Nakaribia kudhulumiwa, naombeni ushauri

Nakaribia kudhulumiwa, naombeni ushauri

Nadhani j3 ingekuwa bora zaidi
Sawa mkuu.

Nitajaribu jmosi kwasababu nitakuwa mitaa ile kwa shughuli nyingine, ikishindikana basi nitarudi tena j3 kwasababu bado nitakuwepo Dsm.
 
Nenda kachukue dawa kwa mganga ukija iweka ukafagia na ufagio wakat anatoka hatarudi Tena atasahau Hadi vitu vyake humor ndani
 
Wakuu habarini za wakati huu. Naandika uzi huu nikiwa na simanzi sana!

Nina eneo langu Ukonga KMKM ambapo nimejenga nyumba moja kubwa ya kupangisha na vyumba vingine 4 vyenye sebule na choo ndani. Nimefanya uwekezaji huu kwa kujinyima sana tena nikitumia pesa yangu halali.

Mimi siishi Dsm kwa sasa. Changamoto ipo kwa mpangaji mmoja bwana mdogo ambaye ni Mwanajeshi mwenye cheo cha Coplo, ni rika langu, yuko kati ya 30-37; ananisumbua sana kulipa kodi. Nimemvumilia vya kutosha. Pamoja na kuweka kodi ndogo lakini bado jamaa ananisumbua mno.

So far namdai zaidi ya milioni moja. Kuna wakati nasafiri kwenda Dar kutazama maendeleo ya makazi yangu na nakutanaga nae lakini anaishia kunipiga sound. Jamaa ni mtaratibu sana, anazungumza kwa upole; kila nikijaribu kumtoa hata kwa kumsamehe hiyo kodi huwa napatwa na huruma.

Kwa sasa enough is enough. Mara ya mwisho nimekutana nae Desemba mwaka jana, akakiri kwa maandishi kwamba namdai na atalipa deni lote Jan. 29 mwaka huu. Kilichotokea ni kwamba tarehe 29 imepita na kakaa kimya! Nikimpigia simu zangu hapokei. Kwasababu niko mbali, nimemtuma mpangaji wangu mmoja ninayemwamwini ili anipe nizungumze nae ila inasemekana jamaa hayupo pale kwa takribani wiki 3, kuna tetesi ameenda kwenye kozi Kibaha.

Ningeweza kwenda kumshtaki kambini kwake lakini sijui yuko kambi gani, kuna wanaosema yuko Lugalo ila hawana uhakika.

Naombeni msaada wakuu, naamini kuna watu ni Wanajeshi humu, wengine mna ndugu zenu Jeshini na hamuwezi kukubali dhuluma ya namna hii, naombeni msaada wa namna ya kuitambua kambi yake, majina yake nayajua, niko tayari kumsamehe hiyo kodi ila anipishe ili nitafute mpangaji mwingine.

Naomba kuwasilisha.

N:B: Wapangaji wote wana Mikataba. Kimsingi huyu jamaa ameshavunja terms za Mkataba muda mrefu. Naweza kumdai kodi Kimahakama lakini sitaki kupoteza muda.
Ahaaaa!! Mkuu hilo suala nalo ni la kulia lia?!! Achana na mambo ya jeshi kwenye jambo hili wala halihusiani kabisa!! Huyo ni raia kama raia mwingine,.
 
MREJESHO:

Kama wengi mlivyoshauri, jana nilifika Ngome-Upanga majira ya saa 9 alasiri. Nikapokelewa na na maafande pale getini nikaulizwa shida yangu, nikajieleza kwa ufupi, kabla ya kukaribishwa ndani nikapewa kiti kwanza nikae palepale getini na kupewa pole!

Afande mmoja muungwana sana ambaye alionekana ndio kiongozi wa walinzi wa siku ya jana pale getini, akaniomba nionyeshe nyaraka zozote (kama ninazo) kuthibitisha namdai. Nikatoa mkataba na commitment aliyoifanya Kwa maandishi nilipokutana nae mara ya mwisho Desemba mwaka Jana na kuahidi kunilipa ifikapo tar 29/01/2024.

Kwanza maafande wakanishangaa kwanini nimemruhusu akae muda wote huo bila kumbananisha alipe au nimfukuze.

Wakaniuliza kama nina picha yake nikawaonyesha picha yake aliyoweka Whatsapp. Baadhi ya maafande wakamtambua.

Wakaniomba sana kwamba nisipeleke hili swala ndani, watakachofanya ni kwamba watawasiliana nae ili j3 aje alipe au kama hana pesa achukue mkopo anilipe j3 hiyohiyo.

Kwahiyo wakaniomba nifike Ngome j3 kabla ya saa sita mchana. Nitamkuta mdeni wangu. Nikachukua namba ya yule afande in charge nikasepa zangu.

Wakuu, leo asubuhi wakati naamka nimekuta msg za mdeni wangu akinibembeleza kwamba j3 tukutane pale Ngome nje anilipe pesa yangu yote . Nadhani wale maafande wenzake wameshampigia.

Ndugu zangu, nawashukuru sana kwa ushauri. JF forever! Nimepanga akishanilipa tu j3 namlamba na notice ya mwezi mmoja ahame.

ASANTENI SANA NA MUNGU AWABARIKI.
 
MREJESHO:

Kama wengi mlivyoshauri, jana nilifika Ngome-Upanga majira ya saa 9 alasiri. Nikapokelewa na na maafande pale getini nikaulizwa shida yangu, nikajieleza kwa ufupi, kabla ya kukaribishwa ndani nikapewa kiti kwanza nikae palepale getini na kupewa pole!

Afande mmoja muungwana sana ambaye alionekana ndio kiongozi wa walinzi wa siku ya jana pale getini, akaniomba nionyeshe nyaraka zozote (kama ninazo) kuthibitisha namdai. Nikatoa mkataba na commitment aliyoifanya Kwa maandishi nilipokutana nae mara ya mwisho Desemba mwaka Jana na kuahidi kunilipa ifikapo tar 29/01/2024.

Kwanza maafande wakanishangaa kwanini nimemruhusu akae muda wote huo bila kumbananisha alipe au nimfukuze.

Wakaniuliza kama nina picha yake nikawaonyesha picha yake aliyoweka Whatsapp. Baadhi ya maafande wakamtambua.

Wakaniomba sana kwamba nisipeleke hili swala ndani, watakachofanya ni kwamba watawasiliana nae ili j3 aje alipe au kama hana pesa achukue mkopo anilipe j3 hiyohiyo.

Kwahiyo wakaniomba nifike Ngome j3 kabla ya saa sita mchana. Nitamkuta mdeni wangu. Nikachukua namba ya yule afande in charge nikasepa zangu.

Wakuu, leo asubuhi wakati naamka nimekuta msg za mdeni wangu akinibembeleza kwamba j3 tukutane pale Ngome nje anilipe pesa yangu yote . Nadhani wale maafande wenzake wameshampigia.

Ndugu zangu, nawashukuru sana kwa ushauri. JF forever! Nimepanga akishanilipa tu j3 namlamba na notice ya mwezi mmoja ahame.

ASANTENI SANA NA MUNGU AWABARIKI.
Halafu nafkiri kuna shida ya viongozi au sisi watu tunaofanya kazi huku chini chini. Hapo Ngome ukifika wanakupokea vizuri kuliko makambini. Sehemu ya majeshi wanayokupokea kwa changamoto zaidi ni pale Makumbusho
 
Nyie wanajeshi wa karne hii ni matapeli mbayaaa 😂😂🤣🤣 sijui wanakwama wapiii.
Halafu ni wababe vibaya mno heri huyo unamdai hela nyingi.... kuna huyu jamaa alikopa vitu dukani vya elfu 40,000 tu lakini ni miezi inakatika
 
Halafu nafkiri kuna shida ya viongozi au sisi watu tunaofanya kazi huku chini chini. Hapo Ngome ukifika wanakupokea vizuri kuliko makambini. Sehemu ya majeshi wanayokupokea kwa changamoto zaidi ni pale Makumbusho
Ni kweli mkuu. Sijui huku chini kuna shida gani yani . Watu wamejaa viburi sana.
 
Nyie wanajeshi wa karne hii ni matapeli mbayaaa sijui wanakwama wapiii.
Halafu ni wababe vibaya mno heri huyo unamdai hela nyingi.... kuna huyu jamaa alikopa vitu dukani vya elfu 40,000 tu lakini ni miezi inakatika
Ajabu sana mkuu! Dawa yao ni kwenda kuwaripoti tu. Wakati mwingine shida inakuwa sio pesa ila kuwafundisha uungwana na kuepusha madhara kwa watu wengine.
 
MREJESHO:

Kama wengi mlivyoshauri, jana nilifika Ngome-Upanga majira ya saa 9 alasiri. Nikapokelewa na na maafande pale getini nikaulizwa shida yangu, nikajieleza kwa ufupi, kabla ya kukaribishwa ndani nikapewa kiti kwanza nikae palepale getini na kupewa pole!

Afande mmoja muungwana sana ambaye alionekana ndio kiongozi wa walinzi wa siku ya jana pale getini, akaniomba nionyeshe nyaraka zozote (kama ninazo) kuthibitisha namdai. Nikatoa mkataba na commitment aliyoifanya Kwa maandishi nilipokutana nae mara ya mwisho Desemba mwaka Jana na kuahidi kunilipa ifikapo tar 29/01/2024.

Kwanza maafande wakanishangaa kwanini nimemruhusu akae muda wote huo bila kumbananisha alipe au nimfukuze.

Wakaniuliza kama nina picha yake nikawaonyesha picha yake aliyoweka Whatsapp. Baadhi ya maafande wakamtambua.

Wakaniomba sana kwamba nisipeleke hili swala ndani, watakachofanya ni kwamba watawasiliana nae ili j3 aje alipe au kama hana pesa achukue mkopo anilipe j3 hiyohiyo.

Kwahiyo wakaniomba nifike Ngome j3 kabla ya saa sita mchana. Nitamkuta mdeni wangu. Nikachukua namba ya yule afande in charge nikasepa zangu.

Wakuu, leo asubuhi wakati naamka nimekuta msg za mdeni wangu akinibembeleza kwamba j3 tukutane pale Ngome nje anilipe pesa yangu yote . Nadhani wale maafande wenzake wameshampigia.

Ndugu zangu, nawashukuru sana kwa ushauri. JF forever! Nimepanga akishanilipa tu j3 namlamba na notice ya mwezi mmoja ahame.

ASANTENI SANA NA MUNGU AWABARIKI.
We una moyo mlainiiii 👀
Mimi ningeenda kumreport ndani tu akapate na adhabu huko kambini😂
 
MREJESHO:

Kama wengi mlivyoshauri, jana nilifika Ngome-Upanga majira ya saa 9 alasiri. Nikapokelewa na na maafande pale getini nikaulizwa shida yangu, nikajieleza kwa ufupi, kabla ya kukaribishwa ndani nikapewa kiti kwanza nikae palepale getini na kupewa pole!

Afande mmoja muungwana sana ambaye alionekana ndio kiongozi wa walinzi wa siku ya jana pale getini, akaniomba nionyeshe nyaraka zozote (kama ninazo) kuthibitisha namdai. Nikatoa mkataba na commitment aliyoifanya Kwa maandishi nilipokutana nae mara ya mwisho Desemba mwaka Jana na kuahidi kunilipa ifikapo tar 29/01/2024.

Kwanza maafande wakanishangaa kwanini nimemruhusu akae muda wote huo bila kumbananisha alipe au nimfukuze.

Wakaniuliza kama nina picha yake nikawaonyesha picha yake aliyoweka Whatsapp. Baadhi ya maafande wakamtambua.

Wakaniomba sana kwamba nisipeleke hili swala ndani, watakachofanya ni kwamba watawasiliana nae ili j3 aje alipe au kama hana pesa achukue mkopo anilipe j3 hiyohiyo.

Kwahiyo wakaniomba nifike Ngome j3 kabla ya saa sita mchana. Nitamkuta mdeni wangu. Nikachukua namba ya yule afande in charge nikasepa zangu.

Wakuu, leo asubuhi wakati naamka nimekuta msg za mdeni wangu akinibembeleza kwamba j3 tukutane pale Ngome nje anilipe pesa yangu yote . Nadhani wale maafande wenzake wameshampigia.

Ndugu zangu, nawashukuru sana kwa ushauri. JF forever! Nimepanga akishanilipa tu j3 namlamba na notice ya mwezi mmoja ahame.

ASANTENI SANA NA MUNGU AWABARIKI.
Kumbe inawezekana eeh? Nitaenda na mimi
 
Back
Top Bottom