Mzee Kawawa afariki dunia!

Mzee Kawawa afariki dunia!

Rashid Kawawa ni mmoja ya mifano ya loyal people to their leaders; alibeba mengi (mazuri na mabaya). Nakumbuka kuna miaka tulimkandya kwa kukosa elimu, maamuzi na hata mambo ya kishirikina... lakini hata siku moja hakukurupuka kujibizana na yeyote kama alivyo mzee wetu kibogoyo au makamba nk. Alisimama kwenye yake anayoyaamini

Alilea family, ni mmoja wa mifano hai ya siasa ni kilimo na sera ya vijiji!!! ameinua kila alipoweka mji na amefaidi ujana wake pia

RAshid alikuwa shujaa, family man, hero, villain na kila unachoweza define kutokana na perception yako/yake

Mungu ampumzishe kwa amani

Swali: Je aliyepost jana alikuwa sahihi?? Na hii si kama ile ya JK??
 
Indeed, the man need to be prayed for a nice rest in peace. pole sana Ndg. Vita Rashid.
 
RIP Kawawa.

Kwa hiyo utabiri wa Yahya unafanya kazi siyo. Shibuda endelea na mpango wako kama unataka uwe statistic by the end of 2010.
 
RIP RASHIDI!.

Halisi/Mode, kwa kuanzia kama JF initial Tribute ya Mzee Kawawa, nashauri ile profile ya Mzee Mwanakijiji kuhusu iwekwe chini ya tangazo la Halisi, kama inawezekana Halisi aiweke mwenyewe, ama mode ili kila atakalog kutoa pole apate zaidi kidogo.

Asante Halisi kwa hii ya ukweli sasa. Asante Invicible kwa angalizo la jana kuhusu afya yake na asante Mzee Mwanakijiji kwa profile yake, young generation wasiojua haya ni wengi kuliko sisi old guards.

He was the most humble in times of Mwalimu.

Pole sana Zamaradi na familia nzima ya Mzee Wetu, Shujaa Wetu, Kipenzi Chetu na Mwenzetu Simba wa Vita.

RIP RASHIDI!.

Kaka Pasco, Invisible anafanyia kazi. natetemeka hapa nilipo. Inasikitisha
 
Au ndio mambo ya utabiri wa Sheikh Yahya? RIP Simba wa vita.
 
Masikini mzee wetu Rashidi Mfaume Kawawa, Mungu akuweke mahali pema peponi.
Ulifanya mengi. TANU,Tanganyika,Tanzania na CCM havitakusahau daima.
R.I.P
 
Hakika sisi ni wenye kurejea kwa mwenyezi mungu. Twamuomba mola wetu amsaheme madhambi yake
 
Rip Mzee wetu Kawawa tutakumbuka kwani unaliacha taifa ambalo viongozi wake wanajali zaidi matumbo Yao na sio watanzania
 
Kumaliza mwaka ni jambo ZITO sana. MUNGU ashukuriwe, maana ndiye mwenye uwezo wa kupanga na kupangua. Sote tuombe Mungu.. Mengine zaidi baadaye... INASIKITISHA

Halisi,
Kati ya watu ambao hawatamsahau Mzee huyu ni Rais mstaafu wa Mozambique Joaquim Chisano enzi za nchi za mstari wa mbele wa uhuru kusini mwa Africa. Yeye na Brigedia Hashim Mbita walikuwa hawalali. RIP Kawawa.
 
Haiwezekani, Kwanini asisubiri Jumaatatu?
MNHHHH, BE SERIOUS MKUU!
kwani alikua na mkataba na Mungu??
huwezi jua wewe mwenyewe kama utafika kesho, hujafa hujaumbika na usitukane mamba ilhali hujavuka mto!
HAPPY NEW YEAR 2010!
 
Raha ya milele umpe ee Bwana na mwanga wa milele umwangazie,apumzike kwa amani.Amina

Poleni sana wanafamilia, ndugu,jamaa na marafiki pia taifa lote kwa msiba huu mzito..Hakika daima utakumbukwa!
 
R.I.P. Mzee Rashid Mfaume Kawawa (Simba wa Vita). Uliishi kwa upendo mkubwa kwa Taifa lako. Ulitumia busara nyingi na uwezo wako mkubwa katika kutimiza wajibu wa kutetea, kulinda na kujenga nchi yako. Tanzania inamshukuru Mungu kwa maisha yako.

Mungu ailaze roho ya Marehemu Rashid Mfaume Kawawa mahali pema peponi. Amen
 
Kaka Pasco, Invisible anafanyia kazi. natetemeka hapa nilipo. Inasikitisha
Asante, Nilisahau kukupo pole,
Pole Halisi.
Pole Wanafamilia
Poleni wanaJF
Poleni Watanzania Wenzetu Wote.
RIP MZEE RASHIDI MFAUME KAWAWA!.
 
Poleni sana Watanzania wenzangu. Kama taifa napendekeza tuwe na KAWAWA DAY kuanzia mwaka ujao wa 2010. Tarehe 31/12 ya kila mwaka ni siku muafaka zaidi. Nini kifanyike kitaifa kila siku hiyo, ni suala la kujadiliana na kupanga kama taifa. Naamini Serikali italiafiki na kulifanyia kazi wazo hili ili kuhakikisha historia yake haipotei katika taifa letu na Afrika kwa ujumla.

MUNGU awe nawe katika maisha yako mapya
Mzee wetu na shujaa wa kipekee katika taifa letu.
 
Mungu aileze roho yake mahali pema peponi.
ilibaki kidogo auone mwaka 2010. ila yote ni mungu anapenda.
 
Back
Top Bottom