Nafsi imesahaulika. (a rant).

Nilitaka ufike hapa 😹😹

Kumbe hakuna Mungu ni fix tu?
Sasa mbona umemuelezea Mungu na utatu wake mtakatifu? 😹
 
Nilitaka ufike hapa 😹😹

Kumbe hakuna Mungu ni fix tu?
Sasa mbona umemuelezea Mungu na utatu wake mtakatifu? 😹
Hujaelewa shwetani mtoa roho wewe

Nimesema kuwa stori kuhusu uwepo wa Mungu nyingi ni fix, ila haimaanishi Mungu hayupo

It's just not Mtu anaye ishi mbinguni.

Ni both, body, mind and soul

Yaani totality ya kila kitu kuhusu wewe na uwepo wako na wakila mtu na kila mnyama na kila ndege na kila kitu
 
Sija kataa mbona Daah, alaf mm nilisha rudi kuwa de gunner😁
Hujakataa wapi? Ukikubali uwepo wa Mungu basi na bible umeikubali na Adamu na Hawa ni chimbuko la uwepo wako ingawa wao ni wazungu wewe ni msukuma..!! 😹😹

Ukiikataa Bible basi na Mungu umemkataa na imani na dini zake zilizoletwa na wazungu..!!

Haya sasa tuambie wewe upo upande upi?
 
Mungu ni imani, na wewe umekiri uwepo wake..!!

Sasa Mungu ni nani? Anaishi wapi?

Kwahiyo unataka kusema ndege ni Mungu?
Mazingira yanayotuzunguka ni Mungu?

Je, mavi yako nayo ni Mungu? 😹
 
Sijui nise meje?

Labda nitumie mfano wa mti na matawi yake...

Mungu ni mti na sisi ni matawi
Hujajibu swali, hivyo vitu tunavyovitumia alivitengeneza nani? Na ukisema aliumba dunia je, wakati anaiumba yeye alikaa wapi??
 
Hujajibu swali, hivyo vitu tunavyovitumia alivitengeneza nani? Na ukisema aliumba dunia je, wakati anaiumba yeye alikaa wapi??
Energy can neither be created nor destroyed

Physics form 3 hiyoo
Majibu yako wazi

Mchakato wa matter na unadilikaji wake ni natural, maji yana exist katika form 3(solid, liquid and gas) ila it's still water

Vivyo hivyo wewe, mimi, mimea na kila kitu ni kitu kimoja(energy), =Mungu
 
Kwa vyakula, tukipunguza au kuacha kuiga uzungu, na kuendeleza taratibu za kiafrika za ukulima, uuaji na tunavyopika vyakula vyetu, inaweza kutuepusha na madawa wanayoweka katika mbegu za vyakula, nyama n.k. tutaonekana tuko nyuma, pengine hatutengezi pesa, kwa kutoharakisha na kukuza uzalishaji, ila tutakuwa salama kiafya ya mwili na akili.
 
Neno Energy kidini ni spirit na sayansi inatambua kuwa kuna NAFSI NA SAYANSI INATAMBUA KUWA NAFSI NI ENERGY PIA sasa utasema vipi hii hoja ndiyo ifanye kuwe na Mungu? Tumia akili ....hoja ya kutambua kuwa yupo Mungu tunaipata kwetu sisi binadamu pia... Sasa tuunganisha hizi logic..
1) je sisi ni Energy? Jibu ni ndiyo.
2)je sisi ni nafsi ? Jibu ni ndiyo
3)je nafsi nayo ni Energy ? Jibu ni ndiyo.
4)je akili ni energy ? Jibu ni ndiyo
5)je binadamu kaumbika kwa akili kubwa sana yenye mpangilio wa hali ya juu sana ? Jibu ni ndiyo .
6)je binadamu kaumbika kwa nguvu za energy ? Jibu ni ndiyo .

SASA TUNAKWENDA KUUNGANISHA DOT ZA LOGIC ...kama tumekubali kisayansi kuwa nguvu za energy ndiyo ziumbazo au zifanyikazo vitu mbalimbali na tumekubali kisayansi kuwa vitu vimeumbika kwa mpangilio wa akili kubwa sana ..na tumekubali kisayansi kuwa nguvu energy inaweza kufanyika nafsi na kufanyika akili . Sasa unasemaje hakuna NGUVU KUU ZENYE UFAHAMU(NAFSI) NA AKILI ZILIZO UMBA HUU MFUMO WA MWANADAMU ..? Uwezi kusema kuwa binadamu kaumbika kwa bahati pasipo akili kubwa kumuumba kwa mpangilio.
 
Energy sio Mungu

Unachanganya Imani na science.
Science haimjui Mungu na haitambui uwepo wake…!!

Ukija kwenye imani za dini wao wana amini Mungu yupo na katulia zake mbinguni na ndiye aliyeumba kila kitu..!! Hawaamini science wala hivyo vitabu tulivyosoma mashuleni. Wao wanaamini vitabu vyao viwili Bible na Quran ambavyo vinamuelezea Mungu ndio creator wa yote mpaka binadamu..!!

Sasa jibu swali wewe unaamini kipi?
Acha kuwa vuguvugu hueleweki..
 
Hapo hatuta elewana

Wewe umeshikilia hadithi..

Mimi niko kwenye physical and metaphysical realization of God.. Ukifatiliia ancient teachings hata before ujio wa Christianity ndo utaelewa na maanisha nini.

Religion sio Christianity na Islam pekee... Hizi zimmekaa kimafumbo zaidi.

Umeshawahi kusoma kuhusu Buddhism and Hinduism? Hizi ni ancient religions kutoka Asia... Zinakkaribiana kushibana na science maana zinnaelezea kwa undani kuhusiana na higher powers zinavyolink na mwili wa binadamu.

Kuna energy body(chakra system)

Mungu si kitu au mtu ni kile ki nacho kufanya uwe, kila kiungo kina chembe chembe ya uuungu na energy portal kufikia Enlightenment..

Sasa kama hivi vitu huuvijui bado, tuishie hapa kwanza maana hatutaelewana
 
Wewe unaamini Mungu yupi? Tuanzie hapo kwanza.

Christianity wao wanaamini kwenye Mungu mmoja kupitia utatu mtakatifu, Mungu baba, Mungu mwana (Yesu kristo) na Mungu roho mtakatifu ambao wewe umeuelezea kwenye uzi wako.
Na wanaamini ndio aliyeumba kila kitu..!!

Islam wao wanaamini Mungu mmoja Allah
Muumba wa kila kitu. Hana mshirika, hana mtoto, wala si sehemu ya Utatu. Yesu (Isa) ni nabii, si Mungu kwao…!!

Hinduism wao huabudu miungu kama Vishnu, Shiva na Devi, huku mapokeo mengine yakiona miungu hiyo kama maonyesho.. ni kama vile nyie wasukuma mnavyoabudu mizimu ya kwenu..

Mnavyowaamini machifu waliokufa kwamba mkiomba mvua na kutoa sadaka na kupiga ngoma na kucheza mvua zitanyesha..!!

Hao science yao ya kificho wapo kundi moja na wachawi 😹

Wasukuma si huwa mnatumia fisi kama usafiri? 😹 lakini hauonekani kwa macho ya nyama..!!

Buddha wao waamini uwepo wa viumbe wa kiungu, lakini si Mungu muumba mwenye mamlaka ya mwisho..

Hao ndio wanaofungua jicho la tatu na mbanga za chakra zote zipo humo..!!

Mimi naona uzi wako haueleweki na wewe hujui unachokitaka wala kukisimamia..!! Maybe umewasilisha vitu vingi kwa wakati mmoja ndiomana unapingana na kila member..!!
 
Nilicho kuleta hapa ni universality ya hizi dhana zote

Utatu mtakatifu unawiana sana na human aspect.. (mind, body and spirit)

Lakini pia hatuwezi kusema kuna Mungu wa aina flani na flani huko nibkujidanganya

All religions point out to the same GOD

Utakuwa ni ujinga mtu kudhani Mungu wa wakristo ni mmoja na wa waislamu ni mwingine.

What I did kwenye huu uzi ni kutafuta common ground

That's the thing. Hata wanascience wanafanya, Albert Einstein na wakina Newton walisoma sana ancient texts ndo maana wakaja na uvumbuzi wa kisayansi.

Tusikalie kudhani dogma za makanisani ndo ukweli mtupu wakati haziko practical.


Kama unataka kujua zaidi kuna video nikutumie link inaitwa Samadhi.. A portal to awakening.. Hii hailengi dini moja bali unatafuta common ground..
 
Mimi naona uzi wako haueleweki na wewe hujui unachokitaka wala kukisimamia..!! Maybe umewasilisha vitu vingi kwa wakati mmoja ndiomana unapingana na kila member..!!
Issue ni kuwa tunataka tubaki kwenye zone moja ya uelewa, hapo ndo tunapojifunga..

Alaf acha bwana wasukuma sisi tunavihoja vya kuchekecha sana.. Sasa sijui ni kweli huwa ni fisi wanaendesha ama? 😂
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…