Ninashindwa kuelewa mtu anavyotoa hoja, akajibiwa kwa hoja anaishia kutukana bila kujitathimini ni wapi amekosolowa ili ajirekebishe baadae akijua siasa zipo kila siku....
Nape! Mwanasiasa mzuri ni yule anayeyafakari kabla ya kuongea, ni yule anayejiandaa na kupangilia agenda za kuzungumza kabla hajapanda jukwaani,ni yule anayethamini na kutathimini aina ya hadhara/wahusika anaotaka kuwa-address siku hiyo, ni yule anayesoma upepo wa siasa upo upande gani na unavuma kuelekea upande gani, lazima ujue unatumia chanel gani kufikisha ujumbe. Hayo ni machache tu, naomba nizungumzie kidogo.
1.Kutafakari kabla ya kuongea. Hapa ni lazima ujue aina ya topic iliyoko mezani, lazima ujue umuhimu wa topic hiyo kwa mahali hapo, manufaa, changamoto na suluhu kwa wanaosikiliza. Usipende kuongelea topic bila kuangalia umuhimu, manufaa yke na jns ya kukabidhiana na changamoto zitakazojitokeza wakt au baada ya kuzungumza!
2. Aina ya hadhara, ni lazima ujue ni watu gani unawapelekea ujumbe wako, ni wazee, vijana, watu wa kati, wasomi au watoto! Lazima ujue mwitikio wao, je wanapokeaje ujumbe wako? Je wananielewa? Wana idea na hiki ninachokizungumza? Wanafaidka kwa sasa au ni baadae, watakuwa na subira? Mood zao ziko je katika kuniskiliza? Wamekula wakashiba,? Ni wahusika? Usije ukaingiza mguu wa kulia kwenye kiatu cha mguu wa kushoto.
3. Upepo wa siasa unavuma vipi ni suala la msingi sana, kwa mfano upepo wa siasa kwa Tanzania ni wa mageuzi na macho ya watu wengi hata wanasiasa wanalenga zaidi kujua je huyu au chama hiki kitatufanyia nini iwapo kitapewa serikali, sasa lazima ujue kila unachozungumza watu wanakitafsiri mara mbili yako, wanaangalia faida ya moja kwa moja, muda wa hiyo faida na madhara yake! Je huyu ni nani? Anataka nini na ni kwa faida gani kufanya hvyo?
4. Chanel au lugha ya kufikisha ujumbe wako kwa hadhara. Lazima ujue lugha unayotumia kama ni vijana unatumia lugha ya ujana, kama ni wasomi kuna lugha yao, kama ni akina mama kuna lugha yao, KAMA NI WAZEE KUNA LUGHA YAO, watu wa kati na watoto wote wana lugha yao. Kwa mfano refer Mbunge wa mbeya mjini Mh. Sugu alitumia lugha gani kuwatuliza vijana/ wamachinga waliokuwa wanavutana na polisi kule mbeya.
Tatizo ninalo liona kwa ndugu zangua hawa wanasiasa , hawajui kama siasa ni science pia wanashindwa kujua kwamba wao ni viongozi na siku zote psychology ya watu wengi wanaamini kwamba kiongozi anajua zaidi kuliko wale anaowaongoza hata kama wamemzidi kielimu au uzoefu! Ndugu yangu Nape najua labda ni kutokujua au makusudi kamili huwa napenda sana kumsikiliza sana lakin kuna kitu anakosa kati ya hivyo nilivyovitaja hapo juu! Yeye mwenyewe akitafakari atajua au wenzangu walionielewa watamsaidia.
Inawezekana mbinu iliyoasisiwa kihalali kwamba hata kama nikiongea kitu ambacho hakijafurahisha wazee au vijna hakuna wakuniuliza, kwa kuwa mimi ni mimi watake wasitake wataheshimu tu na watanipigia makofi. Kwa hili la kusema wale wote wanaoshabikia serikali tatu ni wazee wanaokaribia kufa... Hata mimi lilinishutua sana japokuwa kila mtu atakufa..... Jaribu kufanya siasa sa kisomi kwa kuzingatia taaluma yako...
Asanteni