Ertugrul Bey
JF-Expert Member
- Aug 6, 2020
- 13,186
- 26,305
Habar za siku ya nane nane,na kwa wanasimba wenzangu leo ndio Ile sikukuu yetu ya kipekee kabisa,tuwe proud kuwa wanasimba daima NGUVU MOJA.
Mara nyingi sana hapa jf utasikia kauli kama Watu wenyewe tunatumia fake id msichukulie mambo serious au kauli kama Watu wenyewe tunatumia utambulisho bandia tusipangiane maisha
Ni sahihi kabisa humu hatujaja kupangiana maisha wala kuwa serious muda wote, lakini huwa nashangazwa na mtu ambaye anafanya upuuzi au ujinga kwa kisingizio kwamba eti tunatumia fake id
Listen very well ndugu zangu, ikiwa unazungumzia fake id na maisha halisi ya watu wanao kujua huko mtaani upo sahihi kwamba kweli hakuna wanao kujua humu ndani ya jamii forums hivyo unaweza sema chochote na hutukufanyi kitu
Lakini ukiwa unazungumzia fake ID ukiwa ndani ya jf halafu unajificha ndani ya id yako eti unaweza sema chochote na lolote na hakuna kitu tutakufanya,just think twice homies,unajidanganya
Hapa ndani ya jamii forums kupitia id yako tunakuchukulia ni mtu kamili na nafsi kamili na tunakujaji kwa matendo yako, kwasababu ndio jina tunalo kufahamu nalo na ndio utu wako,sasa utapimwa kwa tabia yako na matendo yako,na ndio maana hata moderators watakuadabisha kwa I'd yako la sivyo wangesema hawa ngoja tuwaache kwakuwa watu wenyewe wanatumia utambulisho bandia.
Ukitaka kuona ukweli juu ya hili,ebu ona pale ambapo I'd yenye kuheshimika ikiandika ujinga, hapo utaona watu wanashangaa na kuisakama Wewe nawe pamoja na ukongwe wako unaandika upuuzi?
Hii maana yake nini? Inamaana kupitia michango yako,machapisho yako na mienendo yako Umejenga your own identity ambayo tunakujua nayo hapa jf
Kwahiyo kupitia I'd yako fake tuta kuheshimu au tutakudharau,kupitia I'd yako tutasoma chapisho lako kwa umakini na adabu au tutalisoma juu juu na kutolipa umuhimu, kupitia I'd yako tutachukua ushauri wako au tutaumwaga chini na kuukanyaga kanyaga
Kwahiyo utambulisho wako kupitia I'd yako ndio wewe mwenyewe kwenye maisha halisi ya jf, kwahiyo acha kujificha kupitia I'd yako na kufanya upuuzi na ujinga eti kwa kisingizio kwamba hatukujui,tunakujua kupitia I'd yako
Kuwa humble,ishi huku vizur,heshimu kila mtu na mind your own business,kama kutofautiana tutatofautiana kibinadamu lakini usiamue kuwakwaza watu makusudi kisa eti hatukufahamu, tunakufahamu kupitia I'd yako
Ni hayo tu!