Nabii Musa hajawahi kumtaja Shetani mahali popote katika maandishi yake; Uasi ni uamuzi wa MTU na sio Shetani

Robert Heriel Mtibeli

JF-Expert Member
Mar 24, 2018
21,340
51,891
NABII MUSA HAJAWAHI KUMTAJA SHETANI MAHALI POPOTE KATIKA MAANDISHI YAKE; UASI NI UAMUZI WA MTU NA SIO SHETANI.

Anaandika, Robert Heriel
Kuhani

Mhusika Shetani amekuwa zaidi maarufu katika vitabu vya Injili kuliko vitabu vya Torati, Zaburi na vitabu vya manabii wadogo kama kina Daniel, Yona, Habakuki n.k.

Vitabu vya Musa ambavyo ni Mwanzo, Kutoka, mambo ya Walawi, Hesabu na kumbukumbu la Torati havijamtaja Mhusika Shetani Kwa namna Yoyote Ile.

Ni kitabu cha mwanzo pekeake ambacho kinamtaja Mhusika Nyoka pale Edeni akimdanganya Eva. Wakristo wanadai nyoka ndiye Shetani Jambo ambalo sio Kweli. Sio kweli kwa hoja zifuatazo;

1. Maandishi ya Musa Kwa 99.9% hayakuandikwa kifasihi na kifalsafa, yaliandikwa Kwa Lugha ya moja Kwa moja.
Musa ni mwandishi wa Historia pamoja na Mwanasheria (aliyeandika sheria/Torati) kikawaida Historia haiandikwi kimafumbo na wala sheria haiandikwi kimafumbo.

Hivyo wanaosema neno Nyoka lilitumika kama Lugha ya picha kubeba taswira ya Ibilisi wanakosa mantiki.
Ndio haohao wanaosema pia tunda ni Lugha ya picha Jambo ambalo sio kweli. Tunda lilikuwa tunda Kutokana na nature ya maandishi ya Nabii MUSA.

Hii ni tofauti na Nabii Yesu au ISSA bin Mariam ambaye uhusika wake ulikuwa ni mwalimu na mara kadhaa alitumia mbinu ya Brainstorming Kwa kutoa metaphor (visa vya kifasihi vyenye mafumbo). Lugha atakayoitumia mtu wa kifasihi na Falsafa inaweza Isiwe Lugha ya moja Kwa moja na ikawa na matawi mengi ya tafsiri kulingana na Msikilizaji au msomaji.

2. Nyoka anayetajwa na adhabu alizopewa hazina uhusiano wowote na mhusika Shetani anayetajwa katika vitabu vya Injili.

Yule alikuwa Nyoka Halisi kama hawa tunaowaona hivi Leo. Kwa sababu ni kweli Nyoka anajongea Kwa tumbo mpaka hivi SASA.

Ushahidi WA wanyama kuongea upo mpaka hivi leo kwani hata Kasuku anaongea licha ya kuwa Hana Ala Sauti nzuri zinazomwezesha kuzungumza kama binadamu. Ila akiongea anaeleweka.

Wanyama wengine waliowahi kuongea ni pamoja na Farasi aliyepandwa na Balaki.

Hivyo kusema shetani(kama mhusika) alimuingia Farasi au Nyoka pale Edeni na kuzungumza hakuna mantiki yoyote Kwa sababu Mungu ndiye anaamua Kiumbe hiki kiongee na hiki kisiongee. Ukizingatia wapo binadamu wasioweza kuongea (Mabubu).

Maandishi ya Musa hayamtambui Shetani kama chanzo cha Uasi au dhambi hapa Duniani. Isipokuwa yanatambua Uhuru WA kuchagua wa viumbe wenyewe.

Yaani binadamu anayohiyari ya kuchagua kutenda Mema na Mabaya pasipo kusingizia Wahusika wa Kiroho wasioonekana. Yaani suala la Uasi NI ishu ya Uhuru binafsi WA MTU.

NABII MUSA ambaye ndiye Nabii namba moja Duniani aliyejenga msingi WA dini zenye asili ya Uyahudi(Ibrahim) ambaye ndiye Nabii pekee maandishi yake yanaeleza asili ya Mwanadamu na jinsi alivyoamua Kutumia Uhuru wake kuchagua kuasi, hatambui kitu kinachoitwa SHETANI kama Mhusika.

Bali anatambua uchaguzi hasi na nguvu hasi iliyomo ndani ya mtu.

Musa hakumtaja Shetani kama Mhusika Bali binadamu Kwa sababu;
1. Mwanadamu ndiye aliyewekewa sheria na ushahidi WA sheria hizo tunazo mpaka hivi leo.

Kusema shetani aliasi Mbinguni na hatujui sheria za Mbinguni hata Moja ni dalili ya kuongea vitu Kwa Uongo.
Huwezi sema Shetani aliasi Mbinguni alafu muda huohuo ukiulizwa utaje sheria hata mbili za Mbinguni huna unachojua.

2. Matokeo ya Uasi na adhabu za Uasi zinampata Mwanadamu mtendaji Kwa mujibu wa sheria na sio Shetani kama Mhusika.

Matokeo ya uzinzi, ubakaji, uuaji, wizi, n.k. Anayewajibika nayo ni Mwanadamu kama Mhusika aliyewekewa sheria.

Vitabu vya Musa MTU anapokosea au kufanya dhambi hajawahi kusingiziwa Shetani Bali mhusika akiyetenda na anayewajibishwa na mhusika.

Hii inafanana na Dini zote Duniani za Asili zikiwemo dini za kiafrika ambapo hakuna Mhusika Shetani, isipokuwa MTU akiamua kuwa Mbaya ndio huchukuliwa kama Mbaya na mwenye nguvu Hasi.

Hata kwenye Mahakama za kiulimwengu hawatambui Mhusika Shetani wala Mungu katika ishu ya Uasi au kufanya Makosa Bali wanajua MTU ndiye anamaamuzi ya kufanya Makosa au kutokufanya.

Kuwa Mwema ni maamuzi na kuwa Mbaya ni maamuzi pia ya MTU.

Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa sasa Dar es salaam
 
Basi ukiona hivyo usiende tena Kanisani kwake cos ni free,hulazimishwi na mtu.......haya mambo ya Dini ukiona sehemu hupaelewi endelea na mishe zako.........utaonekana unatumika kumchafua Kwa maslahi watu fulani......Chagua kile roho yako inapenda
 
Wahubiri wenye utata wamekuwa wengi, wengine kumtaja Yesu ni shughuli pevu. Zumaridi mwenyewe tu kumtaja Yesu kama mwokozi hatambui hilo.

Kuna wengine wanataja jina la Yesu kimagumashi kuzugia washirika wao. Mwingine utasikia akitamka mungu asifiwe badala ya Yesu asifiwe kama ilivyo kawaida. Waimbaji uchwara wa injili nao wameibuka wengi kumtaja Yesu kwenye nyimbo zao ni shughuli pevu
 
Tunaona hapo mwanzo wakati wa Mussa shetani alikuwa bado haaasi,alikuwa ni malaika mwema. Hbari za uasi wake tunakuja kuzisoma katika kitabu cha Ezekieli hapo ndio tunaanza kuona habari za huyo malaika aliye asi. hivyo ilikuwa sahihi kwa Mussa kutomtaja.

Kuhusu habari ya nyoka na eva, kama alikuwa nyoka kweli na tunda lilikuwa Tunda kweli kwanini walijikuta uchi? kwanini moja ya adhabu yake eva ilikuwa ni kuzaa kwa uchungu? naomba ufafanuzi kula tunda na kujikuta uchi,kuzaa kwa uchungu.
 
Basi ukiona hivyo usiende tena Kanisani kwake cos ni free,hulazimishwi na mtu.......haya mambo ya Dini ukiona sehemu hupaelewi endelea na mishe zako.........utaonekana unatumika kumchafua Kwa maslahi watu fulani......Chagua kile roho yako inapenda

Soma uelewe. Usikurupuke.
Hapa anayezungumziwa ni Musa wa kwenye Biblia
 
Mkuu unatafdiri Biblia kwa uekewa wako ambao ni finyu.

Nyoka wa zamani, Ibilisi na Shetani wote kitu kimoja.

Kumbuka kuwa upeo wa binadamu kutafsiri Neno unategemea sana si kufunuliwa tu, bali na elimu ya kitheologia uliyo nayo.
 
Neno shetani limetajwa kama mara 52 kwenye biblia nzima , nara 15 agano la kale na mara 37 agano jipya , na limeanzia kutajwa kwenye kitabu cha mambo ya nyakati , sio lazima iwe neno shetani chochote kilicho tofauti na maagizo ya Mungu ndo shetani mwenyewe , neno uovu limetumika mara nyingi kama mbadala
 
Mkuu unatafdiri Biblia kwa uekewa wako ambao ni finyu.
Nyoka wa zamani, Ibilisi na Shetani wote kitu kimoja.
Kumbuka kuwa upeo wa binadamu kutafsiri Neno unategemea sana si kufunuliwa tu, bali na elimu ya kitheologia uliyo nayo.

Rejea nilichoandika, nimesema hakuna sehemu yoyote ambayo Nabii Musa alitumia falsafa au Fasihi kuelezea maandishi yake.

Yeye ni mwanahistoria aliyeandika Historia ya Mwanadamu na pia ni Mwanasheria aliyeandika Torati.
Historia na Sheria sio masomo ya Fasihi na Falsafa. Yanaelezewa waziwazi tuu.

Sema waliofuata baadaye ambao ni wanafasihi na wanafalsafa ndio walitafsiri maandiko ya Musa Kifasihi na kifalsafa.

Na unapomzungumzia Fasihi na Falsafa kila MTU anaweza kutafsiri vile aonavyo kulingana na logic yake. Lakini Historia na sheria hazitegemei hayo mambo.

Ndio nitakupa mfano, ikiwa Nyoka alikuwa Ibilisi, vipi tunda lililoliwa lilikuwa tunda gani?
 
Neno shetani limetajwa kama mara 52 kwenye biblia nzima , nara 15 agano la kale na mara 37 agano jipya , na limeanzia kutajwa kwenye kitabu cha mambo ya nyakati , sio lazima iwe neno shetani chochote kilicho tofauti na maagizo ya Mungu ndo shetani mwenyewe , neno uovu limetumika mara nyingi kama mbadala

Upo sahihi Kabisa.
Kwa unavyoelewa Shetani ni Tabia hasi auvni kiumbe kama tulivyo Mimi na wewe?
 
Ni kwel mtibeli sema watakupinga mno ,watu wengi wanaishi na hadithi za Sunday school mpka Leo, amin nakuambia kundi kubwa wanazani wanamjua Yesu kwa sura kila wanapo vuta fikra za uwepo wake , wanavuta za yule mkal Brian dikon.
 
Mkuu kitabu cha mwanzo hizo sehemu ni lugha za picha tu ndio imetawala.

Nyoka ni lugha ya picha iliotumika kumuelezea shetani. Labda cha kujiuliza ni kwanini muandishi wa icho kitabu atumie mnyama nyoka na asitumie mnyama mwingine au biumbe wengine.

Nafikiri hilo ndio lingekuwa suala la msingi zaidi la kujiuliza na sio kwamba nyoka anetajwa hapo kwenye icho kitabu cha mwanzo mwansishi alitaka kumaanisha ni nyoka kama nyoka mnyama tu

Kumbuka hata Yesu mwenyewe alishatumia lugha ya picha ya nyoka. Kwahiyo cha msingi kujua hapo ni jinsi gani nyoka mnyama alijulikana kwa wayahudi wakati huo mpaka atumike kama lugha ya picha kumuelezea shetani.
 
Shetani ni mfumo ulio duniani, Mungu ni mfumo ulio juu mbinguni.. sasa Mussa alikusudia kuelezea mfumo wa juu mbinguni hakutaka kumwandika shetani
 
Unazijua mision 3 za Moze hapa duniani kibiblia?
1. Kuwaongoza waisrael kutoka utumwani kuelekea nchi ya ahadi.
2. Kuwaonesha waisrael kwa vitendo kwamba BWANA ni mkuu sana.
2. Kuwatafsiria sheria au amri za Mungu waisrael ili waenende katika misingi ya sheria hizo.

Hapo sheitwan hakuwa na nafasi amonv mision ya Musa. Kila nabii au mtume kwenye biblia alikuja na mision yake.

Soma biblia vzr usikurupuke
 
Back
Top Bottom