Prince Mhando
JF-Expert Member
- Mar 25, 2014
- 9,584
- 12,064
Mimi ni kijana ambae nipo kwenye umri wa kuuvuka ujana na kuuendea utu uzima. Miaka ya nyuma mara kadhaa nimeshawahi kuumizwa sana kwenye mahusiano. Ilifikia kipindi nikaamua kuyapa kisogo mahusiano. Mbinu haswa niliyokuwa naitumia ni ku hit and run.
Ila baadae miaka 6 nyuma nilikutana na msichana wa KIMACHAME nilimpenda akanipenda ila kwa bahati mbaya alikuwa na mpenzi wake tuseme walikuwa kwenye long-distance relationship, hope uzalendo ulimshinda huyu msichana tukajikuta tumeingia kwenye mahusiano, akamuacha mpenzi wake waliosoma wote chuo huko Mwanza.
Miaka mitatu baada ya mahusiano yetu nilibahatika kumpa mimba huyo msichana, kuna siku mimba ilivyokuwa na miezi 5 aliondoka nyumbani from no way... kuanzia saa 11 jioni akarudi saa 2 usiku nilikasirika sana lakini siku muuliza ukizingatia ilikuwa mimba yake ya kwanza.
Maisha yaliendelea tukawa na furaha sana akajifungua mtoto wa kiume. Kipindi chote hiki huyu msichana alikuwa na kazi ambayo kwa kiasi fulani ilikuwa inamuingizia kipato, sikuwahi kujua analipwa kiasi gani na wala sikuwahi kabisa kujua tarehe za mshahara huwa anapokea tarehe ngapi....kiukweli sikuwa na kazi na majukumu yote alikuwa anafanya mwenyewe...nilijitahidi kutafuta kazi {kipindi hicho} lakini jitihada zilikuwa zinagonga mwamba.
Ni mwaka sasa tokea nipate kazi ninayoifanya, kazi yangu hii inanifanya niwe narudi nyumbani asubuhi... hivyo kwa wiki nalala nyumbani mara moja tu...! Mwaka huu mwezi wa tano mwenzangu ni kama alipoteza kabisa hisia za mapenzi na mimi akawa hataki kabisa kushirikiana na mimi kwenye tendo {mnyanduano} nikawa nikimgusa tupo kitandani haonyeshi mshituko wowote wala haonyeshi ushirikiano unaweza ukampapasa masaa mawili mfululizo bila yeye kuonyesha mshituko wowote huku nikona dalili zote za yeye kuwa macho.
Niliivumilia hiyo hali kwa muda wa miezi miwili. Ni kama vile alikuwa ananitafutia sababu mara kwa mara alikuwa na tabia ya kuchunguza simu yangu haswa nikiwa nimelala.. sasa kipindi hiki ambacho alikuwa ananinyima tendo nilitafuta mchepuko nikawa namalizia hamu zangu huko. Baadae huyu msichana alifumania meseji za mchepuko, ikawa kesi nikamkumbusha kuwa umeyataka mwenyewe mimi sio hanisi tuwe tunalala kitandani kama mtu na dada yake.
Tuliyasuluhisha yakaisha tukanyanduana.... baadae akaanzisha tabia ya kumlaza mtoto katikati yetu... yaani nikitaka game hadi nimruke mtoto kisha ndipo nipige game na tokea mwezi wa nne hajawahi hata siku moja kuonyesha dalili kuwa ana hamu ya kunyanduana yani mpaka nimuanze. Kiukweli sijafunga nae ndoa ila kwa muda wote tulioishi sisi ni wanandoa tunao subiri mambo yakae sawa tuibariki ndoa yetu.
Nimeivumilia halii hii ndugu zangu najiona uzalendo unanishinda. Ajabu ni kuwa hana furaha na mimi ila kuna kijana mmoja akija huwa namuona anakuwa na furaha, atacheka hadi jino la ndani kabisa utaliona...
Mwenzangu hataki kunisikia kabisa. Kimaadili mimi ni muislam vile vile niliwahi mara nyingi kumuelekeza juu ya jinsi ninavyotaka awe lakini hakuwahi kabisa kufuata maadili ninayo yataka mimi.... Nimeamua kumuacha japo kwa shingo upande ninawaomba wana JamiiForums mnisaidie mawazo nipo njia panda ndugu yenu
Ila baadae miaka 6 nyuma nilikutana na msichana wa KIMACHAME nilimpenda akanipenda ila kwa bahati mbaya alikuwa na mpenzi wake tuseme walikuwa kwenye long-distance relationship, hope uzalendo ulimshinda huyu msichana tukajikuta tumeingia kwenye mahusiano, akamuacha mpenzi wake waliosoma wote chuo huko Mwanza.
Miaka mitatu baada ya mahusiano yetu nilibahatika kumpa mimba huyo msichana, kuna siku mimba ilivyokuwa na miezi 5 aliondoka nyumbani from no way... kuanzia saa 11 jioni akarudi saa 2 usiku nilikasirika sana lakini siku muuliza ukizingatia ilikuwa mimba yake ya kwanza.
Maisha yaliendelea tukawa na furaha sana akajifungua mtoto wa kiume. Kipindi chote hiki huyu msichana alikuwa na kazi ambayo kwa kiasi fulani ilikuwa inamuingizia kipato, sikuwahi kujua analipwa kiasi gani na wala sikuwahi kabisa kujua tarehe za mshahara huwa anapokea tarehe ngapi....kiukweli sikuwa na kazi na majukumu yote alikuwa anafanya mwenyewe...nilijitahidi kutafuta kazi {kipindi hicho} lakini jitihada zilikuwa zinagonga mwamba.
Ni mwaka sasa tokea nipate kazi ninayoifanya, kazi yangu hii inanifanya niwe narudi nyumbani asubuhi... hivyo kwa wiki nalala nyumbani mara moja tu...! Mwaka huu mwezi wa tano mwenzangu ni kama alipoteza kabisa hisia za mapenzi na mimi akawa hataki kabisa kushirikiana na mimi kwenye tendo {mnyanduano} nikawa nikimgusa tupo kitandani haonyeshi mshituko wowote wala haonyeshi ushirikiano unaweza ukampapasa masaa mawili mfululizo bila yeye kuonyesha mshituko wowote huku nikona dalili zote za yeye kuwa macho.
Niliivumilia hiyo hali kwa muda wa miezi miwili. Ni kama vile alikuwa ananitafutia sababu mara kwa mara alikuwa na tabia ya kuchunguza simu yangu haswa nikiwa nimelala.. sasa kipindi hiki ambacho alikuwa ananinyima tendo nilitafuta mchepuko nikawa namalizia hamu zangu huko. Baadae huyu msichana alifumania meseji za mchepuko, ikawa kesi nikamkumbusha kuwa umeyataka mwenyewe mimi sio hanisi tuwe tunalala kitandani kama mtu na dada yake.
Tuliyasuluhisha yakaisha tukanyanduana.... baadae akaanzisha tabia ya kumlaza mtoto katikati yetu... yaani nikitaka game hadi nimruke mtoto kisha ndipo nipige game na tokea mwezi wa nne hajawahi hata siku moja kuonyesha dalili kuwa ana hamu ya kunyanduana yani mpaka nimuanze. Kiukweli sijafunga nae ndoa ila kwa muda wote tulioishi sisi ni wanandoa tunao subiri mambo yakae sawa tuibariki ndoa yetu.
Nimeivumilia halii hii ndugu zangu najiona uzalendo unanishinda. Ajabu ni kuwa hana furaha na mimi ila kuna kijana mmoja akija huwa namuona anakuwa na furaha, atacheka hadi jino la ndani kabisa utaliona...
Mwenzangu hataki kunisikia kabisa. Kimaadili mimi ni muislam vile vile niliwahi mara nyingi kumuelekeza juu ya jinsi ninavyotaka awe lakini hakuwahi kabisa kufuata maadili ninayo yataka mimi.... Nimeamua kumuacha japo kwa shingo upande ninawaomba wana JamiiForums mnisaidie mawazo nipo njia panda ndugu yenu