habari za leo ndugu zangu...kuna bf wangu ambaye tulianza urafiki zaidi ya miaka kama 2 na nusu iliyopita, japo tulijuana kwani tulisoma primary pamoja lakini hatukua na uhusiano wowote ule. kwa miaka hiyo 2 na nusu tulikua na long distance relationship coz kila mmoja wetu alikua akisoma nje, tukakubaliana kuoana hapo baadae. jamaa karudi 2 months ago nikafurahi sana coz kama mjuavyo long distance rltn huwa inamitihani mingi. sasa hali imeanza kuwa tete baada ya kukuta message za mapenzi tena kutoka kwa wasichana tofauti zaidi ya wawili, kumuuliza baba kulikoni jibu ni kuwa 1. hawezi kutolea maelezo kila message nitakayoiona....2. yeye mwanamke akimtumia message zenye design ya mapenzi na yeye atarudisha hivohivo...!!......nabaki njia panda maana kama mjuavo mapenzi raha yake kuoneshana mahaba japo kwa kuitana tu honey, baby...nk., sms na simu kupigiana. niko njia panda kama kweli ana mapenzi nami au ndo mambo ya changa la macho.....:A S embarassed: