Mzee wa Upako alimtabiria Raila ODINGA angeshinda uchaguzi

Mzee wa Upako alimtabiria Raila ODINGA angeshinda uchaguzi

Hapa aliotea vibaya
ila angeshinda kweli angeongeza wateja kwa asilimia 50% +1
 
Mimi toka nlopomwona anajisifu na yale magari ya hela za waumini nilimdharau yy na waumini wake.they are all undergoes idiotism

ni rahisi ngamia kupenya kwenye tundu la sindano kuliko tajiri kuuona ufalme wa mbingu. Mjini shule wajinga ndio waliwao, kuna wengne wanatumia hammer
 
Jibu ni rahisi atasema waliiba kura na waumini kama kawaida wataunga mkono. "INUKENI ENYI MAZOMBI"
 
Namkubali sana mzee wa upako sema hapa aliteleza kidogo. It happens yeye sio mungu.
Hana lolote mganga wa kienye
ji huyo. Tatizo alisoma upepo kwenye kura za maoni asijue kua upepo huwa unageuka. Wajanja sana hawa watu.
 
Alikwishasema hata kazi ya uchungaji ni usanii, tusubiri atawaambia nini waumini wake, ndoto ilikuwa wongo? Na kama ndivyo kwahiyo alioteshwa na mapepo? Hapa ndio inapothibitisha kuwa sio kila wanalosema latoka kwa Mungu wengine ni kwa tamaa zao.



atawaambia Mungu ameghaili.
 
Hawa jamaa huwa wanasikitisha sana huwa nikiwatazama naona wazi wanauzalilisha ukristo.

Yani sawa tu na mpiga ramli
 
Alikwishasema hata kazi ya uchungaji ni usanii, tusubiri atawaambia nini waumini wake, ndoto ilikuwa wongo? Na kama ndivyo kwahiyo alioteshwa na mapepo? Hapa ndio inapothibitisha kuwa sio kila wanalosema latoka kwa Mungu wengine ni kwa tamaa zao.

.
2mambo ya nyakati 18-22.
''Mikaya akasema, sikieni basi neno la BWANA; Nalimwona BWANA ameketi katika kiti chake cha enzi na jeshi lote la mbinguni wamesimama mkono wake wa kuume na wa kushoto. BWANA akasema ni nani atakaemdanganya Ahabu mfalme wa Israel ili akwee Ramoth-gileadi akaanguke? Basi huyu akasema hivi; na huyu hivi. Akatoka pepo akasimama mbele za BWANA, akasema, mimi nitamdanganya. BWANA akamwambia, jinsi gani? Akasema, nitaondoka na kuwa pepo wa uongo vinywani mwa manabii wake wote. Akasema utadanganya, na kudiriki pia; ondoka ukafanye hivyo. Basi sasa angalia, BWANA ametia pepo wa uongo vinywani mwa manabii wako hawa, nae BWANA amenena mabaya juu yako''.
My take; ni nini kilipelekea wale manabii kuingiwa na pepo la uongo na kutabiri uongo wakifikiri ndio kweli? Jibu ni kwamba walikuwa ni manabii(system) iliyokuwa ikilipwa posho lake kutoka kwa hao watawala, kitu ambacho kilipelekea washindwe kuona neno la nabii Eliya alilokuwa amenena dhidi ya mtawala Ahabu.
Vivyo hivyo na huu mtandao(system) wa viongozi wa kidini wa leo. Posho lao lipo kwa watawala kiasi cha wao kushindwa kuona kweli ya Mungu kuwahusu.
.
 
Mchungaji Anton Lusekelo au kwa jina maarufu la Mzee wa upako tarehe 31 januari 2013 ,ndani ya kanisa lake alisema Raila Odinga ndiye angeshinda uchaguzi wa Kenya na Uhuru Kenyatta asingeshinda labda asubiri miaka ijayo na si kwenye uchaguzi huu.

Aliongea maneno haya kwa msisitizo na kurudiarudia sana na kwa mujibu wake utabiri huo alikuwa ameoteshwa na mungu wake.
Hawa wahubiri huwa wanacheza mchezo wa kubahatisha tu. Wakibahatisha wafuasi wao wanazidi kuwaamini na biashara yao inanoga zaidi.
 
Atapata aibu ya mwaka analeta mambo ya akina Sheikh Yahya afanye kazi ya (U T P) Utapeli tu mana hana lolote zaidi ya uzushi tu mara kuchinja mara mtabiri. Ila sishangai maana ilishatabiriwa kuwa watatokea manabii wa uongo na Lusekelo akiwamo
 
Ganga Ongo ni jitu fulani linalojivika uganga au ujuzi wa kuponya/kutabiri kama hivi kwa uongo.

Linaweza hata kukupa sumu likakwambia dawa.

Mkuu, mi nilishakuelewa mapema.
Semea mie nilidhani ume'use lafdhi ya kidosi, kwani mwenye asili ya Asia yeyote asingemudu kutamka "mganga muongo!"
angetamka "ganga ongo".
 
Tupo kwenye ulimwengu wa YUDA Esikaliyoti, Mzee wa Mipasho kamsaliti muumba wake kwa muusisha na mambo yake binafsi.
 
Utabiri na Unabii ni vitu viwili tofauti! Utabiri unaongozwa na ufahamu, hekima na maarifa ya kibinadamu. Unabii, mtu anaonyeshwa na Mungu juu ya mambo yatakayotokea. Kama mzee wa upako alitabiri basi yuko sahihi. Ingekuwa alitoa unabii basi tumshike uongo. Naomba mtoa uzi atoe clarification, mzee wa Upako alisema anatabiri au ananena jambo aliloambiwa na Mungu?
 
Hivi wafuasi wake wanajisikiaje baada ya utabiri huo kutotimia

Atawaambia kuna pepo liliingilia uchaguzi baada ya waumini kupunguza maombi..Huyu bwana kazidi dini yeye, siasa yeye, utabiri yeye..!! I wish angejkita kuhubiri neno ya Kaisari akaachana nayo..!
 
Mfanyabiashara tu huyo!

Tena sio Mfanyabiashara wa Kawaida, bali ni "TAPELI"tu huyu kama Matapeli wengine!

Huyu tumeshamzoea alijidanganya na zile Takwimu zilizokua zikitolwa na MATAPELI NA MAONGO MAKUBWA "SYNOVET"pamoja na wenzao kwamba RAILA ODINGA,angeshinda kwa kuwa alikua akiongoza kwenye Kura zao za Maoni!!

Walisahau kwamba kwamba Wapiga kura ni WAKENYA,na sio SYNOVET na washirika wenzake!!
Ukweli Huyu anaejiita MZEE WA UPAKO hamna kitu ni Tapeli tu anaetumia "kivuli"cha Kanisa Kuibia watu.....!Asubirie tena Uchaguzi ujao ajaribu kupiga "RAMLI"..!

Kuna Yule mwenzake sijui anaitwa nani vile...!Sijui Nabii FLORA, alitabiri kwamba SIOY SUMMARI [Mgpmbea wa CCM] angeshinda dhidi ya JOSHUA NASSARI,[Mbunge kwa sasa] ktk Uchaguzi mdogo Jimbo la Arumeru Mashariki,uliofanyika mwanzoni mwa mwaka jana kutokana na Kufariki kwa aliekuwa Mbunge, Summary!!

Lakini utabiri wa Nabii huyo Feki uligonga Mwamba,kwani JOSHUA Nassari alishinda kwa Kishindo!!

LUSEKELO anataka kutuambia huyu MUNGU wake wa Uongo alishindwaje Kumuonyesha kwamba RAILA hatashinda??
Na sasa tutamwaminije kama Mungu wake sio sawa na yule Mungu wa Majirani zetu(Wa..i.....s....lamu) ambaye hutetewa kwa kuuwa Watu wasio na Hatia huku yeye (Mungu"MFU"akishindwa Kujitetea)!!
Yeye Asubirie tu siku ya Hukumu akatowe Hesabu zake!
MUNGU IBARIKI TANZANIA!!!!
MUNGU IBARIKI CHADEMA!!!!
 
Utabiri na Unabii ni vitu viwili tofauti! Utabiri unaongozwa na ufahamu, hekima na maarifa ya kibinadamu. Utabiri, mtu anaonyeshwa na Mungu juu ya mambo yatakayotokea. Kama mzee wa upako alitabiri basi yuko sahihi. Ingekuwa alitoa unabii basi tumshike uongo. Naomba mtoa uzi atoe clarification, mzee wa Upako alisema anatabiri au ananena jambo aliloambiwa na Mungu?

.
Tofautisha kwanza kile ulichoita tofauti kati ya unabii na utabiri. Mbona hujafanya hivyo katika hii post yako? Hebu rudia kuisoma kwa makini.
.
 
Back
Top Bottom