Nahitaji msaada wa mawazo na ushauri nini nifanye juu ya hii Tsh Milioni 8

Jumanne Mwita

JF-Expert Member
Nov 18, 2014
424
1,044
Habarini za majukumu? Pamoja na hayo natumaini wote ni wazima pia! Mimi sijambo na naendelea na majukumu yangu ya kila siku kwa ajili ya maisha yangu ya sasa na ya baadae.

Katika kitu kinachonichanganya nikaona naweza kupata wapi mawazo mazuri na ya kujenga zaidi ya #JamiiForum. Nikasema hapana ngoja nifikishe ujumbe na wazo hili nililonalo ili niweze kuchanganua nawezaje kulifanya hili na nisije kujutia baadae.

KWENU.

Nimepata kiasi cha Tsh million 8 taslimu, hizi hela nimejikuta napata mawazo ya hapa na pale, nianze na nini kati ya mambo makuu mawili ambayo ni.

1. Wazo la kwanza
Nimepanga nijenge nyumba ya vyumba 3 maana kiwanja ninacho kabla ya kupata hii pesa na kama ikibaki hata million 2 kwenye hiyo hela niangalie ntakachoiwekezea ili nisipate shida hapo baadae.

2. Wazo la pili
Hili ndio linaniumiza kichwa mpaka basi, kwanza nilitaka niifanyie biashara kwanza kabla haijaisha ili niikuze baadae ndio nijenge sasa maana kiwanja tayari ninacho.

Sasa najikuta nawaza nitaifanyia niashara gani wakati sina experience yeyote na biashara na sijui biashara gani ambayo nitawekeza hiyo hela ili nisije kujuta mbeleni huko.

Pia najikuta niko njia panda kati ya mawazo hayo mawili nimeshindwa nianze na lipi ambalo lingeniwezeshea hela hiyo ikatumika vyema na baadae nikaitwa mtu katika watu.

Nitangulize shukrani zangu kama mchango wako kwangu na mawazo yako ili niweze kulishinda hili
 
Umepataje? Kama ni kwa njia ya biashara nasisitiza irudishe huko huko kwenye hiyo biashara.

Kama zali (kubeti, kuokota, kurithi, umeiba..etc), jaribu biashara ila lazima iyo biashara uwe ushaianza uongeze tu mtaji.

Hiyo hela haitoshi nyumba labda uwe kiwanja unacho na upo mkoani.
 
Yaani ulivyoandika tu asilimia nyingi za kupoteza ni kubwa nyumba ujenge kwa 8m? Au uko vijijini mkuu?

Izungushie kwenye biashara...ss angalia ww passion yako ni nn? Unapenda nn kufanya sikiliza insticts zako ingia mara moja kufanya usighairi ghairi...usitumie hela yote anza hata na 2m.

Kuna wakala,wakala wa maji,wakala wa oil.mwe mbona mambo mob...jibidishe
 
Nilitaka kusema ilete nikuwekee mwanangu ila acha tu.

Nyumba ndio kitu muhimu kwa hiyo vyumba 2 vya masta sebule na chumba kidogo kama jiko ukisimamia mwenyewe 100%, waweza weka hadi bati la kibongo lakini baadae ukamalizia hizo finishing kidogo kidogo.

Biashara ni kama kamari waweza kula au kuliwa.

Yote kwa yote omba Mungu akusimamie.
 
Umepataje? Kama ni kwa njia ya biashara nasisitiza irudishe huko huko kwenye hiyo biashara.

Kama zali (kubeti, kuokota, kurithi, umeiba..etc), jaribu biashara ila lazima iyo biashara uwe ushaianza uongeze tu mtaji.

Hiyo hela haitoshi nyumba labda uwe kiwanja unacho na upo mkoani.
Kiwanja ninacho kabla ya kupata hii pesa
 
Ahsante, ndio maana nikaomba ushauri wenu ambao mna mawazo mengi na mnaona mbali. Pia sijengei mjini ni mbali na town vitu vipo simple sana vya ujenzi
Kujenga nyumba ya kuishi definetly ni woga tu... maana kama ni kijijin hata kikopea benk kipengele...kuna biashara kibao..kuna matofali kufyatua na kuuza..etc etc angalia na eneo ulipo
 
Back
Top Bottom