Na Mvua Hizi Ntawakamata Wengi....!!!

Na Mvua Hizi Ntawakamata Wengi....!!!

Nimerudi home mida hii, naona eti dada wa kazi kakamata hao insects kibao..ameingia jikoni, akakarangiza, ataka kula...watoto wangu wametamani. Nikampiga marufuku...nikamwambia "kula mwenyewe". Hivi ni chakula ama takataka hao wadudu?

mi hujanilisha hao wadudu, senene wenyewe sili, sembuse hao...
 
daaa hapa dar sijui wanapatikana wapi jamani maana daaaa hawa KUMBIKUMBI ni watam sana unawakaanga kidogo then na chumvi pilipili unawa unga mbona lazima mshikane mashati
 
kwetu songea kwa kingoni wanaitwa mbulika.

tena ukienda pale mshangano,msamala,bombambili,makambi,mateka,matogoro,mahiro,mfaranyaki,ruvuma,lizaboni,matarawe,ruhuwiko acha wanatoka kwenye VICHUGUU wenyewe mnaviita VIDULI ni balaa.
 
daaa hapa dar sijui wanapatikana wapi jamani maana daaaa hawa KUMBIKUMBI ni watam sana unawakaanga kidogo then na chumvi pilipili unawa unga mbona lazima mshikane mashati
mkuu mvua ikinyesha wanapatikana popte tuu!
 
Mimi nimesha wala sana hawa wakati nipo mtoto mdogo miaka 40 iliyopita. Wewe kama huwakuli basi hujafaidika kabisa.

mkuu MziziMkavu hao sio senene aisee hao ni kumbikumbi senene wenyewe wanakuwa kama panzi vile wanakuwa wakubwa sana na wanarangi ya kijani na wengine kaki. hao ni kumbikumbi na ukiwatoa hayo mabawa ni kama mchwa vile
 
Mimi nimesha wala sana hawa wakati nipo mtoto mdogo miaka 40 iliyopita. Wewe kama huwakuli basi hujafaidika kabisa.
Miaka 40 ilopita bado unakumbuka ladha yake...Naona wanasifiwa sana itabidi na mm nionje...Lkn ukitafuna ule utumbo/ mweupe wanaokuwa nao insects inakuwaje unauhisi mdomoni 😕
 
Back
Top Bottom