King Kong III
Platinum Member
- Oct 15, 2010
- 62,891
- 95,189
Mkuu, kuna kitu kinaitwa standard. Ndiyo maana nchi zinazojielewa huweka minimum salary kulingana na level na aina ya kazi. Mfano, UAE ina viwango maalum vya mishahara kwa baadhi ya professions.Mkuu matumizi yake sio sawa na yako
Kuna mtu ukimtajia hela ambayo WEWE unaona unatoboa kwa mwezi anakushangaa na anaona haitoshi
Let's be humble kidogo
Si kwamba kila mtu ana matumizi sawa, bali kuna basic cost of living ambayo lazima izingatiwe.
Mimi naweza kutumia mafuta ya kawaida ya korie, mwingine atanunua alizeti premium oil. Mimi perfume ya 6,000, tajiri ya milioni. Mimi nitaenda kazini kwa usafiri wa umma, tajiri atatumia Range Rover Autobiography mwaka wa mbele au LC300 kaweka FULL TANK. Hiyo ni lifestyle.
Lakini kwenye basic needs, hesabu lazima izingatiwe.
Kwa askari mwenye familia, laki 5 ni ndogo. Mshahara unatakiwa kuzingatia chakula, maji, usafiri, kodi, afya, watoto na gharama nyingine za msingi, pamoja na kiasi cha dharura.