Mzee Kawawa afariki dunia!

Mzee Kawawa afariki dunia!

Rais Jakaya Kikwete, katika sauti ya huzuni kubwa, ametangaza siku saba za maombolezo kwa bendere kupepea nusu mlingoti.
 
Alilazwa jana katika Hospitali ya Taifa Muhimbili katika wodi wa wagonjwa mautihuti (ICU)

JK ameondoka muda si mrefu nadhani ndiyo anaenda kulitangazia taifa kuhusu huu msiba mzito wa Marehemu Mzee wetu Kawawa.

Mazishi nadhani bado mipango maana ndugu na jamaa bado wapo hapo hospitalini. wakiongozwa na mama JK

RIP Kawawa
..Mipango ya mazishi inafanyika nyumbani kwake madale na mwili umehamishiwa hospitali ya lugalo!!
 
Poleni sana Watanzania wenzangu. Kama taifa napendekeza tuwe na KAWAWA DAY kuanzia mwaka ujao wa 2010. Tarehe 31/12 ya kila mwaka ni siku muafaka zaidi.

Nini kifanyike kitaifa kila siku hiyo, ni suala la kujadiliana na kupanga kama taifa. Naamini Serikali yetu italiafiki na kulifanyia kazi wazo hili ili kuhakikisha historia yake haipotei katika taifa letu na Afrika kwa ujumla.

MUNGU awe nawe katika maisha yako mapya
Mzee wetu na shujaa wa kipekee katika taifa letu.
 
RIP simba wa vita nakutakia maisha mema poponi tafadhali usiwasimulie Nyrere na Moringe uliyo yaacha huku duniani(Tanzania) kama ufisadi kwani watahuzunika sana mungu akulaze pema ppeponi
 
Mungu amlaze pema peponi. Tutakukumbuka daima mzee wetu.
 
Safi sana....ila naomba kuuliza swali inakuwaje mtu anakufa then ndani ya dakika 35 tayari wimbo uko redio tayari na unachezwa?
 
Tulikupenda sana lakini Mungu alikupenda zaidi, lala salama ndugu yetu Simba wa vita.
 
Jamani, give me a break. We already have too many holidays. Katika siku ya Kawawa tutafanya nini? Tutamkumbuka nini? Siku ya Nyerere watu wanafanyaga nini? Ya Karume je? Hata watoto wetu hatuwaambii tunakumbuka nini siku hizo, basi watu kazi yao ni kulewa na kulala tu. Jamani, itakuwa aibu tukifanya jambo hili. Mimi nadhani tungekuwa na siku moja tu ya waasisi wa taifa, tukawakumbuka wote kwa pamoja, tuache kuongeza siku za uvivu, tuchape kazi.
 
AM NOT.
tutakua tunaadhimisha siku kama hizi ngapi kwa viongozi wa serikali???, which means itakua public holiday?, waTZ tuache uvivu, mtu kama kaondoka akumbukwe ndani ya nafsi, TUCHAPE KAZI JAMANI.
 
Naona JK ndo anatoa habari mjinsi ilivokuwa. Live TBC1
 
Poleni sana Watanzania wenzangu. Kama taifa napendekeza tuwe na KAWAWA DAY kuanzia mwaka ujao wa 2010. Tarehe 31/12 ya kila mwaka ni siku muafaka zaidi.

Nini kifanyike kitaifa kila siku hiyo, ni suala la kujadiliana na kupanga kama taifa. Naamini Serikali yetu italiafiki na kulifanyia kazi wazo hili ili kuhakikisha historia yake haipotei katika taifa letu na Afrika kwa ujumla.

MUNGU awe nawe katika maisha yako mapya
Mzee wetu na shujaa wa kipekee katika taifa letu.


Mkulu,

umenena vyema,litakua jambo la busara sana ili kuhakikisha vizazi vijavyo haviwasahau mashujaa wetu kama ilivyokua kwakina Abdul Sykes,Sheikh Takadir na Mzee Mshumi (alipewa mtaa lkn watu kwa kutojua umuhimu wake kwenye historia ya inchi hii wakaufuta jina lake)
 
Poleni sana Watanzania wenzangu. Kama taifa napendekeza tuwe na KAWAWA DAY kuanzia mwaka ujao wa 2010. Tarehe 31/12 ya kila mwaka ni siku muafaka zaidi.

Nini kifanyike kitaifa kila siku hiyo, ni suala la kujadiliana na kupanga kama taifa. Naamini Serikali yetu italiafiki na kulifanyia kazi wazo hili ili kuhakikisha historia yake haipotei katika taifa letu na Afrika kwa ujumla.

MUNGU awe nawe katika maisha yako mapya
Mzee wetu na shujaa wa kipekee katika taifa letu.

Tumalize msiba kwanza Wakuu, mambo a kawawa day ni sawa na kugombea mali za marehemu hata kabla hajazikwa.

Mbona mna haraka sana? priority kwa sasa ni maombolezo (Kuwafariji wafiwa) na mazishi.

haya ya kawawa day tutayapanga tu si priority kwa sasa sawa wakuu?
 
Safi sana....ila naomba kuuliza swali inakuwaje mtu anakufa then ndani ya dakika 35 tayari wimbo uko redio tayari na unachezwa?

Duu Hii Kali, ndani ya dk 35 tayari wimbo umeshatungwa kurekodiwa na kurushwa hewani???.

Sijaona Efficiency kama hii katika Tanzania
 
AM NOT.
tutakua tunaadhimisha siku kama hizi ngapi kwa viongozi wa serikali???, which means itakua public holiday?, waTZ tuache uvivu, mtu kama kaondoka akumbukwe ndani ya nafsi, TUCHAPE KAZI JAMANI.


Asante sana. I also dont like this idea at all. Watu siku hiyo hawamkumbuki huyo shujaa hata kidogo halafu tunataka holiday, heh!
 
Safi sana....ila naomba kuuliza swali inakuwaje mtu anakufa then ndani ya dakika 35 tayari wimbo uko redio tayari na unachezwa?
r u serious? walijiandaa na kifo chake mapema nini? tungekuwa sharp hivi na kwenye mambo mengine ,mbona tungefika mbali.
 
Back
Top Bottom