tpaul
Platinum Member
- Feb 3, 2008
- 27,195
- 27,806
Sitaki kuwachosha, hebu twende kwenye mada moja kwa moja. Nabii na mtume mkuu wa kanisa la WRC amewaambia wafuasi wake na jamii kwamba kufunga ndoa kanisani ni upagani.
Mtume huyo, ambaye ni maarufu kwenye kauli tata, amesema hayo wakati akiwahubiria waumini wake huko Matembele, Kata ya Kivule, na mahubiri hayo yamesambaa nchi nzima hadi kwa raia wa kawaida. Wengi wa wananchi niliowashirikisha hii video, wamesema mtume yupo sahihi kwa mujibu wa maandiko matakatifu. Siongezi neno. Hebu msikilize wewe mwenyewe hapo chini mkuu:
MAONI YANGU
Ijapokuwa sikubaliani na huyu nabii katika mambo mengi, kwa hili la ndoa, namuunga mkono 💯%. Kama kufunga ndoa kanisani ndiyo deal, basi hata Mungu angewafungisha Adam na Hawa ndoa ya kanisani. Vinginevyo, ufungishaji ndoa unaosisitizwa na viongozi wa dini na kuvalishana mipete mbele ya mchungaji au askofu, ni ubatili na uopagani mtupu. Hawa viongozi wanalazimisha kufungisha ndoa kwa ajili ya maslahi yao binafsi.
Nawasilisha.
Mtume huyo, ambaye ni maarufu kwenye kauli tata, amesema hayo wakati akiwahubiria waumini wake huko Matembele, Kata ya Kivule, na mahubiri hayo yamesambaa nchi nzima hadi kwa raia wa kawaida. Wengi wa wananchi niliowashirikisha hii video, wamesema mtume yupo sahihi kwa mujibu wa maandiko matakatifu. Siongezi neno. Hebu msikilize wewe mwenyewe hapo chini mkuu:
MAONI YANGU
Ijapokuwa sikubaliani na huyu nabii katika mambo mengi, kwa hili la ndoa, namuunga mkono 💯%. Kama kufunga ndoa kanisani ndiyo deal, basi hata Mungu angewafungisha Adam na Hawa ndoa ya kanisani. Vinginevyo, ufungishaji ndoa unaosisitizwa na viongozi wa dini na kuvalishana mipete mbele ya mchungaji au askofu, ni ubatili na uopagani mtupu. Hawa viongozi wanalazimisha kufungisha ndoa kwa ajili ya maslahi yao binafsi.
Nawasilisha.