Tatizo lenu nyie wapambe njaa ndio zinazo watoa akili sasa nani asiyejua kwa nafasi ya Mwigulu posho anazochokuwa anauwezo wa kwenda kanisa lolote duniani kila jumapili akiamua?
Swala hapa yeye ni kiongozi kuwa kioo cha jamii angeenda kimya kama kweli anamfuata mungu kwa malengo yake nani angepiga kelele.
Lakini unapoanza kufanya publicity za wewe kwenda makanisa ya Nigeria linakuwa zaidi ya swala la imani bali kujionyesha ya kuwa wewe una option mbele ya jamii ambao wengi hawana huo uwezo isitoshe kuna watu wanaweza amini Nigeria kuna kanisa bora zaidi hadi waziri analifuata mara kwa mara ndio maana yake hiyo.
Kwani unadhani hao akina Sokoine au Nyerere wangeshindwa kuwajengea majumba watoto zao wakaya promote au kuchagua kuendeshwa na magari ya kifahari wakati wa uonogzi.
Issue hapa ni twasira anayoileta kwa jamii kutokana na uwezo wake na direct message anayowatumia waumini wengine wa dini. Unatakiwa uongoze kwa mfano anasa zako ziwe private, kama unaona kuna umuhimu kwa kwenda kwa TB Joshua nenda kimya basi sio kutuonyesha sie tusio na uwezo uongozi maana yake utajiri.
Ndugu yangu, ndio tatizo lilelile la kuona hali yako ni hali ya wengine, unadhani kila mtu anaishi kwa upambe kwa ajili ya kufurahisha watu.Wengine tunajadili tu kutokana na tunavyoona hali ilivyo na uhalisia ulivyo.Na huyo Mwigulu hana uwezo wa kunilipa.
Hayo ya kwenda Nigeria ni anasa?yaleyale limitation zako ndio zinafanya uone anasa kwa sababu bajeti yako labda hilo la kujitangaza?sijaona press conference yoyote imeitishwa Mwigulu akiwataarifu watu kuwa anaenda Nigeria; huyu aliyeleta mada it just happened kuwa ameona kwenye TV na kuleta hapa, asingeona na wengine wasingeangalia huko TV basi tusingejua kuwa yupo huko maana naamini hiyo ibada haionyeshwi TBC wala Tv yoyote za Tanzania.
Bottom line ni kuwa hakuna cha ajabu na wala sio anasa kwa dunia hii ya leo mtu kutembelea Nigeria, umbali na ukaribu ni related term kutokana na uwezo wa mtu, kwa mshahara wa Ubunge anaweza kabisa na sio anasa.
Hayo ya Nyerere na Sokoine kuishi kimaskini, sioni inahusiana vip na hii topic maana kwenda Nigeria sio utajiri. Kama Mwigulu katumia mshahara wake na hajatumia ata senti ya serikali kwenye safari yake, kajilipia mwenyewe hotel na chakula huko Nigeria, yes hajavunja kanuni yoyote ya uadilifu tunaoutaka.
Kumbuka dunia inabadilika, walivyoishi mwaka 1980 sivyo tunavyoishi leo.Na KUWA MASKINI AU KUISHI KIMASKINI WAKATI UWEZO UNAO SIO SIFA.
WAtanzania hawahitaji kiongozi maskini bali wanahitaji kiongozi mwenye uwezo, nia ya dhati na uadilifu wa kusimamia rasilimali za nchi na kujenga mazingira ya kujenga uchumi unaonufaisha nchi na wananchi walio wengi.
Na kufanya hivyo, kiongozi huyo ni lazima asiwe na akili za kimaskini maana kipofu hawezi muongoza kipofu mwenzake.Muhimu hapa ni UWEZO WAKE, UADILIFU WAKE NA UCHU WA KUBADILISHA HALI KUWA BORA ZAIDI KULIKO ILIVYO SASA.