Damidizzo
JF-Expert Member
- Apr 28, 2014
- 399
- 170
Hiduma kwa wateja umewapata kwa namba ipi mkuu maana me nawatafuta siku ya nne leo siwapati!SENSA 2022.
Nimefanikiwa kujaza form ya maombi ya kazi ya muda kwa ajiri ya kazi ya sensa 2022,lakini nimekosea kuandika majina ya mdhamini mmoja yaani jina la kwanza nimeliweka mwisho na jina la mwisho limekuwa la kwanza.
nimejaribu ku log in kwenye account ili nifanye editing ya majina lakini inaleta nifanye editing ya sehemu inizoja ambazo ziko sahihi ilhali sehemu niliyokosea haileti.
FORM niliyoijaza ya maombi ya kazi ya sensa 2022 ina sehemu tatu yaani sehemu A ni kujaza taarifa zangu binafsi, sehemu ya B ni kijaza taarifa za wadhamini wawili na sehemu C ni kujaza taarifa au viambatanishi vya vyeti.
Sasa nikienda sehemu ya KUHUISHA taarifa kwa ajiri ya kufanya marekebisho ya majina mdhamini, zinatokea sehemu mbili tu yaani sehemu A na sehemu C ambazo zimejazwa kwa ufasaha Ila sehemu B haionekani kwa aijri ya KUHUISHA taarifa ya Wadhamini ambazo nimekosea, nahitaji kufanya marekebisho.
USHAURI WANGU, nikipakuwa form hiyo harafu nikaifanyia marekebisho form kwa kufuta na correction pen na kuandika majina kwa ufasaha kwa mkono harafu nika pakia form mtandaoni, je nitakuwa nimekosea? maana nimewapigia simu huduma kwa wateja wao nao wananambia labda kuna shida ya mtandao kwenye mfumo wao na hawajui wanisaidiaje na muda wa kutuma maombi unakaribia kuisha.