LazyDog
JF-Expert Member
- Apr 10, 2008
- 2,473
- 189
Nionacho mimi wala sio FAME, bali ni pale jambo linapokugusa kwa karibu. Ufisadi watu wengi hawau-feel directly na ndio maana sio wengi wanaopiga kelele.
Alichofanya Mengi ni kukoroga kidogo jambo lililopelekea kuwa na muendelezo wa vita dhidi ya MAFISADI. Sio mbaya watu wakiendelea kutetea "keki zao" hadharani, maana hapa ndipo tunapogutuka nani yuko upande upi na kutambua upana wa tatizo hili. Kwa njia hii utatuzi utakuwa rahisi.
Hatimaye mwananchi wa kawaida naye ataguswa kwa karibu, hapo ndipo atapotetea keki ambayo amekuwa akiikosa. Baada ya Mengi - maji kwenye mtungi yakitulia, tunahitaji mdau mwingine kulikoroga kidogo.
Alichofanya Mengi ni kukoroga kidogo jambo lililopelekea kuwa na muendelezo wa vita dhidi ya MAFISADI. Sio mbaya watu wakiendelea kutetea "keki zao" hadharani, maana hapa ndipo tunapogutuka nani yuko upande upi na kutambua upana wa tatizo hili. Kwa njia hii utatuzi utakuwa rahisi.
Hatimaye mwananchi wa kawaida naye ataguswa kwa karibu, hapo ndipo atapotetea keki ambayo amekuwa akiikosa. Baada ya Mengi - maji kwenye mtungi yakitulia, tunahitaji mdau mwingine kulikoroga kidogo.