Nakaribia kudhulumiwa, naombeni ushauri

Nakaribia kudhulumiwa, naombeni ushauri

Unajua umeandika kama sisi humu ndio majirani zake huyo afande, sikiliza mdogo wangu, wakati wowote unapopatwa na tatizo lolote jaribu kuwa mtulivu na kama unahitaji ushauri toa maelezo ya kutosha yanayohusiana na msaada unaohitaji, pia usikurupuke kutoa hukumu au kuchukuwa maamuzi kwa kutumia hasira au utashi wako binafsi, unaweza kuwa umeonewa, umedhulumiwa, au vyovyote itakavyokuwa, lakini dunia hii haki pekee haikufanyi uwe na sauti mbele ya mamlaka au sheria, hususan upande huo wa magwanda, kwao wao hakuna sheria za duniani wala za mbinguni zinazofanya kazi, kwahiyo kuwa makini huyo anaweza hata kukunyanganya hiyo nyumba akasema ni yake na mamlaka ikakuweka wewe ndani na kusema ulitaka kumdhulumu, kwa kifupi umeyatimba, nakushauri mvumilie na mpe siku au mwezi kama hajalipa mwambie mimi nyumba nauza, utamuwachia msala huyo atakaekuja kununua, kwa kifupi umeyatimba.
Ila wewe jamaa, umeandika nini hiki?
 
Yes.
Kweli Maisha magumu, kama umempangisha nyumba mzima anaweza kutengeneza documents akampiga hiyo nyumba
Huyo anachukulia poa lkn tumpe muda huyo jamaa hata kama ni kuruta sio maskini wakushindwa kulipa kodi, mshahara wa chini kwa mwanajeshi haupungui 1.2 take home, ndio ashindwe kulipa 50 au 70 kwenye hilo, na kama anaishi bila ya familia itakuwa pesa zote anamalizia kwenye pombe au wanawake, maana kwenye kambi nyingi za jeshi wameweka bar mshahara ukitoka tu inakuwa kama fungulia goli.
 
Wakuu habarini za wakati huu. Naandika uzi huu nikiwa na simanzi sana!

Nina eneo langu Ukonga KMKM ambapo nimejenga nyumba moja kubwa ya kupangisha na vyumba vingine 4 vyenye sebule na choo ndani. Nimefanya uwekezaji huu kwa kujinyima sana tena nikitumia pesa yangu halali.

Mimi siishi Dsm kwa sasa. Changamoto ipo kwa mpangaji mmoja bwana mdogo ambaye ni Mwanajeshi mwenye cheo cha Coplo, ni rika langu, yuko kati ya 30-37; ananisumbua sana kulipa kodi. Nimemvumilia vya kutosha. Pamoja na kuweka kodi ndogo lakini bado jamaa ananisumbua mno.

So far namdai zaidi ya milioni moja. Kuna wakati nasafiri kwenda Dar kutazama maendeleo ya makazi yangu na nakutanaga nae lakini anaishia kunipiga sound. Jamaa ni mtaratibu sana, anazungumza kwa upole; kila nikijaribu kumtoa hata kwa kumsamehe hiyo kodi huwa napatwa na huruma.

Kwa sasa enough is enough. Mara ya mwisho nimekutana nae Desemba mwaka jana, akakiri kwa maandishi kwamba namdai na atalipa deni lote Jan. 29 mwaka huu. Kilichotokea ni kwamba tarehe 29 imepita na kakaa kimya! Nikimpigia simu zangu hapokei. Kwasababu niko mbali, nimemtuma mpangaji wangu mmoja ninayemwamwini ili anipe nizungumze nae ila inasemekana jamaa hayupo pale kwa takribani wiki 3, kuna tetesi ameenda kwenye kozi Kibaha.

Ningeweza kwenda kumshtaki kambini kwake lakini sijui yuko kambi gani, kuna wanaosema yuko Lugalo ila hawana uhakika.

Naombeni msaada wakuu, naamini kuna watu ni Wanajeshi humu, wengine mna ndugu zenu Jeshini na hamuwezi kukubali dhuluma ya namna hii, naombeni msaada wa namna ya kuitambua kambi yake, majina yake nayajua, niko tayari kumsamehe hiyo kodi ila anipishe ili nitafute mpangaji mwingine.

Naomba kuwasilisha.

N:B: Wapangaji wote wana Mikataba. Kimsingi huyu jamaa ameshavunja terms za Mkataba muda mrefu. Naweza kumdai kodi Kimahakama lakini sitaki kupoteza muda.
Acha kuogopa vyeo.. Nenda Kambi yake ongea na Mkuu wa Kambi... Imeisha hiyo....
 
Mimi nimetoa ushauri wangu kwa mujibu wa huyo mtoa mada akili yake ilivyo, sikutoa ushauri kama ningekuwa mimi, kwa sababu ningelikuwa mimi asingewahi hata kujaribu kunifanyia hivyo, tungeheshimiana
 
Unajua umeandika kama sisi humu ndio majirani zake huyo afande, sikiliza mdogo wangu, wakati wowote unapopatwa na tatizo lolote jaribu kuwa mtulivu na kama unahitaji ushauri toa maelezo ya kutosha yanayohusiana na msaada unaohitaji, pia usikurupuke kutoa hukumu au kuchukuwa maamuzi kwa kutumia hasira au utashi wako binafsi, unaweza kuwa umeonewa, umedhulumiwa, au vyovyote itakavyokuwa, lakini dunia hii haki pekee haikufanyi uwe na sauti mbele ya mamlaka au sheria, hususan upande huo wa magwanda, kwao wao hakuna sheria za duniani wala za mbinguni zinazofanya kazi, kwahiyo kuwa makini huyo anaweza hata kukunyanganya hiyo nyumba akasema ni yake na mamlaka ikakuweka wewe ndani na kusema ulitaka kumdhulumu, kwa kifupi umeyatimba, nakushauri mvumilie na mpe siku au mwezi kama hajalipa mwambie mimi nyumba nauza, utamuwachia msala huyo atakaekuja kununua, kwa kifupi umeyatimba.
Are you normal?
 
Wakuu habarini za wakati huu. Naandika uzi huu nikiwa na simanzi sana!

Nina eneo langu Ukonga KMKM ambapo nimejenga nyumba moja kubwa ya kupangisha na vyumba vingine 4 vyenye sebule na choo ndani. Nimefanya uwekezaji huu kwa kujinyima sana tena nikitumia pesa yangu halali.

Mimi siishi Dsm kwa sasa. Changamoto ipo kwa mpangaji mmoja bwana mdogo ambaye ni Mwanajeshi mwenye cheo cha Coplo, ni rika langu, yuko kati ya 30-37; ananisumbua sana kulipa kodi. Nimemvumilia vya kutosha. Pamoja na kuweka kodi ndogo lakini bado jamaa ananisumbua mno.

So far namdai zaidi ya milioni moja. Kuna wakati nasafiri kwenda Dar kutazama maendeleo ya makazi yangu na nakutanaga nae lakini anaishia kunipiga sound. Jamaa ni mtaratibu sana, anazungumza kwa upole; kila nikijaribu kumtoa hata kwa kumsamehe hiyo kodi huwa napatwa na huruma.

Kwa sasa enough is enough. Mara ya mwisho nimekutana nae Desemba mwaka jana, akakiri kwa maandishi kwamba namdai na atalipa deni lote Jan. 29 mwaka huu. Kilichotokea ni kwamba tarehe 29 imepita na kakaa kimya! Nikimpigia simu zangu hapokei. Kwasababu niko mbali, nimemtuma mpangaji wangu mmoja ninayemwamwini ili anipe nizungumze nae ila inasemekana jamaa hayupo pale kwa takribani wiki 3, kuna tetesi ameenda kwenye kozi Kibaha.

Ningeweza kwenda kumshtaki kambini kwake lakini sijui yuko kambi gani, kuna wanaosema yuko Lugalo ila hawana uhakika.

Naombeni msaada wakuu, naamini kuna watu ni Wanajeshi humu, wengine mna ndugu zenu Jeshini na hamuwezi kukubali dhuluma ya namna hii, naombeni msaada wa namna ya kuitambua kambi yake, majina yake nayajua, niko tayari kumsamehe hiyo kodi ila anipishe ili nitafute mpangaji mwingine.

Naomba kuwasilisha.

N:B: Wapangaji wote wana Mikataba. Kimsingi huyu jamaa ameshavunja terms za Mkataba muda mrefu. Naweza kumdai kodi Kimahakama lakini sitaki kupoteza muda.
Jua jina lake kamili, then nenda makao makuu ya jeshi kamshtaki.
nawe utapangishaje mwanajeshi? pole sana
 
Unajua umeandika kama sisi humu ndio majirani zake huyo afande, sikiliza mdogo wangu, wakati wowote unapopatwa na tatizo lolote jaribu kuwa mtulivu na kama unahitaji ushauri toa maelezo ya kutosha yanayohusiana na msaada unaohitaji, pia usikurupuke kutoa hukumu au kuchukuwa maamuzi kwa kutumia hasira au utashi wako binafsi, unaweza kuwa umeonewa, umedhulumiwa, au vyovyote itakavyokuwa, lakini dunia hii haki pekee haikufanyi uwe na sauti mbele ya mamlaka au sheria, hususan upande huo wa magwanda, kwao wao hakuna sheria za duniani wala za mbinguni zinazofanya kazi, kwahiyo kuwa makini huyo anaweza hata kukunyanganya hiyo nyumba akasema ni yake na mamlaka ikakuweka wewe ndani na kusema ulitaka kumdhulumu, kwa kifupi umeyatimba, nakushauri mvumilie na mpe siku au mwezi kama hajalipa mwambie mimi nyumba nauza, utamuwachia msala huyo atakaekuja kununua, kwa kifupi umeyatimba.
Hakuna kitu kama hicho
 
Unajua umeandika kama sisi humu ndio majirani zake huyo afande, sikiliza mdogo wangu, wakati wowote unapopatwa na tatizo lolote jaribu kuwa mtulivu na kama unahitaji ushauri toa maelezo ya kutosha yanayohusiana na msaada unaohitaji, pia usikurupuke kutoa hukumu au kuchukuwa maamuzi kwa kutumia hasira au utashi wako binafsi, unaweza kuwa umeonewa, umedhulumiwa, au vyovyote itakavyokuwa, lakini dunia hii haki pekee haikufanyi uwe na sauti mbele ya mamlaka au sheria, hususan upande huo wa magwanda, kwao wao hakuna sheria za duniani wala za mbinguni zinazofanya kazi, kwahiyo kuwa makini huyo anaweza hata kukunyanganya hiyo nyumba akasema ni yake na mamlaka ikakuweka wewe ndani na kusema ulitaka kumdhulumu, kwa kifupi umeyatimba, nakushauri mvumilie na mpe siku au mwezi kama hajalipa mwambie mimi nyumba nauza, utamuwachia msala huyo atakaekuja kununua, kwa kifupi umeyatimba.
Khaa!kwa hiyo wapo juu ya sheria au ameyatimba kivipi?Acha kumtisha mwenzio
 
Katika kada wanazoishi maisha magumu ni wanajeshi.
Hapo ukitoa vitu bila yeye kuwepo una kesi utatengenezewa.
Hivi vikozi vifupi havizidi miezi 4, subiri arudi umtoe kwa kutumia mjumbe au mwanasheria mchezo umeisha. Atalala mitaroni huyo nguchiro
Too generalised mkuu., nahisi umeandika kwa hisi bila fact. Mambo kwa ground ni tofauti mkuu.

Kwa hiyo JWTZ wana hali ngumu kuliko kada zingine means PT, MT, ualimu nk?? Unafahamu hata bajet ya JWTZ kulinganisha ni hizo kada zingine?
 
Huyo anachukulia poa lkn tumpe muda huyo jamaa hata kama ni kuruta sio maskini wakushindwa kulipa kodi, mshahara wa chini kwa mwanajeshi haupungui 1.2 take home, ndio ashindwe kulipa 50 au 70 kwenye hilo, na kama anaishi bila ya familia itakuwa pesa zote anamalizia kwenye pombe au wanawake, maana kwenye kambi nyingi za jeshi wameweka bar mshahara ukitoka tu inakuwa kama fungulia goli.
Tusubiri marejesho
 
Migogoro ya ardhi likiwemo hilo la kodi hayapokelewi polisi kwa sababu hiyo sio jinai bali ni shauri la madai hivyo apeleke shauri lake baraza la ardhi na nyumba la wilaya.
Uko sahihi kwa sehemu mkuu.

Ingawa lazima shauri lianzie Baraza la Ardhi la Kata kwa ajili ya Usuluhishi. Wakishindwa Kata ndio liende Wilaya.

Thanks anyway, ingawa sitaki huu usumbufu, nataka tu aachie chumba changu.
 
Hawa watu wanaitwa askari si watu wa kufanya nao ukaribu hata kidogo, kama ni urafiki uwe wa kupeana tu salamu barabarani ila kuwaingiza kwenye maisha yako binafsi hasa ya kifedha utaishia kulia
Ni vile tu sina muda mkuu.

Ila ningeamua kuruka naye mbona hakuna rangi angeacha kuona.

Ni vile tu kila nikifikiria kumuharibia mtu kibarua chake roho inakuwa nzito.
 
Dalali aliyemleta most likely anajua.

Hao wapangaji jirani zake, most likely yawezekana alishawahi spit-out kambi yake.

Anzia hapo Lugalo, kama sio wa kambi hiyo, Mkuu wa Kambi atakusaidia kumlocate sababu una mjua majina yake.
Akishajua force number yake tu mchezo umeisha

Aende hapo lugalo au ngome watajua wapi Kambi yake ilipo.
 
Nenda hapo Upanga kama ulivyoshauriwa ukiwa na kopi ya nyaraka zote muhimu zitakazokusaidia ktk mdai yako, muhimu majina yake matatu,hao wanaokushauri umsubiri arudi vp kama anajiandaa kwenda zake nje ya nchi kwamwaka mzima.
Pia naomba kuuliza je haishi nafamilia ambayo ingekusaidia kujua kambi yake
Hana familia mkuu. Ni mtu wa pombe ila ana kadem kake kamoja ambako kanakujaga akiwepo.

Next stop ni Upanga mkuu.
 
Back
Top Bottom