Nafasi za kazi nchi za nje

Nafasi za kazi nchi za nje

Kwa UK nitafikaje wadau wa Birmingham nipeni udambwidambwi
 
Hivi kupiga boksi kunamaanisha kufanya kazi za kubeba boksi kweli au maana yake imebadilika na kuwa kazi yoyote tu ile afanyayo Mtanzania aliyeko ughaibuni?

Tafuta mada yangu ya faida za wabeba boksi kwenye uchumi wa Tanzania nilieleza vizuri sana kuhusu wabeba boksi search iko umu
 
Kwa mara nyingine tena nachua fursa hii kuwasilisha mada katika jukwaa hili lenye watu wenye mitizamo tofauti ya kimaisha hiyo basi nitapokea maoni yenu. Hitaji langu nikupata mtu anayeweza kunisaidia kupata kazi zisizo hitaji kiwango kikubwa cha elimu (low skilled labour) maarufu kama kupiga box nje ya tanzania kwenye nchi za uarabuni ulaya magharibi marekani na ocenia(Australia na New Zealand) kwa mwenye uzoefu tasaidiane mawazo nawasilisha ahsanteni.
 
Money Stunna MKUU nime search ila sijaona huo uzi ..naamini nitajifunza kitu
 
Last edited by a moderator:
Maisha ya ulaya yana raha yake na kalaha yake. Kuna watu wanaenda Ulaya wanafanya hizo kazi wanapata hela wanarudi Bongo, maisha yanakuwa magumu, wanatamani kurudi Ulaya wanashindwa kwani walishanyea kambi kwa kuzidisha muda wao wa viza. Mifano hiko mingi.
 
Maisha ya ulaya yana raha yake na kalaha yake. Kuna watu wanaenda Ulaya wanafanya hizo kazi wanapata hela wanarudi Bongo, maisha yanakuwa magumu, wanatamani kurudi Ulaya wanashindwa kwani walishanyea kambi kwa kuzidisha muda wao wa viza. Mifano hiko mingi.

Ingekuwa vizuri tufanye kama wazee wetu walivyokuwa manamba kwenye mashamba ya mkonge, walikuwa wanaenda kufanya kazi kwa miaka miwili hadi mitatu kisha wanarudi nyumbani kufanya kitu na kuangalia familia zao, kisha wanaenda tena. Kwa mwengo huo tungefanya mengi mazuri bongo kwa kiwango chetu kuliko kuzamia huko majuu.
 
Kwa mara nyingine tena nachua fursa hii kuwasilisha mada katika jukwaa hili lenye watu wenye mitizamo tofauti ya kimaisha hiyo basi nitapokea maoni yenu. Hitaji langu nikupata mtu anayeweza kunisaidia kupata kazi zisizo hitaji kiwango kikubwa cha elimu (low skilled labour) maarufu kama kupiga box nje ya tanzania kwenye nchi za uarabuni ulaya magharibi marekani na ocenia(Australia na New Zealand) kwa mwenye uzoefu tasaidiane mawazo nawasilisha ahsanteni.


Muone Kuveta atakusaidia
 
Last edited by a moderator:
Kwa kuanzia huwezi kupewa viza na nchi za magharibi kwa ajili ya kwenda kupiga box, unachokifanya ama wengi walioko huko Ulaya na Marekani walivyofanya ni kutafuta chuo kwenye nchi hizo, kuomba viza na ukifika huko sasa akili kichwani mwako kusoma ama kupiga box nk. Ila kwa njia hii inahitaji pesa ndefu ambayo kama unayo ni bora kujiendeleza bongo kuliko kwenda huko ambako still inabid uendelee kutafuta vibali vya kuishi na kufanya kazi ni process ndefu. Kwa nchi za kiarabu sifahamu vzr ila huko inabid uwe makini unaweza kujikuta uko utumwani ukaikumbuka bongo kuwa makini sana !!
 
Vip kuhusu australia na new zealand
 
Box mbona zipo kibao tu hata hapa Tz hadi vijijini. Zinatupwa tu majalalani karibia na maduka au mahospitalini zinazoishia dawa, unaenda unazipigapiga weee ukichoka unarudi kulala.

uwezo wako wa kufikiri ni mbovu kama jina lako
 
Habarini za wakti huu wana JF wenzangu bila kupoteza muda namleta kwenu kijana mwenye umri wa miaka 21 ambaye alimaliza kidato cha nne mwak 2011 na kupata daraja la tatu na alama 25 hata hivyo haku bahatika kupata bafasi ya kuendelea na shule za serikali na kutokana na uwezo wa familia yake hawakuweza kumlipia shule za private hivyo akaamua kuingia mtaani kuanza kupambana na maisha. Ni miaka mitatu sasa amefanya kazi mbali mbali za viwandani na hata madukani lakini kwa mujibu wake bado mambo hayajaenda sawa ndipo mwishoni mwa mwa mwaka jana alipo pata habari kuhusu kazi mbali mbali zisizohitaji kiwango kikubwa cha elimu katka nchi za uarabuni ulaya na marekani. Kutokana na hali yake ya maisha akaona kuwa anaweza kuzifanya hizo kazi lakini tatizo ni jinsi ya yeye kuweza kufika huko kwa maana ya visa na mahala pa kufikia hivyo akaniomba ushauri.nami kwa kua si mjuzi saana wa mambo ya safari za nje ya nchi nikaona nimsaidie kufikisha hoja yake hapa kwenye jukwaa ili kwa wale wenye kuweza kumshauri kumsaidia kwa vitu kama invitational letter ili apate visa kwa urahisi muweze kumsaidia kwani ansema yupo tayari kwenda huko kupambana maana anaamini maisha popote. Kwa maelezo haya basi nikaribishe michango yenu hususani kwa wale mliop huko ughaibuni.....
 
yuko tayari kufanya kazi haramu...magazeti ya udaku hutoa namba za kupiga ili ukapigwe kazi uarabuni...ni kama sishauri hv, ulaya ataenda tu apige kazi kwa bidii hapa hapa atapata chanel
 
Habari wana JF hivi majuzi nili weka uzi kuhusu kijana wa miaka 21 ambaye anatafuta nafasi ya kwenda nje ya nchi kutafuta kazi za kiwango cha chini (low skilled) na anatafuta mtu wa kumsaidia katika hili lakini naona uzi ule umefutwa. Lakini bado tena leo naendelea kumleta kwenu ili mwenye kuweza kumsaidia amsaidie
 
Habari wana JF
KWA MARA NYINGINE TENA naweka bango langu la kuelezea nia yangu ya kuelekea ughaibuni.
Hivi majuzi niliweka bango huku kuelezea nia yangu hii lakini nashangaa sikuliona tena yaani limefutwa sasa najiuliza kwani tatizo liko wapi mimi kueleza nia yangu hii.
Kwa kifupi nilimaliza kidato cha nne mwaka 2010 then nikajiunga na colege moja ya clinical asistance na kumaliza mwaka 2013 nikapangiwa kituo huko mkoani iringa kwa kweli katika ufanyaji kazi wangu sijaona faida yoyote kwani mshahara wenyewe ni mdigo kiasi kwamba ukichanganya na makato ya kodi mifuko ya jamii na bima unakua huja save chochote hivyo basi nikaona bora nitafute njia ya kuingia ughaibuni hata kama nitafanya kazi za hadhi ya chini lakini nikaweza kusave angalu kiwango kidogo

Hivyo basi kwa wale wenye uzoefu na huko hebu nipeni mbinu za kuweza kufika huko...
 
Habari wana JF
KWA MARA NYINGINE TENA naweka bango langu la kuelezea nia yangu ya kuelekea ughaibuni.
Hivi majuzi niliweka bango huku kuelezea nia yangu hii lakini nashangaa sikuliona tena yaani limefutwa sasa najiuliza kwani tatizo liko wapi mimi kueleza nia yangu hii.
Kwa kifupi nilimaliza kidato cha nne mwaka 2010 then nikajiunga na colege moja ya clinical asistance na kumaliza mwaka 2013 nikapangiwa kituo huko mkoani iringa kwa kweli katika ufanyaji kazi wangu sijaona faida yoyote kwani mshahara wenyewe ni mdigo kiasi kwamba ukichanganya na makato ya kodi mifuko ya jamii na bima unakua huja save chochote hivyo basi nikaona bora nitafute njia ya kuingia ughaibuni hata kama nitafanya kazi za hadhi ya chini lakini nikaweza kusave angalu kiwango kidogo

Hivyo basi kwa wale wenye uzoefu na huko hebu nipeni mbinu za kuweza kufika huko...

wadau mbona kimya ss
 
Back
Top Bottom