Sijaona hiyo unayosema siasa sio fani inahusiana vip na topic hii, maana sioni hapa chochote kinachohusiana na hilo, zaidi tu inaleta taswira ya HOFU YA MUNGU ambayo ni muhimu kwa kiongozi kujiona yeye sio juu ya wote na kuwa ana wajibu wa kufanya mema kwa watu, refer "HUWEZI KUMPENDA MUNGU USIYEMUONA KAMA HUWAPENDI WATU UNAOWAONA".
Na sioni hiyo ya kufananishwa na Sokine inahusiana vip na hili, sijawahi sikia kama Sokoine alikuwa anawapangia viongozi sehemu za kwenda kuabudu?kama angefanya hivyo nadhani asingepata sifa alizopata maana angekuwa ni mtu wa ajabu sana kufanya, serikali yetu haina dini na watu wana haki kuwa na imani zao ilmuradi hawavunji sheria ya nchi.
Kingine, kila zama ina kanuni zake, ata Sokoine angekuwepo leo asingezui soko huria ambalo wakati huo halikuruhusiwa maana ata waliokuwa reference yetu, Uchina na Urusi wameruhusu, sembuse Tanzania?mazingira na wakati hubadilisha mtazamo.
Ila msingi tunaomsifia Sokoine ni UADILIFU WAKE NA UFUATILIAJI WA MASUALA YA MSINGI, japo kuna sehemu hatukubaliana na sera alizokuwa anazisimamia wakati huo.
Na naamini wanaomfananisha Mwigulu hawaamaanishi kuwa atakuwa Sokoine 100%, maana haohao wanaomfananisha hawataki turudi kwenye Tanzania ya mwaka 1980s kwa kila kitu bali wahitaji USIMAMIZI WA MAKINI ULIOJAA UADILIFU NA UNAOANGALIA MASLAHI YA NCHI NA WATU WAKE.