Najiuliza kama Spika aliapa kuilinda na kuitetea Katiba, kwanini anaivunja?

Umeeleweka sana maana si mara ya kwanza unalisema hili la Karma.
 
Mkuu unawajua "wachumia tumbo" au unawasikia? Wenyewe kuapa viapo vya uongo au kumshirikisha Mungu kwenye uovu wao si sehemu ya maisha yao ya kawaida kwa maana hawana hofu ya Mungu wala hawaamini kama kuna kufa!!!
 
Mkuu "Mwanakawe.." mbona unaogopa kumtaja huyo "naniliu" kwani wale "wasionaniliu" wangaliko baada ya "naniliu" kunaniliu?
 
Mkuu "Mwanakawe.." mbona unaogopa kumtaja huyo "naniliu" kwani wale "wasionaniliu" wangaliko baada ya "naniliu" kunaniliu?
No, ni kwasababu, hata kabla naniliu, hajananiliu, kulizuka minong'ono mingi kuhusu hali ya afya ya naniliu, na kwamba alikuwa hoi bin taaban, katika kujaribu kuokoa maisha yake, akakimbizwa kule naniliu, ikashindikana, ndio akananiliu akiwa kule, ikaonekana itakuwa ni aibu dunia ikijulishwa naniliu ali naniliu kule kwa ugonjwa wa naniliu, sasa kwa vile taifa lilishatangaziwa rasmi, alinaniliu tarehe fulani kwa ugonjwa wa naniliu, ukitoa sababu nyingine yoyote, au tarehe rasmi ya kunaniliu, utakuwa umemfanya naniliu naye, aonekane muongo, hivyo bora kuendelea kuamini kile tuu tulichotangaziwa rasmi.
P
 
Hajui maana ya KIAPO...anafiiri kuapa ni justification tu kumbe ni kitu muhimu na kibaya saana kama hutayatii hayo uliyouyaapa kwani yaweza kuwa chanzo cha laana / roho za kukataliwa etc ... na mbaya zaidi laana hurisishwa hadi vilembwe (kizazi cha nne cha mpata laana).

Laana yaweza kuwa ni adhabu nyingi hata pamoja na kuwa na maisha mafupi hapa duniani.(kifo).

Kuna sheria nyingi za ulimwengu wa kiroho wanasiasa hawazijui ama wanadharau...ulimwengu huu unataliwawa kwa sheria...

Mwacheni aendelee kukiuka kiapo chake...ataona mwisho wake !!
 
Kabisa Mkuu saa zingine inabidi kunaniliu ili tuendelee kunaniliu pasipo kuleta misigano na kina naniliu... ila "karma" haitawaacha wanaovichezea viapo kwa maana imeandikwa "...na wala msiape! Msiape kwa uongo! Msiape viapo kwa upuuzi!! Ole wao waapao..." hadi hapo uzito wa kuapa uko wazi...
 
Usipende kutajataja watu na mahusiano yao ya faragha. Ni utoto.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…