It was 2007....Mapenzi yetu yalikuwa mazuri(kwa kiwango cha ufaham nilichokuwa nacho)nilimpenda ila yeye hakunipenda kama nilivyodhani!.....Tulikuwa karibu sana na kutokana na baba kulazwa hosptl kwa maradhi ya moyo kila nilipoenda kusalimia baba nilikuwa nae......Ilikuwa ni tarehe 14 July 2007 mchana nilipojulishwa kuwa Dad pass away!Nilichanganyikiwa lakini baada ya nusu saa nilirudi kawaida,nilienda hosptl nikakuta baadhi ya ndugu,mwili ulihifadhiwa vizuri,nikampigia mpenzi wangu nimjulishe hakupatikana,baba yangu mdogo akaniambia niende kwa kaka yangu nikamjulishe kwani hakuwa anapatikana,.....Nilifika kwa bro akanikaribisha nilipita mpaka chumbani kama nilivyoea(alikuwa hajaoa)ndipo nikakutana na balaa,my biological brother alikuwa ndo anavaa bukta halafu mpenzi wangu alikuwa kajifunika shuka tu na wote walikuwa wanatoka kijasho!Kuashiria walitoka kwenye "Game",sikumbuki kilichoendelea kwani nilipopata fahamu nilikuwa nimelala chini nikipepewa,niliondoka na kuelekea msibani....,.Tulimaliza msiba lakini kwa mateso na maumivu,yule ex wangu sikumwona msibani pia sikuzungumza chochote na bro!Ndipo bro aliniomba tuzungumze,aliniambia kuwa nimsamehe,pia akaniambia walikuwa kwenye mahusiano kwa miezi miwili,niliumia sana,sikua na jinsi nilimsamehe kwa maumivu makubwa,kwani pamoja na yote bado alikua ni kaka yangu tu!Ilipita miezi miwili nilibadili namba simu na nilihama nilipokua naishi kwani ex alianzisha usumbufu!I had a bussines,na mahali ilipokuwa nilipanga niihamishe kuepuka usumbufu wa ex,nikiwa kwenye mchakato huo ndipo asubuhi moja nikakuta duka jeupe limeibiwa lote!!Katika kufuatilia nikaja kuambiwa kuwa ule ulikua ni mpango wa ex,lakini kulikuwa hakuna ushahidi wa kumtia hatiani,NILICHANGANYIKIWA,nilipata ushauri wa kila aina na baada ya miaka 2 nilipona,nimeingia kwenye maisha upya na nimesahau yote,naanza moja!...,.Najua wapo wamepitia kwenye changamoto zaidi ya hizi au wapo walioko kwenye changamoto,nimeamua kushare nanyi ili kama yupo wa kujifunza kupitia mimi basi na ajifunze,changamoto hizi zimenipa uzoefu mkubwa japokuwa nimepitia maumivu makubwa,.Wewe mwenye changamoto,jipe moyo hakuna kisichokuwa na mwisho,chukulia hiyo kama shule ya kujifunza japokuwa unajifunza kwa maumivu makubwa ya hisia na mwili,niliekuwa namuita mpenzi amenidisha nyuma,KUWENI MAKINI,i love u all!
Mungu mkubwa na ni mwenye nguvu,Glory to God Babu!Duh! Pole sana E...inatia moyo kuona kwamba umeweza kuendelea na maisha yako baada ya kuumizwa kiasi hicho na watu wawili muhimu kwenye maisha yako. Shukuru Mungu kwamba aliamua kukuonyesha kabla hujaoa, vinginevyo kaka angeendelea kukumegea hata baada ya harusi.