Nakaribia kudhulumiwa, naombeni ushauri

Nakaribia kudhulumiwa, naombeni ushauri

Nitamfanya nini?? Aisee

Kwani kinachothibitisha umiliki wa nyumba ni hati ya nyumba au existance ya mtu kwenye nyumba hiyo?

Hili swali ni la ajabu sana mkuu

Mamlaka kama Mahakama zipo mkuu, naweza kumtoa kwa nguvu kwa amri ya Mahakama, lakini huyu ni bwana mdogo sana siwezi kufika huko. Najua namna ya ku-deal nae.
Hujawahi kusikia malalamiko ya mwenye nyumba kuzulumiwa na mpangaji?
 
Nimesikia kuna ushirikiano wa hali ya juu sana. Wanadai ni afadhali ufanye ufedhuli jeshini kuliko uraiani kwasababu unakuwa unalidhalilisha jeshi.

Na mara nyingi ukiweza ku-justify madai yako huwa wanamkopesha askari husika kwa lazima wakulipe halafu watamkata kwa utaratibu wanaoujua wao.
Sasa kama ni hivyo unakwama wapi
 
Wakuu habarini za wakati huu. Naandika uzi huu nikiwa na simanzi sana!

Nina eneo langu Ukonga KMKM ambapo nimejenga nyumba moja kubwa ya kupangisha na vyumba vingine 4 vyenye sebule na choo ndani. Nimefanya uwekezaji huu kwa kujinyima sana tena nikitumia pesa yangu halali.

Mimi siishi Dsm kwa sasa. Changamoto ipo kwa mpangaji mmoja bwana mdogo ambaye ni Mwanajeshi mwenye cheo cha Coplo, ni rika langu, yuko kati ya 30-37; ananisumbua sana kulipa kodi. Nimemvumilia vya kutosha. Pamoja na kuweka kodi ndogo lakini bado jamaa ananisumbua mno.

So far namdai zaidi ya milioni moja. Kuna wakati nasafiri kwenda Dar kutazama maendeleo ya makazi yangu na nakutanaga nae lakini anaishia kunipiga sound. Jamaa ni mtaratibu sana, anazungumza kwa upole; kila nikijaribu kumtoa hata kwa kumsamehe hiyo kodi huwa napatwa na huruma.

Kwa sasa enough is enough. Mara ya mwisho nimekutana nae Desemba mwaka jana, akakiri kwa maandishi kwamba namdai na atalipa deni lote Jan. 29 mwaka huu. Kilichotokea ni kwamba tarehe 29 imepita na kakaa kimya! Nikimpigia simu zangu hapokei. Kwasababu niko mbali, nimemtuma mpangaji wangu mmoja ninayemwamwini ili anipe nizungumze nae ila inasemekana jamaa hayupo pale kwa takribani wiki 3, kuna tetesi ameenda kwenye kozi Kibaha.

Ningeweza kwenda kumshtaki kambini kwake lakini sijui yuko kambi gani, kuna wanaosema yuko Lugalo ila hawana uhakika.

Naombeni msaada wakuu, naamini kuna watu ni Wanajeshi humu, wengine mna ndugu zenu Jeshini na hamuwezi kukubali dhuluma ya namna hii, naombeni msaada wa namna ya kuitambua kambi yake, majina yake nayajua, niko tayari kumsamehe hiyo kodi ila anipishe ili nitafute mpangaji mwingine.

Naomba kuwasilisha.

N:B: Wapangaji wote wana Mikataba. Kimsingi huyu jamaa ameshavunja terms za Mkataba muda mrefu. Naweza kumdai kodi Kimahakama lakini sitaki kupoteza muda.
Nenda kwa mkuu wake wakazi....namaandishi hayo kama ushaidi,utanishukuru baadaye
 
Wote huwa ni wamoja, raia anaweza asisikilizwe.
Sio kweli kuna jamaa ni fundi ujenzi iliwahi mtokea kuna mjeda mmoja *2 alimuita fundi kuja mrekebishia nyumba yake na fundi alivyomaliza jamaa akawa anamzingua kumlipa hela kama laki 5 hivi na ushee kila fundi akikumbushia kuhusu hela yake jamaa anamletea vitisho vingi mixer matusi jamaa akaona sasa amefika ukingoni akaomba ushauri kwa wadau wakampa muongozo jinsi ya kwenda kupata haki yake jamaa akaufuata mpaka akafika kwa mwajiri wake jeshini nadhani ni upanga akapokelewa nakutoa malalamiko yake hapo hapo jamaa akapigiwa simu akaulizwa uko wapi jamaa akasema sijui yuko mwenge akaambiwa nakupa dakika 15 uwe umeshafika hapa, kweli bhana jamaa akafika ile anaingia tu anakutana na jamaa anayemdai akashtuka kilichooendelea hapo ni siri ya kambi ila mkuu wake aliamlisha akatwe kwenye mshahara wake na fundi aliondoka na mzigo wake siku ile ile
 
Sio kweli kuna jamaa ni fundi ujenzi iliwahi mtokea kuna mjeda mmoja *2 alimuita fundi kuja mrekebishia nyumba yake na fundi alivyomaliza jamaa akawa anamzingua kumlipa hela kama laki 5 hivi na ushee kila fundi akikumbushia kuhusu hela yake jamaa anamletea vitisho vingi mixer matusi jamaa akaona sasa amefika ukingoni akaomba ushauri kwa wadau wakampa muongozo jinsi ya kwenda kupata haki yake jamaa akaufuata mpaka akafika kwa mwajiri wake jeshini nadhani ni upanga akapokelewa nakutoa malalamiko yake hapo hapo jamaa akapigiwa simu akaulizwa uko wapi jamaa akasema sijui yuko mwenge akaambiwa nakupa dakika 15 uwe umeshafika hapa, kweli bhana jamaa akafika ile anaingia tu anakutana na jamaa anayemdai akashtuka kilichooendelea hapo ni siri ya kambi ila mkuu wake aliamlisha akatwe kwenye mshahara wake na fundi aliondoka na mzigo wake siku ile ile
Inategemea na aina ya bosi
 
Inategemea na aina ya bosi
Inategemea na aina ya bosi
Chief kule makao makuu yao huwezi fanywa kitu chochote maana cdf wao yupogo kule alaf jeshi ni nidham kwanza yule *2 alivyofika tu kwa mwajir wake akaambiwa apunguze urefu mbele ya jamaa aliyepeleka malalamiko ndio akaanza kujibu maswali aliyoulizwa na boss wake ambae ni mwajiri wake ……..kwaiyo iyo kitu unayowaza wewe kule hakuna nii nadhalia tu za mitaani izo tumejimezesha
 
Wakuu habarini za wakati huu. Naandika uzi huu nikiwa na simanzi sana!

Nina eneo langu Ukonga KMKM ambapo nimejenga nyumba moja kubwa ya kupangisha na vyumba vingine 4 vyenye sebule na choo ndani. Nimefanya uwekezaji huu kwa kujinyima sana tena nikitumia pesa yangu halali.

Mimi siishi Dsm kwa sasa. Changamoto ipo kwa mpangaji mmoja bwana mdogo ambaye ni Mwanajeshi mwenye cheo cha Coplo, ni rika langu, yuko kati ya 30-37; ananisumbua sana kulipa kodi. Nimemvumilia vya kutosha. Pamoja na kuweka kodi ndogo lakini bado jamaa ananisumbua mno.

So far namdai zaidi ya milioni moja. Kuna wakati nasafiri kwenda Dar kutazama maendeleo ya makazi yangu na nakutanaga nae lakini anaishia kunipiga sound. Jamaa ni mtaratibu sana, anazungumza kwa upole; kila nikijaribu kumtoa hata kwa kumsamehe hiyo kodi huwa napatwa na huruma.

Kwa sasa enough is enough. Mara ya mwisho nimekutana nae Desemba mwaka jana, akakiri kwa maandishi kwamba namdai na atalipa deni lote Jan. 29 mwaka huu. Kilichotokea ni kwamba tarehe 29 imepita na kakaa kimya! Nikimpigia simu zangu hapokei. Kwasababu niko mbali, nimemtuma mpangaji wangu mmoja ninayemwamwini ili anipe nizungumze nae ila inasemekana jamaa hayupo pale kwa takribani wiki 3, kuna tetesi ameenda kwenye kozi Kibaha.

Ningeweza kwenda kumshtaki kambini kwake lakini sijui yuko kambi gani, kuna wanaosema yuko Lugalo ila hawana uhakika.

Naombeni msaada wakuu, naamini kuna watu ni Wanajeshi humu, wengine mna ndugu zenu Jeshini na hamuwezi kukubali dhuluma ya namna hii, naombeni msaada wa namna ya kuitambua kambi yake, majina yake nayajua, niko tayari kumsamehe hiyo kodi ila anipishe ili nitafute mpangaji mwingine.

Naomba kuwasilisha.

N:B: Wapangaji wote wana Mikataba. Kimsingi huyu jamaa ameshavunja terms za Mkataba muda mrefu. Naweza kumdai kodi Kimahakama lakini sitaki kupoteza muda.
Hawa wajeda wapuuzi sana.
Nilipanga kwa mmoja, ila nyumba ilitaka ukarabati kabla ya kuingia. Jamaa kasema hana pesa, nitangulize kodi ili aitumie kurekebisha nikaona fresh.. nimelipia miezi 6 akasema ndani ya siku tatu kutakuwa tayari. Siku 3,5,wiki, wiki ya pili.. nkaona mazoea yanazidi nikaamua kumjia juu, akasema njoo ulete vitu nyumba tayari. Nikaenda kupaona aisee.. ukarabati low budget.. choo hajaweka mlango. Nkamwambia mwenye nyumba jiheshimu basi, me naingiaje kuko hivi.. eti ooh nimeona una haraka sana, sasa we leta tuu vitu af tutaendelea kupaweka sawa. Nkamwambia siingii nyumba iko hivi.

Maneno yakawa mengi, mwisho wa siku tukashindwana nkamwambia anirudishie kodi yangu siingii kwake tena.. tukenda mpaka kuandikishana kwa mwenyekiti wa mtaa. Kufika kwa Mwenyekiti kumbe wanafahamiana lakini tukaenda hivyo hivyo. Makubaliano yalikuwa anilipe baada ya mwezi. Yaaani anavyonisumbua saivi.. Bora nichukue namba pale juu nimrogee.. maana haiwezekani pesa yangu inisumbue tena kuifuatilia. Yeye kakaa kimya, mimi nna kazi ya kumpigia daily, na kiswahili kingi.. shida saivi tupo mikoa tofauti.. Bora nimroge tuu.. at akifa sio mbaya.
 
Sio kweli kuna jamaa ni fundi ujenzi iliwahi mtokea kuna mjeda mmoja *2 alimuita fundi kuja mrekebishia nyumba yake na fundi alivyomaliza jamaa akawa anamzingua kumlipa hela kama laki 5 hivi na ushee kila fundi akikumbushia kuhusu hela yake jamaa anamletea vitisho vingi mixer matusi jamaa akaona sasa amefika ukingoni akaomba ushauri kwa wadau wakampa muongozo jinsi ya kwenda kupata haki yake jamaa akaufuata mpaka akafika kwa mwajiri wake jeshini nadhani ni upanga akapokelewa nakutoa malalamiko yake hapo hapo jamaa akapigiwa simu akaulizwa uko wapi jamaa akasema sijui yuko mwenge akaambiwa nakupa dakika 15 uwe umeshafika hapa, kweli bhana jamaa akafika ile anaingia tu anakutana na jamaa anayemdai akashtuka kilichooendelea hapo ni siri ya kambi ila mkuu wake aliamlisha akatwe kwenye mshahara wake na fundi aliondoka na mzigo wake siku ile ile
Hii scenario yako imenitia moyo sana mkuu. Nashukuru mno! Umebaki utekelezaji tu.
 
Chief kule makao makuu yao huwezi fanywa kitu chochote maana cdf wao yupogo kule alaf jeshi ni nidham kwanza yule *2 alivyofika tu kwa mwajir wake akaambiwa apunguze urefu mbele ya jamaa aliyepeleka malalamiko ndio akaanza kujibu maswali aliyoulizwa na boss wake ambae ni mwajiri wake ……..kwaiyo iyo kitu unayowaza wewe kule hakuna nii nadhalia tu za mitaani izo tumejimezesha
Bravo mkuu!
 
Back
Top Bottom