Nakaribia kudhulumiwa, naombeni ushauri

Nakaribia kudhulumiwa, naombeni ushauri

Wakuu habarini za wakati huu. Naandika uzi huu nikiwa na simanzi sana!

Nina eneo langu Ukonga KMKM ambapo nimejenga nyumba moja kubwa ya kupangisha na vyumba vingine 4 vyenye sebule na choo ndani. Nimefanya uwekezaji huu kwa kujinyima sana tena nikitumia pesa yangu halali.

Mimi siishi Dsm kwa sasa. Changamoto ipo kwa mpangaji mmoja bwana mdogo ambaye ni Mwanajeshi mwenye cheo cha Coplo, ni rika langu, yuko kati ya 30-37; ananisumbua sana kulipa kodi. Nimemvumilia vya kutosha. Pamoja na kuweka kodi ndogo lakini bado jamaa ananisumbua mno.

So far namdai zaidi ya milioni moja. Kuna wakati nasafiri kwenda Dar kutazama maendeleo ya makazi yangu na nakutanaga nae lakini anaishia kunipiga sound. Jamaa ni mtaratibu sana, anazungumza kwa upole; kila nikijaribu kumtoa hata kwa kumsamehe hiyo kodi huwa napatwa na huruma.

Kwa sasa enough is enough. Mara ya mwisho nimekutana nae Desemba mwaka jana, akakiri kwa maandishi kwamba namdai na atalipa deni lote Jan. 29 mwaka huu. Kilichotokea ni kwamba tarehe 29 imepita na kakaa kimya! Nikimpigia simu zangu hapokei. Kwasababu niko mbali, nimemtuma mpangaji wangu mmoja ninayemwamwini ili anipe nizungumze nae ila inasemekana jamaa hayupo pale kwa takribani wiki 3, kuna tetesi ameenda kwenye kozi Kibaha.

Ningeweza kwenda kumshtaki kambini kwake lakini sijui yuko kambi gani, kuna wanaosema yuko Lugalo ila hawana uhakika.

Naombeni msaada wakuu, naamini kuna watu ni Wanajeshi humu, wengine mna ndugu zenu Jeshini na hamuwezi kukubali dhuluma ya namna hii, naombeni msaada wa namna ya kuitambua kambi yake, majina yake nayajua, niko tayari kumsamehe hiyo kodi ila anipishe ili nitafute mpangaji mwingine.

Naomba kuwasilisha.

N:B: Wapangaji wote wana Mikataba. Kimsingi huyu jamaa ameshavunja terms za Mkataba muda mrefu. Naweza kumdai kodi Kimahakama lakini sitaki kupoteza muda.
Pole sana ndgu! Ulicheka na nyani sasa unavuna mabuwa. Ktk biashara ondoa kitu kinachoitwa huruma, Kuna watu hawana mishipa ya aibu.
 
Khaa!kwa hiyo wapo juu ya sheria au ameyatimba kivipi?Acha kumtisha mwenzio
Sio wapo juu ya sheria hao jamaa wanajipata sana, inakuwaje mjeda ashindwe kulipa kodi huoni kuna tatizo hapo, haiwezekani kushindwa kulipa kodi wakati anapokea mshahara mara mbili kila mwezi, ninachohisi kuna mchezo anamchezea ameona jamaa muoga, mimi kumwambia hivyo sio kumtisha ni kumzindua tu aamke kutoka usingizini, mimi naishi mwenyewe kwenye nyumba yangu na vyumba vipo na umaskini wangu nilionao sijawahi kuwaza kupangisha mtu yeyote, kama ingelikuwa ni lazima kupangisha kwa kujiongezea kipato, hata siku moja haitotokea kukaa na magwanda wa aina yeyote kujadiliana nae mkataba wa kupangishana, hapo ndipo alipoyatimba, umenielewa?
 
Ni vile tu sina muda mkuu.

Ila ningeamua kuruka naye mbona hakuna rangi angeacha kuona.

Ni vile tu kila nikifikiria kumuharibia mtu kibarua chake roho inakuwa nzito.
Kwa nini umuharibie kibarua chake wakati ishu ni simple tu, cha msingi usiende kwa ubabe hao jamaa wanafagilia sana mambo hayo utakuja kushtuka uko mbinguni washakutoa roho, kwanza wana umoja kishenzi halafu kama nati zimelegea fujo ndio wanalolipenda, nenda nae kistaarabu na mpe muda ahame, akishindwa muondoe kwa sheria zinavyotaka, siku ukimuhamisha usiende peke yako nenda na serikali nzima itakuwa ngumu kukuattack,
 
H
Unajua umeandika kama sisi humu ndio majirani zake huyo afande, sikiliza mdogo wangu, wakati wowote unapopatwa na tatizo lolote jaribu kuwa mtulivu na kama unahitaji ushauri toa maelezo ya kutosha yanayohusiana na msaada unaohitaji, pia usikurupuke kutoa hukumu au kuchukuwa maamuzi kwa kutumia hasira au utashi wako binafsi, unaweza kuwa umeonewa, umedhulumiwa, au vyovyote itakavyokuwa, lakini dunia hii haki pekee haikufanyi uwe na sauti mbele ya mamlaka au sheria, hususan upande huo wa magwanda, kwao wao hakuna sheria za duniani wala za mbinguni zinazofanya kazi, kwahiyo kuwa makini huyo anaweza hata kukunyanganya hiyo nyumba akasema ni yake na mamlaka ikakuweka wewe ndani na kusema ulitaka kumdhulumu, kwa kifupi umeyatimba, nakushauri mvumilie na mpe siku au mwezi kama hajalipa mwambie mimi nyumba nauza, utamuwachia msala huyo atakaekuja kununua, kwa kifupi umeyatimba.
Hopeless kabisa wew....ukisoma ulichoandika utaweza jicheka.....yaan niuze nyumba kwa kuhofia mpangaji?
 
Ndiyo tatizo la hawa CPL, huwa wanapenda wahudumiwe kwa kutukuzwa flani, kwa kuwa alipita Depo. Ni uonevu huu, pole sana.

Mpe notice kwanza ili uwe umefuata taratibu za kumwondoa. Kisha ndiyo ziende harakati za kiutaratibu za kumtoa kwenye nyumba yako.

Kama akiendelea ksumbua kutoka na kulipa malimbikizo ya deni, na kwa kuwa hujui kambi yake, basi peleka shauri lake HQ (Upanga) ila jitahidi uwe na nyaraka zote.

Ova
 
Ndiyo tatizo la hawa CPL, huwa wanapenda wahudumiwe kwa kutukuzwa flani, kwa kuwa alipita Depo. Ni uonevu huu, pole sana.


Ova
Mimi hao ndio huwa nawakomesha, akishaleta swaga za ujeshi akidhani ananitisha ndipo ninapofurahi, kama nilikuwa namhudumia kwa unyenyekevu nabadili, tunaenda sawa.

Ila sio katika namna ya kuvunjiana heshima, nambana kwa kutumia utaratibu uliowekwa. Sijui kwanini, mwisho huwa wanakuwa wapole.

Atanifanya nini? Kichwani kuna mtu ananipaga kiburi nitakuja kupigwa mimi jamani!
 
Wakuu habarini za wakati huu. Naandika uzi huu nikiwa na simanzi sana!

Nina eneo langu Ukonga KMKM ambapo nimejenga nyumba moja kubwa ya kupangisha na vyumba vingine 4 vyenye sebule na choo ndani. Nimefanya uwekezaji huu kwa kujinyima sana tena nikitumia pesa yangu halali.

Mimi siishi Dsm kwa sasa. Changamoto ipo kwa mpangaji mmoja bwana mdogo ambaye ni Mwanajeshi mwenye cheo cha Coplo, ni rika langu, yuko kati ya 30-37; ananisumbua sana kulipa kodi. Nimemvumilia vya kutosha. Pamoja na kuweka kodi ndogo lakini bado jamaa ananisumbua mno.

So far namdai zaidi ya milioni moja. Kuna wakati nasafiri kwenda Dar kutazama maendeleo ya makazi yangu na nakutanaga nae lakini anaishia kunipiga sound. Jamaa ni mtaratibu sana, anazungumza kwa upole; kila nikijaribu kumtoa hata kwa kumsamehe hiyo kodi huwa napatwa na huruma.

Kwa sasa enough is enough. Mara ya mwisho nimekutana nae Desemba mwaka jana, akakiri kwa maandishi kwamba namdai na atalipa deni lote Jan. 29 mwaka huu. Kilichotokea ni kwamba tarehe 29 imepita na kakaa kimya! Nikimpigia simu zangu hapokei. Kwasababu niko mbali, nimemtuma mpangaji wangu mmoja ninayemwamwini ili anipe nizungumze nae ila inasemekana jamaa hayupo pale kwa takribani wiki 3, kuna tetesi ameenda kwenye kozi Kibaha.

Ningeweza kwenda kumshtaki kambini kwake lakini sijui yuko kambi gani, kuna wanaosema yuko Lugalo ila hawana uhakika.

Naombeni msaada wakuu, naamini kuna watu ni Wanajeshi humu, wengine mna ndugu zenu Jeshini na hamuwezi kukubali dhuluma ya namna hii, naombeni msaada wa namna ya kuitambua kambi yake, majina yake nayajua, niko tayari kumsamehe hiyo kodi ila anipishe ili nitafute mpangaji mwingine.

Naomba kuwasilisha.

N:B: Wapangaji wote wana Mikataba. Kimsingi huyu jamaa ameshavunja terms za Mkataba muda mrefu. Naweza kumdai kodi Kimahakama lakini sitaki kupoteza muda.
Una uhakika nyumba ni yako na una uhakika wewe ni mwanaume?
 
Unajua umeandika kama sisi humu ndio majirani zake huyo afande, sikiliza mdogo wangu, wakati wowote unapopatwa na tatizo lolote jaribu kuwa mtulivu na kama unahitaji ushauri toa maelezo ya kutosha yanayohusiana na msaada unaohitaji, pia usikurupuke kutoa hukumu au kuchukuwa maamuzi kwa kutumia hasira au utashi wako binafsi, unaweza kuwa umeonewa, umedhulumiwa, au vyovyote itakavyokuwa, lakini dunia hii haki pekee haikufanyi uwe na sauti mbele ya mamlaka au sheria, hususan upande huo wa magwanda, kwao wao hakuna sheria za duniani wala za mbinguni zinazofanya kazi, kwahiyo kuwa makini huyo anaweza hata kukunyanganya hiyo nyumba akasema ni yake na mamlaka ikakuweka wewe ndani na kusema ulitaka kumdhulumu, kwa kifupi umeyatimba, nakushauri mvumilie na mpe siku au mwezi kama hajalipa mwambie mimi nyumba nauza, utamuwachia msala huyo atakaekuja kununua, kwa kifupi umeyatimba.
Akili za loser hizi..umejaa uoga mwili mzima
 
Achana na mambo ya kufatana kazini...wewe mwambie ahame tu kwani amekataa ?

Utatengeneza bifu zito kama ukianza mambo hayo ya kuhalibiana kazi.
Mkuu, sio kwamba bifu siliwezi, nalimudu haswa, huyu ni bwana mdg sana kwangu.

Nataka ajifunze, asije akafanya kama alivyofanya kwangu akihamia kwengine.
 
Kwa nini umuharibie kibarua chake wakati ishu ni simple tu, cha msingi usiende kwa ubabe hao jamaa wanafagilia sana mambo hayo utakuja kushtuka uko mbinguni washakutoa roho, kwanza wana umoja kishenzi halafu kama nati zimelegea fujo ndio wanalolipenda, nenda nae kistaarabu na mpe muda ahame, akishindwa muondoe kwa sheria zinavyotaka, siku ukimuhamisha usiende peke yako nenda na serikali nzima itakuwa ngumu kukuattack,
Mkuu mbona unanilezea kama unanifahamu vile

Ni vile tu tunatumia ID fake.
 
Back
Top Bottom