Mzee Kawawa afariki dunia!

Mzee Kawawa afariki dunia!

kawawa1.jpg

RIP
 
BURIANI MZEE KAWAWA
KIFO KIMEMPATA KATIKA HOSPITALI IPI ?
TARATIBU ZA MAZISHI ZINAKUAJE MAANA WENZETU HUWA HAWALAZI MAITI

QUOTE=Halisi;721891]Kumaliza mwaka ni jambo ZITO sana. MUNGU ashukuriwe, maana ndiye mwenye uwezo wa kupanga na kupangua. Sote tuombe Mungu.. Mengine zaidi baadaye... INASIKITISHA[/QUOTE]
 
R.I.P Simba wa Vita. Mwenyezimungu akupe makazi bora katika Pepo yake. INNA LILLAHI WAINA ILLAIHI RAJIUNA.
 
Ni profile nzuri lakini sababu za kuitwa simba wa vita ni kipindi cha miaka ya late 50s akiwa labour unionist wakati wa mapambano ya siasa/hali bora za wafanyakazi hivyo ujasiri wake kukabili wakoloni ulimpa hiyo hadhi
 
Poleni sana wafiwa.
Natamani angefanya kitu / angetoa tamko wakati wa uhai wake siku za mwisho kuhusu mustakabali wa nchi yetu, basi tena. Poleni sana
 
Eeeeeeweeeee MUNGU wa IBRAHIM, ISSAC na YAKOBO Jina Lako liimidiwe na litukuzwee Milele AMINA
 
RIP Kawawa! Msalimie mpendwa wetu Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere mwambie Taifa alilolipigania linatafunwa na watu wachache. Chama alichokiongoza ili kiwe chama cha wakulima na wafanyakazi na nuru ya mafanikio katika ukombozi wa watanzania kiuchumi, ndo kwanza kimekumbatia matajiri wa kifisadi!!

Amen
 
Mungu ampumzishe kwa amani kamanda wa vita, Simba sports mwenzetu,mwana CCM na Mtanzania mwenzetu, Mungu amempumzisha katika staili ile ile ya Mwalimu JK, alimuacha Mkapa akijiandaa kwa term ya pili na Simba wa vita RMK amemuacha Jakaya akijiandaa na term ya pili, mbele yake, nyuma yetu. Jina Bwana lihimidiwe. Mungu ibariki Tanzania
 
From: Mwanakijiji.com

Waziri Mkuu wa Tanganyika na mpigania huru wa Tanganyika na Muasisi wa Muungano mzee Rashid Mfaume Kawawa amefariki dunia. Habari ambazo zinatiririka taratibu kutoka vyanzo mbalimbali zinadokeza kuwa mzee Kawawa amefariki dunia leo na mpango wa kulitangazia taifa msiba huu mkubwa uko mbioni na wakati wowote kuanzia sasa Rais Jakaya Kikwete atalihabarisha taifa juu ya msiba huu wa kitaifa wa mmoja wa viongozi waliopendwa na waliolitumikia taifa kwa muda mrefu. Mzee Kawawa alikuwa ni swahiba wa karibu zaidi wa baba wa Taifa Mwalimu Julius K. Nyerere.
kawawa_1.jpg
Mzee Kawawa alizaliwa Mei 27 , 1926 huko Songea kijiji cha Matepwende mkoani Ruvuma. Alianza elimu ya msingi huko Liwale Lindi. Aliendelea na elimu ya kati (middle school) hapo Dar-es-Salaam school ambapo mmojawapo wa wanafunzi wengine ni marehemu mzee Kanyama Chiume mpigania uhuru toka Malawi aliyeishi uhamishoni nchini Tanzania kwa muda mrefu. Wengine katika shule hiyo wakati huo ni pamoja na kina Abdul Sykes, Ali Sykes, Hamza Aziz na Faraji Kilumanga.

Aliendelea na masomo yake huko Tabora Boys kati ya 1951-1956. Alikuwa ni Waziri Mkuu wa Tanganyika mwaka 1962 wakati Mwalimu Nyerere alipoamua kwenda mikoani kujenga chama na kufanya shughuli za kisiasa. Baadaye aliteuliwa tena kuwa Waziri Mkuu mwaka 1972-1977 na akawa miongoni mwa wahamasishaji wakubwa wakati wa vita ya kumng'oa nduli Idi Amin ambapo alitembelea wapiganaji wetu waliokuwa mstari wa mbele kule Uganda. Hii ilimpatia jina la "Simba wa Vita" jina ambalo lilimkaa vyema kwa muda mrefu.

Kabla ya kuingia katika harakati za kupigania Uhuru Mzee Kawawa alikuwa ni miongoni mwa waanzilishi wa Shirikisho la Wafanyakazi mwaka 1955 ambapo alichaguliwa kuwa Katibu wake Mkuu wa kwanza. Ni katika nafasi hii ndiyo aliweza kuanza kushiriki kwa nguvu zaidi katika harakati za kupigania uhuru wa Tanganyika akihamasisha wafanyakazi. Kabla ya hapo alikuwa ni Katibu Mkuu wa Shirikisho la Wafanyakazi wa Serikali.

Februari 1956 Mzee Kawawa aliacha kazi yake ya Shirikisho la Wafanyakazi kutokana na kuwa mwajiriwa wa serikali kitu ambacho kilimkataza kuhusisha na siasa na kuamua kuingia katika harakati za kudai uhuru kupitia TANU. Alikuwa Mjumbe wa Kamati Kuu ya TANU mwaka 1957, Makamu mwenyekiti wa TANU mwaka 1960.

Mwaka 1964 baada ya Muungano Mzee Kawawa alikuwa ni Makamu wa Pili wa Rais akiwa ni msaidizi wa Rais wa Muungano kwa upande wa mambo ya Bara.
Katika siasa amewahi kushika nafasi mbalimbali ikiwemo ile ya Ukatibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi na Makamu Mwenyekiti wa CCM na amekuwa mjumbe wa kudumu wa Kamati Kuu ya CCM.

Mzee Kawawa alikuwa ni mtoto wa kwanza kati ya watoto nane na mojawapo ya kazi zake za awali ilikuwa ni uchezaji wa filamu za uhamasishaji na akawa ndiye mcheza filamu wa kwanza kiongozi mweusi (lead actor).

Mzee Kawawa alikimbizwa hospitali hapo jana kutokana na hali yake kuwa mbaya na kulazwa katika chumba cha wagonjwa mahututi; ambapo mapema leo asubuhi alifariki dunia. Mipango ya mazishi inaandaliwa.

Mungu ailaze roho ya Marehemu Pema Peponi, Amina.

Mungu awape faraja na uvumifivu familia ya marehemu maana sote tuko safarini.
 
From: Mwanakijiji.com

Waziri Mkuu wa Tanganyika na mpigania huru wa Tanganyika na Muasisi wa Muungano mzee Rashid Mfaume Kawawa amefariki dunia. Habari ambazo zinatiririka taratibu kutoka vyanzo mbalimbali zinadokeza kuwa mzee Kawawa amefariki dunia leo na mpango wa kulitangazia taifa msiba huu mkubwa uko mbioni na wakati wowote kuanzia sasa Rais Jakaya Kikwete atalihabarisha taifa juu ya msiba huu wa kitaifa wa mmoja wa viongozi waliopendwa na waliolitumikia taifa kwa muda mrefu. Mzee Kawawa alikuwa ni swahiba wa karibu zaidi wa baba wa Taifa Mwalimu Julius K. Nyerere.
kawawa_1.jpg
Mzee Kawawa alizaliwa Mei 27 , 1926 huko Songea kijiji cha Matepwende mkoani Ruvuma. Alianza elimu ya msingi huko Liwale Lindi. Aliendelea na elimu ya kati (middle school) hapo Dar-es-Salaam school ambapo mmojawapo wa wanafunzi wengine ni marehemu mzee Kanyama Chiume mpigania uhuru toka Malawi aliyeishi uhamishoni nchini Tanzania kwa muda mrefu. Wengine katika shule hiyo wakati huo ni pamoja na kina Abdul Sykes, Ali Sykes, Hamza Aziz na Faraji Kilumanga.

Aliendelea na masomo yake huko Tabora Boys kati ya 1951-1956. Alikuwa ni Waziri Mkuu wa Tanganyika mwaka 1962 wakati Mwalimu Nyerere alipoamua kwenda mikoani kujenga chama na kufanya shughuli za kisiasa. Baadaye aliteuliwa tena kuwa Waziri Mkuu mwaka 1972-1977 na akawa miongoni mwa wahamasishaji wakubwa wakati wa vita ya kumng'oa nduli Idi Amin ambapo alitembelea wapiganaji wetu waliokuwa mstari wa mbele kule Uganda. Hii ilimpatia jina la "Simba wa Vita" jina ambalo lilimkaa vyema kwa muda mrefu.

Kabla ya kuingia katika harakati za kupigania Uhuru Mzee Kawawa alikuwa ni miongoni mwa waanzilishi wa Shirikisho la Wafanyakazi mwaka 1955 ambapo alichaguliwa kuwa Katibu wake Mkuu wa kwanza. Ni katika nafasi hii ndiyo aliweza kuanza kushiriki kwa nguvu zaidi katika harakati za kupigania uhuru wa Tanganyika akihamasisha wafanyakazi. Kabla ya hapo alikuwa ni Katibu Mkuu wa Shirikisho la Wafanyakazi wa Serikali.

Februari 1956 Mzee Kawawa aliacha kazi yake ya Shirikisho la Wafanyakazi kutokana na kuwa mwajiriwa wa serikali kitu ambacho kilimkataza kuhusisha na siasa na kuamua kuingia katika harakati za kudai uhuru kupitia TANU. Alikuwa Mjumbe wa Kamati Kuu ya TANU mwaka 1957, Makamu mwenyekiti wa TANU mwaka 1960.

Mwaka 1964 baada ya Muungano Mzee Kawawa alikuwa ni Makamu wa Pili wa Rais akiwa ni msaidizi wa Rais wa Muungano kwa upande wa mambo ya Bara.
Katika siasa amewahi kushika nafasi mbalimbali ikiwemo ile ya Ukatibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi na Makamu Mwenyekiti wa CCM na amekuwa mjumbe wa kudumu wa Kamati Kuu ya CCM.

Mzee Kawawa alikuwa ni mtoto wa kwanza kati ya watoto nane na mojawapo ya kazi zake za awali ilikuwa ni uchezaji wa filamu za uhamasishaji na akawa ndiye mcheza filamu wa kwanza kiongozi mweusi (lead actor).

Mzee Kawawa alikimbizwa hospitali hapo jana kutokana na hali yake kuwa mbaya na kulazwa katika chumba cha wagonjwa mahututi; ambapo mapema leo asubuhi alifariki dunia. Mipango ya mazishi inaandaliwa.

Mungu ailaze roho ya Marehemu Pema Peponi, Amina.

MUNGU atakupokea katika ufalme wake Mzee wetu na shujaa wa kipekee. Msalimie sana Mwalimu.

Wana JF twende mbele zaidi na kufikiria ni kwa namna gani bora tutakuwa tukimkumbuka kila mwaka na kumuenzi SIMBA WA VITA.
 
BURIANI MZEE KAWAWA
KIFO KIMEMPATA KATIKA HOSPITALI IPI ?
TARATIBU ZA MAZISHI ZINAKUAJE MAANA WENZETU HUWA HAWALAZI MAITI


Alilazwa jana katika Hospitali ya Taifa Muhimbili katika wodi wa wagonjwa mautihuti (ICU)

JK ameondoka muda si mrefu nadhani ndiyo anaenda kulitangazia taifa kuhusu huu msiba mzito wa Marehemu Mzee wetu Kawawa.

Mazishi nadhani bado mipango maana ndugu na jamaa bado wapo hapo hospitalini. wakiongozwa na mama JK

RIP Kawawa
 
another African legend has gone..ooh Lord, may his soul rest in peace! we r behind u
 
R.I.P jirani yangu kule madale...mungu akupe mapumziko ya milele na amani ya bwana iwe nawe..

Wafiwa poleni sana na mungu awatie nguvu sana na ujasiri katika kipindi hiki kigumu kabisa kupata kupita katika maisha yenu...

Rafiki Yangu Vita Kawawa mungu akupe subira na nguvu..

Amen
 
ooooooooooooooooooooooooooooooooh God!simba wa vita!tutakukumbuka daima,ulikuwa icon wa siasa za Tanganyika na Tanzania.oh,R.I.P
 
Kweli watu wazuri hawaishi muda mrefu,
Mzee wetu 83 miaka ni kama siku na sio kufuru,
Ni kutokana na mazuri mengi yaliyokupa umaarufu,
Hukusita kukemea viongozi na wakwapuaji sarafu,
Taarifa za msiba zimeufanya mwili wangu uka dhoofu.

RADICAL endelea machozi yananitoka.
 
Back
Top Bottom