MALCOM LUMUMBA
JF-Expert Member
- Jul 26, 2012
- 20,897
- 63,784
Huyu mwanadada Libianca ni mwanamuziki wa Cameroon, na mwaka huu ametoa wimbo uitwao PEOPLE. Binafsi nimeusikiliza mara kadhaa na kutambua kwamba huyu dada ana kipaji kikubwa mno cha uandishi na uimbaji. Mashairi ya huu wimbo yana ujumbe mzito sana na ametumia mahadhi ya Afro-Fusion (Huku akichanganya Blues, Soul, RnB na Highlife) kama ambavyo Burna Boy anafanya.
Mziki una mahadhi mengi lakini bado unausikia Uafrika kwa kiwango kikubwa na kufahamu kabisa huyu ni mwanamuziki kutoka Afrika Magharibi. Kiukweli amejitahidi mno.
Yanaweza yakawa ni maoni yangu binafsi na nimeandika kwasababu ya mahaba na huu wimbo, lakini kama wewe ni mdau wa muziki naomba umsikilize. Kila siku huwa nasema wasanii wetu wanahitaji kujifunza na kubadilika sana kama wanataka kulifikia soko la kimataifa.
Mziki una mahadhi mengi lakini bado unausikia Uafrika kwa kiwango kikubwa na kufahamu kabisa huyu ni mwanamuziki kutoka Afrika Magharibi. Kiukweli amejitahidi mno.
Yanaweza yakawa ni maoni yangu binafsi na nimeandika kwasababu ya mahaba na huu wimbo, lakini kama wewe ni mdau wa muziki naomba umsikilize. Kila siku huwa nasema wasanii wetu wanahitaji kujifunza na kubadilika sana kama wanataka kulifikia soko la kimataifa.