Tanzania ni nchi masikini sana, tangu tupate Uhuru hatujawahi kuwa na nafuu, hata Rais Magufuli ameikuta hivyohivyo ikiwa na hali mbaya. Sio siri, wote tunafahamu kuwa wakoloni hawakuondoka kipumbavu wakati wanaliachia bara la Africa ikiwemo Tanzania yetu. Tunafahamu kuwa wakoloni wanatumia njia mbali kuendelea kupata malighafi, masoko ya bidhaa zao, na nguvukazi. Tunafahamu kuwa wakoloni wanatumia mafariki zao ambao sisi tunawaamini sana kama vile viongozi maarufu, watu maarufu, mashirika ya hisani, mashirika na taasisi za kidini, viongozi wa vyama vya siasa, wanaharakati, WB, IMF, WTO na majasusi kufanikisha adhima zao hizo.
Rais Magufuli ameamua kujilipua na kutumia uncommon sense kutatua common problems zinalolikumba bara lote la Africa hasa kusini mwa jangwa la Sahara. Maana huwezi kutumia common sense kutatua common problems yaliyowashinda Marais wenzako waliokutangulia. Hata wazungu walitumia uncommon sense kufika pale walipofika, uncommon sense yao Ndiyo iliyowatuma watutawale, watufanye watumwa, watufanyishe kazi nyingi bila ujira, kuua Marais wetu waliopinga kunyonywa nk.
Tundu Lissu hakupaswa kupinga kila kitu cha Rais Magufuli kwakuwa vitu ambavyofanya kamavile kuondoa wafanyakazi na wanafunzi hewa, kukamata wakwepa kodi, wauza madawa ya kulevya, kuwaondoa viongozi wasiowajibaka, kujenga miundombinu ya kisasa kama barabara, madaraja na reli, elimu bure , kufufua shirika la ndege na reli, nk. hivi vyote vinaonekana hadharani Kwa watanzania na wasiokuwa watanzania.
Tundu Lissu anapaswa ku acknowledge mazuri na ku condemn mabaya, hapo kila mtu angemuelewa. Rais wetu kuna vitu anavifanya kinyume kabisa na matarajio ya wakoloni tusipomsaidia sio Tu atapandwa na hasira lakini tunaweza kuhatarisha uhai wake Kwa ajili yetu sote.
Hata wademocratics wana vitu wanamkosoa Trump lakini kuna vitu hawezi kumkosoa navyo kwakuwa ni kwamanufaa ya Yao wote