia siasa ya ujamaa ndo hii imetengeneza watu wavivu wasiofikiri vizuri ambao kwao kila kitu ni Serikali.

Imetengeneza watu wajinga waliojaa Serikalini ambao hawatumii akili zao vizuri zaidi ya kuwaza madaraka , posho na vyeo tu.
 
Moja ambalo umekosea, 1995 kama Sio Nyerere ilikuwa Malecela, .
Pili hakuna Muhaya, au Nyakyusa au Chagga aliyekataliwa Kwa Uchaga wake wala Muhindi. salim Ahmed Salimu hakuwa Muhindi.
Nyerere Mpango wake WA awali ulikuwa ni Sokoinne achukue nchi baada yake.
Tatu Nyerere baada ya Sokoinne Kufa, alitegemea Yeye na Jumbe wangejiuzulu pamoja.
Hivyo kusingekuwepo na Nafasi ya Ali Kuwa Kiongozi WA Juu aliye Baki kipindi hicho. Hivyo Raisi wa Jamuhuri angebaki WA kutokea Bara na makamu angekuwa ametokea Visiwani.
Kitu cha kujifunza hapa ni kukubali kuwepo Kwa matukio yalio nje ya nguvu zetu Sisi binadamu, hivyo hayo mambo ya natakiwa kuthibitiwa na Katiba.ambayo haita mruhusu Kiongozi yoyote kuendesha nchi anavyotaka yeye Bali wanavyotaka watanzania.
Mbona John Malecela nimemtaja au hujasoma vizuri nilichokiandika ?

Kuhusu makabila ya HAYA, CHAGGA na NYAKYUSA haiwezi kuwa rahisi kwa watu wao kufika juu kwasababu ya STERETYPES and ANTI-TRIBAL CANARDS. Haya makabila yalishakuwa BLACK-BALLED tokea awamu ya kwanza, na watanzania wamekuwa na hiyo minong'ono kama sehemu ya falsafa yao kwamba haya makabila yana hulka ya kupendeleana. Jambo ambalo halina ukweli wowote ule kwasababu imethibitika tatizo ni mfumo wa kusimamia nafasi za ummah na siyo kabila.

Maana mpaka sasa imethibitika kwamba hata Mkwere na Msukuma wakiingia kama hakuna mifumo imara ya usimamizi wa taasisi za ummah basi lazima upendeleo utaonekana. Hivyo HAYA, CHAGGA na NYAKYUSA ni kuonesha mfumo wa Ubaguzi ambavyo uko hapa nchini na unakubalika. Alipoinga Raisi Magufuli yakaonekana yaleyale dhidi ya WASUKUMA, na hata akaingia Raisi MHEHE yataonekana yaleyale dhidi ya WANYALUKOLO kama ilivyokuwa kipindi Mzee Philemon Luhanjo ni Katibu Mkuu Kiongozi (KMK).

Nakumbuka mwaka 2015, Ridhiwani Kikwete, mtoto wa Raisi wa wakati huo aliwahi kunukuliwa wazi akisema kwa kujivuna kabisa kwamba "Raisi wa Tanzania hawezi kutoka Kaskazini". Hili alilolisema hakukemewa na mtu, ila alitudhihirishia wengi kwamba hizo ndizo kauli ambazo zinazungumzwa pale wakubwa zake pale magogoni.

Kuhusu Mzee Nyerere na Sokione nadhanu umefanya kitu kiitwacho (CHERRY PICKING HISTORY). Mwishoni kabisa Mzee Nyerere hawakuelewana kabisa na Moringe Sokoine. Huwa nashangaa watanzania wanapoamini kwamba hata kifo chenye utata cha Sokoione kilitokea kwa bahati mbaya, ilhali waandishi nguli kama Mzee Ndimara Tegambagwe waliandika vizuri kuhusu kifo cha Sokione mwaka 1992, kwenye kazi yake iitwayo "WHO TELLS THE THRUTH IN TANZANIA ?" ambapo alizungumzia taarifa nyingi zilizozunguka kifo cha Sokione hadi mtu unabaki kushangaa tu.

Mwisho kabisa, Sokione alionekana kupinga baadhi ya sera za Nyerere wazi kabisa jambo ambalo lilimkera mno Mzee Nyerere kwasababu alikuwa hapendi kukosolewa. Mfano, kwenda BoT kumtishia Gavana Charles Nyirabu atoe fedha za kutibu mlipuko wa magonjwa ya mifugo la sivyo anamfukuza kazi. AU kwenye kampeni ya uhujumu uchumi iligusa hadi viongozi wakubwa wa Kanisa ambao ilisemekana walitumika kuwafichia baadhi ya viongozi pesa, Sokione akatishia kuwakamata maaskofu.

Mzee Sokione was a Hard-Worker but also an Erratic Maverick, kuna baadhi ya mambo alikuwa anafanya ni kinyume na utaratibu na ilibidi Mzee Nyerere amuite kumfunga Speed-Governor. Alipoenda Msumbiji kwa Samora Macheli, Nyerere alilalamika kwamba Waziri Mkuu wake anamsumbua, na kuulizwa na Samora kwanini asimfukuze ? Akajibu akimfukuza italeta matatizo kwasababu watu wanamkubali. Ukweli ni kwamba hata alipoondoka mwaka 1980 hawakuwa kwenye Good-Terms, japo aliamua kumrudisha mwaka 1983 kwasababu mambo yalikuwa yameanza kuwa magumu sana ndani ya utawala wa Nyerere.

Namalizia kwa kukubaliana na wewe kwamba, mambo mengine huwezi kuzuia yasiyokee ila unaweza kuyatawala(One cannot stop crisis but Manage It), hivyo nadhani ndiyo muhimu viongozi wetu wa Tanzania kufahamu.​
 
Nyerere aliondoa ubaguzi, wa kidini na kikabila, Ndio maana Mbowe alisoma Kagera, Lowasa alisoma Tabora , weusi walipata nafasi kwenye Shule za wahindi , Shule za wakatoliki au tuseme za kidini zilitaifishwa ili kuwezesha dini zingine wapare fursa
Anyway tumsamehe tu Nyerere lakini yeye ni chanzo cha Matatizo mengi Nchi hii.

Bahati mbaya ccm wameyakumbatia.
 
Pia JPM alijitambulisha kama Msukuma, kabila kubwa kuliko yote nchini, na halina utamaduni wa kubebana. Hatuoni kwamba huo mfumo wa kuogopa makabila makubwa unekufa automatic.
Mbona kulikuwa na Anti-Sukuma Sentiments through-out utawala wake, au ulikuwa huzioni ?

Nachelea kusema kwamba, WE CANNOT OUTLIVE TRIBALISM, na kusema kwamba makabila fulani yanapendeleana nadhani inaweza ukawa ni ukweli nusu. Nasema hivi kwasababu imethibitika kwamba watanzania wengi wakipata nafasi, hata awe anatokea kabila dogo ni lazima atavutia kwake na kupendelea baadhi ya watu. Kama siyo upendeleo wa kikabila basi upendeleo wa kidini.

Hapa tunafikia kwenye HITIMISHO kwamba tatizo siyo UKABILA peke yake, bali MIFUMO yetu ya nchi inayosimamia nafasi za umma haifanyi kazi. Katika nchi ambayo iliwahi kuwa na mvutano mkubwa wa kikabila (Ethnic Tensions), basi Singapore ilikuwa ni hatari. Ile nchi ina makabila makubwa mno na yenye nguvu sana (Ethnic Chinese, Indians and Malays). Wachina ndiyo wengi ambao ni zaidi ya asilimia 50%, jambalo mara ya kwanza lilizua hisia kwamba wao ndiyo watawala.

Ikafika kipindi polisi mwenye asili ya kichini akimkamata mhalifu wa mwenye asili ya kihindi inaonekana kuna uonevu. Hata Malays nao ambao ni waislamu walilamika hivyo-hivyo. Mwishoni Waziri Mkuu Lee-Kuan-Yew akafahamu kwamba tatizo siyo KABILA bali MFUMO, hivyo waliunda MFUMO mpya ambao ulihakikisha watu wanapata nafasi kutokana vigezo (MERIT BASED SYSTEM), ndiyo maana Singapore imefika hapa leo.

Bila MFUMO imara, hata Malaika akiwekwa awe Raisi anaweza akalevwa na mvinyo wa madaraka.​
 
Poleni na misiba mikubwa ya kitaifa.

Nikiri kwamba kila siku naendelea kujifunza kuhusu siasa za taifa changa la Tanzania. Mambo makubwa ambayo mpaka sasa nikiri nimeshuhudia yakitokea bila chenga ni kwamba APANDACHO MTU NDICHO HUVUNA, na MWANADAMU HAWEZI KULINGANA NA MUNGU. Nitaelezea mtazamo wangu kwa ufupi:

Mosi, dhambi ya ubaguzi ambayo ilipandwa kwenye hili taifa dhidi ya makundi ya watu fulani itaendelea kulitafuna hili taifa endapo hatutakubali kubadilika. Ubaguzi ambao upo hapa nchini umekuwa wa kisera (Systemic Discrimination) na watu wameshakubaliana nao kwamba ndiyo utamaduni wetu wa kisiasa. Jambo hili siyo sawa hata kidogo, The Anti-Chagga, The Anti-Nyakyusa and The Anti-Haya Canards rooted at the founding cores of this nation state are very vile and devilish.

Ukifikiria kwa umakini na kuchambua historia ya nchi hii, utafahamu kwamba yale ambayo yaliogopwa kutokea endapo atapatikana Raisi Mchagga, Mnyakyusa au Mhaya yamefanywa hata alipokuwepo Raisi Mmakonde, Mzanzibar, Mkwele na Msukuma. Upendeleo (Nepotism and Cronyism) umeonekana, kama siyo katika minajili ya kikabila na kikanda, basi katika minajili ya kidini. Mifano iko mingi ya maraisi kuvutia kwao aidha kikabila, kikanda au kidini.

Sasa kwanini minong'ono na chuki za chini-chini ziendelee kuwa dhidi ya haya makabila matatu ilhali imethibitika kwamba kila mtu akikalia kiti cha uraisi, hata atoke kabila dogo, kama nchi haina mifumo imara ya kiutawala rushwa na upendeleo vitakuwepo tu. Halafu katabia kingine cha watanzania weusi kupenda kubagua watanzania wenye asili ya asia nako kametusababishia matatizo makubwa.

Huwa najiuliza maswali machache tu, hivi mtu kama Salim Ahmed Salim angekuwa Raisi mwaka 2005, leo hii Tanzania tungekuwepo hapa kweli ? Au mtu aina ya Prof Mark Mwandosya angekuwa Raisi leo hii Tanzania ingakuwa wapi ? Ila ni kwamba, hawa watu mbali na kufanya vyote kwa nchi, kiti cha Uraisi wasingeweza kuachiwa. Haya angalia leo hii tuko wapi.

Pili, hakuna baya utakalolifanya halafu lisikurudie. Hili ntalithibitisha kwa mifano hai kabisa. Marehemu Mzee Nyerere alifanya mazuri mengi, lakini mwishoni mwake alifanya makosa mengi mno ambayo aliyajutia na yalikuja kumrudi mwenyewe. Kuhusu Zanzibar alijutia sana hadi dakika za mwisho, na Mzee Dr Kitine alipoonana naye uwanja wa ndege wakati anaenda kutibiwa nchini Uingereza walizungumza sana kuhusu Zanzibar.

Naamini, kama mambo yangekuwa ni mazuri kuhusu Zanzibar asingeongelea hata kuhusu wao kuwa huru. Muungano haujarekebishwa, na umegeuka donda-ndugu (gangrene) ambalo linaitesa taifa hadi sasa, na nashukuru kwamba watanganyika kizazi kipya wameanza kuelewa kile ambacho G55, CHADEMA na TUME YA WARIOBA wamekuwa wakikizungumzia kuhusu muundo wa muungano. Tungeyamaliza haya mapema, nadhani leo hii taifa lisingekuwa na nyufa na chuki za chini-chini kama ilivyo leo.

Jingine ni suala la Uraisi mwaka 1995, ndani ya CCM na UPINZANI. Tunasema Mzee Nyerere, Fumbled the Bag. Alitumia nguvu yake kubwa ya kiushawishi kuwaumiza wanasiasa wengi kiasi cha kuwageuza moyo na kuwafundisha kwamba michezo michafu inalipa. PRECEDENT ya Mzee Nyerere kumuweka Raisi Mkapa kwa gharama yoyote ile, ilikuwa sahihi kwa muda mfupi (Tactical) lakini mbaya kwa muda mrefu (A Strategic Failure).

Tanzania ilikuwa ndiyo inajifunza kufanya mfumo wa demokrasia ya vyama vingi, 1990-1995 was an advent of multi-party democracy in Tanzania. It simply was a defining moment that could reverberate generations to come. Ilitakiwa CCM chini ya ushawishi wa Baba wa Taifa ioneshe mfano na kuongoza njia, ili kujenga msingi imara wa utawala hapa nchini. Kama watanzania hasahasa wale waliopo ndani ya CCM wangeona kwamba demokrasia inafanya kazi, na wale wenye vigezo ndiyo wanapita na siyo CLIENTISM ambayo Mzee Nyerere aliitumia binafsi naamini hata wale waovu wangeona iabu na CCM ingekuwa imejijengea utamaduni imara sana.

Ila wote tunafahamu baadhi ya wanasiasa akiwemo Mzee John Malecela, Horace Kolimba na Jakaya Kikwete walichofanywa. Huwa najiuliza swali hili: Hivi Jakaya angekuwa Raisi wakati Mzee Nyerere yupo hai angeweza kweli kuunda mtandao ambao wa kutafuta madaraka kwa namna yoyote ile, hata kuumiza watu wengi na kuuza roho yake kwa Ibilisi ili mradi awe Raisi ? Bado najiuliza. Huwa tunaulaumu MTANDAO kwa jinsi ulivyoharibu CCM na nchi, lakini huwa hatupendi kuzungumzia nini kilichopelekea mtandao kuundwa.

Siasa za ndani ya CCM za mwaka 1995 zilichangia sana MTANDAO kuundwa. Vijana ambao walinyimwa haki zao kihalali mwaka 1995 waliamua kujipanga kuhakikisha jambo kama lile halitokei tena mwaka 2005. Bahati mbaya sana walivyounda ule MTANDAO ndipo safari yao ya kumkabidhi IBILISI roho zao ilianza. Nachelea kusema, siyo vizuri kuwasema marehemu, lakini mpaka leo hii wanamtandao wote hawapo hai na maisha yao yalijaa mno uchungu na maumivu. Wamebakia Mzee Jakaya Kikwete na Rostam Aziz.

Wazungu husema, THERE'S NO HONOUR AMONG THIEVES. Punde tu baada ya kutimiza adhma yao ya kuupata Uraisi kwa gharama zozote zile, MTANDAO ulikumbwa na vita kubwa ya wenyewe kwa wenyewe (A Civil War) ambayo ililitesa taifa hili na kutufikisha hapa tulipo leo. Matatizo yote yale ambayo tunakumbwa nayo leo hii ya UFISADI, UKOSEKANAJI WA UMEME, UONGOZI DUNI, MAKUNDI NDANI YA CHAMA, SIASA ZA VISASI, MFUMUKO WA BEI na MATATIZO MENGINE YA KIUCHUMI yalichochewa sana na VITA YA WANA-MTANDAO ambayo ilianza mwaka 2006, ikachukua sura mpya mwaka 2008, na kuleta matokeo mabaya kwenye uchaguzi wa 2010 na mwishowe kufikia mwisho mbaya mwaka 2015 ambapo Tanzania Citizenry was a living collateral damage.

Namalizia hoja hii kwa kusema, Mzee Nyerere alimuweka Mkapa kwa hila, lakini akaanza kujuta na kutaka Mkapa asigombee mwaka 2000. Bahati mbaya wakapishana pakubwa na kuanza kufanyiana siasa za CLOAK & DAGGER ambazo hazikuisha vizuri. Raisi Mkapa alipishana na Mzee Nyerere, na hakuweza kuwa na uvumilivu mkubwa ambao Mzee Mwinyi alikuwa nao, akaonesha wazi-wazi kabisa kukerwa na Mzee Nyerere. Wasomi wengi ambao walikuwa wanamshauri Mzee Nyerere kuhusu kupinga sera za Ubinafsishaji walikiona cha MTEMA KUNI. Mzee Nyerere alilalamika wazi-wazi kwamba kwanini Mkapa anamfedhehesha huku akiwa hai.

Haikuishia hapo, mwaka 2015 kama ilivyokuwa mwaka 1995, Raisi Jakaya akafanya kilekile ambacho yeye mwenyewe alifanyiwa mwaka 1995. Alikata majina ya watu bila hata kuwasikiliza. Kulikuwa na wagombea wazuri mno mbali ya Mzee Lowassa (RIP), kina Prof Mwandosya, Dr Mahiga, Dr Mwele, Jaji Ramadhani, Dr Kitine nk. ambao hawakupewa nafasi. Raisi Mkapa akaamua kutumia karata yake ya ushawishi kuhakikisha kwamba Raisi Magufuli anapenya na Mzee Kikwete akaridhia baada ya kuona mtumbwi unazama na wana-MTANDAO wenzake wanaelekea kumshinda.

Mambo ni mengi mno, aliyewekwa na Raisi Mkapa na Raisi Kikwete akawageuka na kuanza kuwanyoosha, kama ambavyo Mkapa aligeuka kumnyoosha Nyerere aliyemuweka. Mengine tunamwachia Mungu. Ila naomba ujiulize hili swali:

Hivi wangetenda mema mwaka 1995 tungefika huku leo ? Amini, Amini nawaambia. Kama ilivyokuwa mwaka 1995 vijana kuunda MTANDAO, vivyo hivyo mwaka 2015 vijana wameunda MTANDAO mwingine, tofauti ni kwamba sasa hivi iko MITANDAO MINGI na MIZITO.

Tatu, na mwisho kabisa. Mwanadamu usijifanye MUNGU (Never Play GOD), kwasababu mbali na kuwa na uwezo wa kubadilisha mambo, hakuna mwanadamu dunia hii anayeweza kuzuia mabadiliko (No Man Can Ever Stop Changes). Kama tu mwanadamu hawezi kuzuia ukuaji wake binafsi, sembuse taasisi kubwa kama dola. Hivyo basi, hatuwezi kuzuia mabadiliko ila tunaweza kuyamudu (We Can't Stop Changes, But We Can Manage Them). And how do we manage changes? Through thorough preparations. Sisi kama kizazi kipya inabidi tujifunze na kuangalia ni wapi wazee walijikwaa.

Kama tukiendelea kuamini hizi falsafa ovu ambazo tulizikuta, basi hili taifa halitakuwa na amani kwa muda mrefu. Mbinu ambazo zilitumika kuwashughulikia watanzania milion 10-20 kipindi cha TANU/CHAMA KIMOJA haziwezi kuendelea kutumia kudhibiti taifa la kiutandawazi lenye watu zaidi ya milioni 60, ambao wanaingia na kutoka nje ya nchi kila uchwao.

Zile falsafa za kuamini kwamba watu wa UKANDA FULANI, KABILA FULANI, ASILI FULANI, JINSIA FULANI au DINI FULANI ndiyo wanaotakiwa sana kupewa nafasi nyeti kitaifa huku wengine wa kundi jingine wakibaguliwa wazi-wazi utadhani siyo WATANZANIA, kwamba ni wenye hulka ya wizi na kupendeleana ilhali tunasahau kwamba wako wengi na walitangulia kusoma tokea ukoloni. Ukweli mchungu ni kwamba matatizo yanayotokea hapa nchini hayajaletwa na CHAGGAS, NYAKYUSA AU HAYAS. Ni sawa na ule upumbavu wa kuamini kwamba WASUKUMU wa Raisi Magufuli ndiyo wameleta matatizo, jambo ambalo ukiliangalia kimapana halina ukweli wowote zaidi ya STIGMA and STEREOTYPE.

AU kuamini kwamba WAHINDI na WAARABU ndiyo chanzo cha umasikini wa mtu mweusi, ilhali tunasahau ukweli mchungu kwamba hao WAHINDI waliokimbia Tanzania miaka ya 60's na 70's kuelekea Uingereza na America Kaskazini bado wamefika huko na kuendelea kuwashinda hata hao wazungu na jehuri zao. Jiji la London lina wahindi wengi matajiri wa kutupwa ambao walitokea Tanganyika, Kenya na Uganda. Hili ni jambo linalofikirisha.

Ukienda Marekani, ukakutana na Diaspora wa Tanzania, wengi wao ni Wazenji, Wachagga, Wanyakyusa na Wahaya. Sasa unabaki kujiuliza, hii chuki ilitokea wapi, mbona hata huku kwa wazungu bado hawa watu wanafanikiwa mno. Mwisho unakuja kufahamu kwamba, kuna kitu hawa wenzetu walikifahamu muda mrefu, ambacho hata wengi wakikifahamu watafanikiwa tu.

MUHIMU KUKUMBUKA: Mwaka 2024 kutakuwa na uchaguzi mdogo, Mwaka 2025 uchaguzi mkuu. Mambo yatakayofanyika kipindi hiki yawe mema au mabaya, fahamu kwamba tutaishi nayo miaka mingi sana ijayo, kama ambayo tunaishi na yale ya mwaka 1995, 2005 na 2015. Niseme tu, The Domino Effects of 2015 will be profound and long-lasting. Kazi kwetu watanzania.....

APANDACHO MTU NDICHO ATAVUNA, huwezi panda Magugu ukavuna Mtama.

Niwatakie Usiku mwema....​
Nakubaliana na wewe 100%. Tungepata watu kama wewe 100 ndani ya CCM, nchii ingesonga mbele. Viongozi wanafikiria matumbo yao kuliko masilahi ya nchi. Wanasahau kuwa binadamu atapita ila nchi itabaki.
Yu wapi Nyerere, Karume, Mkapa, magufuri Lowasa (to mention few). Wako wapi waliokuwa wanasimama Dar wanakohoa nchi nzima inatetemeka, walikuwa na ulinzi wa kutisha, waliokuwa na Mali za Kila aina.
Tunapomzika E.Lowasa tujifunze kuwa Dunia hii ni ya kupita. Usimtendee mwenzako usivyopenda kutendewa naye.
Brief summary yako izingatiwe na CCM wanaosema wanaipenda Tanzania, kumbe wanajitafutia matumbo yao na watoto wao na wajukuu wao. Wanasahau kuwa vyote hivyo wataviacha na Tanzania itabaki. Wanaangalia hatima ya familia zao na chama Chao, badala ya hatima ya nchi.
Mwisho siyo kweli kwamba unaendelea kujifunza siasa za nchi hii, Bali wewe ni mwalimu wa siasa za nchi hii. And Old is gold.
 
Mbona kulikuwa na Anti-Sukuma Sentiments through-out utawala wake, au ulikuwa huzioni ?

Nachelea kusema kwamba, WE CANNOT OUTLIVE TRIBALISM, na kusema kwamba makabila fulani yanapendeleana nadhani inaweza ukawa ni ukweli nusu. Nasema hivi kwasababu imethibitika kwamba watanzania wengi wakipata nafasi, hata awe anatokea kabila dogo ni lazima atavutia kwake na kupendelea baadhi ya watu. Kama siyo upendeleo wa kikabila basi upendeleo wa kidini.

Hapa tunafikia kwenye HITIMISHO kwamba tatizo siyo UKABILA peke yake, bali MIFUMO yetu ya nchi inayosimamia nafasi za umma haifanyi kazi. Katika nchi ambayo iliwahi kuwa na mvutano mkubwa wa kikabila (Ethnic Tensions), basi Singapore ilikuwa ni hatari. Ile nchi ina makabila makubwa mno na yenye nguvu sana (Ethnic Chinese, Indians and Malays). Wachina ndiyo wengi ambao ni zaidi ya asilimia 50%, jambalo mara ya kwanza lilizua hisia kwamba wao ndiyo watawala.

Ikafika kipindi polisi mwenye asili ya kichini akimkamata mhalifu wa mwenye asili ya kihindi inaonekana kuna uonevu. Hata Malays nao ambao ni waislamu walilamika hivyo-hivyo. Mwishoni Waziri Mkuu Lee-Kuan-Yew akafahamu kwamba tatizo siyo KABILA bali MFUMO, hivyo waliunda MFUMO mpya ambao ulihakikisha watu wanapata nafasi kutokana vigezo (MERIT BASED SYSTEM), ndiyo maana Singapore imefika hapa leo.

Bila MFUMO imara, hata Malaika akiwekwa awe Raisi anaweza akalevwa na mvinyo wa madaraka.​
Mfumo imara nakuunga mkono. Na Lee-Kuan-Yew mwenyewe alikuwa ni mlowezi wa kichina lakini wakati anaanza hizo harakati za kuseti mifumo imara duniani kote aliitwa Ddikteta.

Hata kwetu akiibuka mtu mwenye nia njema atapingwa kitaifa na kimataifa.

Nashauri system iweke ushindani huru. Kama ni mtanzania mwenye asili ya kiarabu, au kutoka kabila kubwa au nje ya Muislam/Catholic na anauwezo wa kutuvusha apewe nafasi. Asipewe kwa sababu ya ukabila au udini wake bali kwa sababu ya uwezo na ubora wake.

Ila powertrend duniani inaonyesha no vigumu sasa hivi mfumo mmoja kuendelea kutawala kwa muda mrefu kama ambavyo imekuwa rahisi moaka ya 70,80,90. Hivyo natofautiana na mtazamo wako kuwa mfumo tulionao 2023+ ukiendelea tutahitaji miaka mingi sana ili mabadiliko yatokee. Mimi naamini kuna siku katikati ya mfumo huu korofi kadili maarifa yanavyoongezeka utajiua wenyewe au kutokea nje yake na kutoa nafasi kwa fikra tofauti hata kama itatokea kwa kuchelewa kidogo.
 
Hakuna wema ndani ya ccm. Shetani hawezi kutubu na sidhani hata kama Mungu naweza kuikubali hiyo toba. CCM haiaminiki hata kwa mtoto mdogo, Cham- msingi, ili nchi hii ijiokoe ni lazima CCM waondoke, Wakiondoka tutaipata Tanganyika, na Zanzibar watakuwa watakuwa huru.

Muungano utakufa, na pengine hatutaungana milele.
Kuanzia hapo tutaanza upya, tutakuwa tumeupata uhuru wetu upya na tutaanza mambo yetu upya kabisa.

Ila kwa hali hii iliyopo, usitegemee chochote kutoka ccm.
Naunga mkono hoja yako,iko haja ya ccm kukaa pembeni je baada ya CCM kukaa pembeni mbadala ni nani?,maana uchaguzi umekaribia
 
Nakubaliana kabisa na wewe kabisa, mchango wa Oscar Kambona kwa hili taifa ni mkubwa mno, tena mkubwa sana. Nadhani hakustahili kufanyiwa vile na kina Mzee Nyerere. Nadhani njia sahihi ilikuwa kumuweka pembeni kuliko kumchafua vile mtu aluetoa mchango mkubwa kwa taifa:​
  1. Kambona alivyoingia TANU ndani ya mwaka mmoja alikusanya wanachama 10000.​
  2. Ndiye aliyeunda mifumo ya usalama hapa nchini akishauri kwamba vijana wa TYL ndiyo waingizwe kwenye idara mpya ya usalama wa taifa. Yeye ndiye aliyeenda kwa waisraeli ili watoe mafunzo kwa watanzania.​
  3. Ndiye aliyezima uasi wa kijeshi wa KAR mwaka 1964 wakati Mzee Nyerere na Rashidi Kawawa wakiwa wamefichwa. Angekuwa ni mtu mbaya basi baadhi ya wanajeshi walipomwambia ajitangaze kuwa Raisi alikataa mzee wa watu.​
  4. Kambona ndiye ARCHITECH wa FOREIGN POLICY ya Tanzania, alichokuwa anakizungumza Kambona miaka ya 60's mwanzoni ndicho ambacho Mzee Nyerere alikuwa akikizungumza miaka yote ya utawala wake.​
Kambona was forced into the Dark-Side. Mambo mabaya aliyofanyiwa ndiyo yalipelekea Kambona aje kuwa na moyo mgumu vile. Mzee Nyerere alimwogopa Kambona hadi mwisho kwasababu yeye ni mmoja kati ya watu waliokuwa wanamfahamu Nyerere kiundani (Hulka na Madhaifu yake), jambo ambalo Nyerere hakulipenda ukizingatia alishajitengenezea A CULT OF PERSONALITY.​
Kambona alitoa ushirikiano kwa kina Hanga na wenzake kufanikisha mapinduzi ya Zanzibar na baadae muungano kuzaliwa,ila kilichofuata ni historia.....huenda kilichompata Kambona ni Karma pia.

JokaKuu zitto junior Nguruvi3
 
Nilishawahi kuandika, kwenye siasa ukitenda uovu hasa wa usaliti au mauaji. Kaa ukijua nawe utafanyiwa vivyohivyo na yule ambaye ulimuamini.

Kuna kijana mmoja ambaye ninamtabiria ndiye atakaye endeleza laana ya kisasi cha usaliti na mauaji kwa masalia. Yupo na kila siku anaonyesha uwepo wake
 
Hili jambo la WAISLAMU na WAKATOLIKI kupokezana MADARAKA linaumiza mno.

YAANI WAISLAMU NA WAKATOLIKI wameshafanya nafasi ya URAIS kuwa yao.
Labda ungesema Waislamu na Wakatoliki.
 
Back
Top Bottom