Mwendawazimu huyo hana upako wa kweli wa Mungu,amebaki kuwa mtabili na mshauri mkuu wa CCM,na kupiga vita viongozi wenzake wa kiroho hasa wanapoonekana kuikosoa serikali wazi wazi.huyu ndiye aliyetoa ushauri kwa ccm,kutumia au kutotumia police kwenye mikutano ya cdm,na ndio matunda ya akina nape na mwigulu kuporomosha matusi kila wanaposimamama jukwaani kuilaani cdm,hata kama wananchi wanadai maji na shule safi wao wanatukana cdm tu.Mchungaji Anton Lusekelo au kwa jina maarufu la Mzee wa upako tarehe 31 januari 2013 ,ndani ya kanisa lake alisema Raila Odinga ndiye angeshinda uchaguzi wa Kenya na Uhuru Kenyatta asingeshinda labda asubiri miaka ijayo na si kwenye uchaguzi huu.
Aliongea maneno haya kwa msisitizo na kurudiarudia sana na kwa mujibu wake utabiri huo alikuwa ameoteshwa na mungu wake.