Heinrich Himmler
Member
- May 20, 2013
- 71
- 151
Huyu nabii juzi kafanya kitu ambacho kimenishtua sana kwenye kipindi chake, katokea mtu anadai ni kipofu kaja na mama yake mzazi, yule mama kaulizwa kadai huyo mtoto wake kazaliwa hana macho kabisa, kabla hajamuombea kamera zilikuwa zinamuonyesha yule kijana akiwa amefumba macho, na ukimwangalia yule kijana alikuwa kama anainama chini muda mwingi.
kuinamisha kichwa chini ni hulka ya binadamu inayoambatana na kuona aibu. Basi nabii akasema huyu mtu tokea kuzaliwa hajawahi kuwa na macho, sasa mungu akimrudishia hata jicho moja si itakuwa safi, basi akachukua maji ya chupa na kummwagia huku akiweka mikono yake kwenye yale macho, eti yule jamaa akafungua jicho moja linaona.
Cha ajabu eti yule kipofu ambaye hajawahi kuona tokea kuzaliwa akapata jicho moja na ye akawa katulia tu kama hamna kilichotokea, yaani fresh tu. Mtu ambaye hajawahi kuona tokea amezaliwa hawezi kuwa vile akiona.
Halafu huu usanii anaofanya nabii anashirikisha hadi wamama watu wazima kuongea uongo mbele ya kadamnasi. Toka lini mungu akamponya mtu nusu kwa kumrudishia jicho moja? Ningekuwepo siku hiyo haki ya mungu ningeomba urudie kuomba ili jicho la pili nalo lirudi.
USHAURI: Katika miujiza ambayo haina longolongo ni upofu, namshauri huyo nabii asiigize tena kuponya mtu kipofu maana kuna siku itamtokea puani. kuna watu kama sisi tukiwa eneo la tukio tutataka tuhakikishe kama huyo kipofu kweli ni kipofu kabla hujamuombea halafu tutakuumbua.
Yeye aendelee na miujiza iliyozoeleka ambayo hatuwezi kuthibitisha kama sijui nilikuwa naumwa ukimwi, tumbo, nilikuwa sizai,mapepo, kichwa kuuma, kutokwa na damu, BP n.k ila asicheze kabisa na kumponya kipofu ambaye hana macho, huo muujiza hata yesu ukimwambia arudie te na hawezi.
kuinamisha kichwa chini ni hulka ya binadamu inayoambatana na kuona aibu. Basi nabii akasema huyu mtu tokea kuzaliwa hajawahi kuwa na macho, sasa mungu akimrudishia hata jicho moja si itakuwa safi, basi akachukua maji ya chupa na kummwagia huku akiweka mikono yake kwenye yale macho, eti yule jamaa akafungua jicho moja linaona.
Cha ajabu eti yule kipofu ambaye hajawahi kuona tokea kuzaliwa akapata jicho moja na ye akawa katulia tu kama hamna kilichotokea, yaani fresh tu. Mtu ambaye hajawahi kuona tokea amezaliwa hawezi kuwa vile akiona.
Halafu huu usanii anaofanya nabii anashirikisha hadi wamama watu wazima kuongea uongo mbele ya kadamnasi. Toka lini mungu akamponya mtu nusu kwa kumrudishia jicho moja? Ningekuwepo siku hiyo haki ya mungu ningeomba urudie kuomba ili jicho la pili nalo lirudi.
USHAURI: Katika miujiza ambayo haina longolongo ni upofu, namshauri huyo nabii asiigize tena kuponya mtu kipofu maana kuna siku itamtokea puani. kuna watu kama sisi tukiwa eneo la tukio tutataka tuhakikishe kama huyo kipofu kweli ni kipofu kabla hujamuombea halafu tutakuumbua.
Yeye aendelee na miujiza iliyozoeleka ambayo hatuwezi kuthibitisha kama sijui nilikuwa naumwa ukimwi, tumbo, nilikuwa sizai,mapepo, kichwa kuuma, kutokwa na damu, BP n.k ila asicheze kabisa na kumponya kipofu ambaye hana macho, huo muujiza hata yesu ukimwambia arudie te na hawezi.