Nafikiria kuachana na mke wangu

Nafikiria kuachana na mke wangu

Hatukushauri umuache... fata ushauri wa wadau
Kuna rafiki angu kaolewa 2015 mpk leo hajazaa na hawajaachana. Vumilia mkuu huwezi jua kwanini hamzai kwa wakati huu.
Kuna mmama huku kazaa mtoto mmoja tena kwa kumtafuta sana kwa madawa kabla hajafa alijutia matendo ya huyo mtoto yalimfanya ajute kumzaa
 
Habari za muda humu ndani,nawaza kuachana na wife niliyekaa nae kwenye mahusiano miaka 5 kwa maana miaka mitatu tumeishi pamoja.
Sababu iliyofanya kufikiria maamuzi haya ni kukosa mtoto mpaka leo,sasa nafikiria kuanza maisha mapya tu.Naombeni ushauri wenu juu hili.
Umejaribu kujua chanzo tatizo? Hatua gani umechukua?
 
Habari za muda humu ndani,nawaza kuachana na wife niliyekaa nae kwenye mahusiano miaka 5 kwa maana miaka mitatu tumeishi pamoja.
Sababu iliyofanya kufikiria maamuzi haya ni kukosa mtoto mpaka leo,sasa nafikiria kuanza maisha mapya tu.Naombeni ushauri wenu juu hili.
Labda wewe mbegu zako hazioti?? nendeni kwa bingwa mpimwe fertility wote waili
 
Endelea kuwa na subira, ila kama unajihisi humtaki tena na huwezi kuishi nae tena basi mueleze hali yako ya kihisia kwa mapenzi na huruma, baada ya hapo achana nae kwa wema na usimdhulumu katika kile kinachotakiwa kuwa haki yake.
 
Kama tatizo ni mtoto tu, ila kwa vingine yuko vizuri si sahihi kumuacha.
Unachoweza kufanya ni kuzaa tu nje idadi ya watoto unaotaka,muhimu tu kwenye ndoa yako kuwepo utulivu.

Jiulize, ukiwa kipofu na ukawa ombaomba, atakuvumilia?
Nb: Tusikimbilie kuoa kwa kutamanishwa na muonekano wa nje.​
 
Mmeshajua shida ni nini? Piteni kwa wataalam mnaweza kupata solution,pia kuna Dr yupo pale Kairuki alimsaidia jamaa yangu,mkewe amejifungua last week.Pia nina Kaka yangu wa hiyari amezunguka mpaka India hakufanikiwa lakini amepata watoto watatu ndani ya miaka mitano ila wote wanazaliwa na miezi saba maana ikivuka hapo kiumbe kinakufa,kuna Dr yupo na clinic yake pale Buyuni njia ya kwenda Chanika,kama utahitaji mawasiliano yao nitakupa, ni rahisi kuchukua kwa hawa jamaa zangu.

Binafsi nakushauri usimwache kwasababu hiyo utampa shemeji psychological torture ya hali ya juu sana.Fanya jitihada ili mjue shida ni nini, kama hakuna solutions then mtafanya mutual agreement 🙏
Ni yupi alikuwa na shida kati ya me au ke,??? Maana ulivyo andika ni mix by yas
 
P2 zimerejesha hali ya ugumba wa enzi za bibi zetu miaka ya 1960 hadi 1990.
Pima kwanza ukiona wewe uko sawa nikupe namba anywe dawa usukumani huko
 
Pole najua unajisikia vibaya ila niuulize haya maswali halafu nikupe kisa kimoja.

1.Je ,anakupenda?
2.Anakutendea mazuri?
3.Anakuheshimu?
4.Je umeshirikiana nae katika hilo?
5.Una uhakika tatizo lenu halitokani na wewe au ukoo wenu?

Mkuu watoto ni muhimu kwenye ndoa ila pia wanaweza wakawa sio muhimu,,pindi ukiugua mtu muhimu wa kwanza ni mke wako,hata watoto wakikua watakuacha kwenda kutafuta maisha yao ila mkeo inawezekana akabaki mpaka unakufa.

Njia nyingi zipo za kutafuta hiyo furaha,kumuacha tu kisa hiko ni ukatili mkubwa sana kama ni mwema kwako kwa muda wote.

Mfano
Pale hospital kesi nyingi za namna yako zinakuja lakini ajabu majibu yanatoka mwanaume ndo shida.
 
Kuna mwamna ndoa yake ilikua na changamoto kama ya mleta uzi.
Na yeye akaamua maamuzi kama hayohayo, mwisho wa siku bibie akaolewa mlango wa pili tu kutoka kwake, walikua kwenye nyumba ya kupanga.

Baada ya miezi kadhaa tu bibie akaanza kutema mate, kitu imooo.

Angalia tatizo nini mkulungwa, asijeenda huko akadungwa mimba, ukabaki na masononeko.
 
Habari za muda humu ndani,nawaza kuachana na wife niliyekaa nae kwenye mahusiano miaka 5 kwa maana miaka mitatu tumeishi pamoja.
Sababu iliyofanya kufikiria maamuzi haya ni kukosa mtoto mpaka leo,sasa nafikiria kuanza maisha mapya tu.Naombeni ushauri wenu juu hili.
Itakufedhehesha hii. Mara anatoka tu afu anapata mimba. Utaonekana wewe ni boya. Nakushauri Fuatilia hospital wote mpime mjue shida ni nini. Yawezekana ikawa shida kwako. Nakushauri usifanye hivyo. Utafedheheka hata huko utakako enda kama shida ni wewe itakuumiza na utapata msongo wa mawazo. Nakushauri tulia hata Ukiweza ukafanye IVF siku hizi maisha yamekuwa mazuri sana
 
Back
Top Bottom