Mwigulu hili hapana

Mwigulu hili hapana

Ukiangalia ile video kuna watu wanne walimfuata nape
1:aliyemtolea bastola
2:alivaa shati jeupe alimuamuru yule jamaa arudishe bastola
3:alivaa Tshirt nyeusi ,jeans na sneaker alifungua mlango wa gari
4:alivaa nguo sare na jamaa aliyetoa bastola
Wote ni polisi na wanajuana mwigulu una tuzuga na je lini atapelekwa mahakamani maana wote wanajulikana ni polisi
utasikia amehukumiwa kwenye mahakama za kijeshi au kapewa onyo kali
 
Mwigulu nchemba ndugu yangu usijaribu kama unaweza jitoe mzima mzima kama nape simamia haki but jiandae nawewe jutumbuliwa
 
Usiume na kupuliza, mtu aliyemtolea bastola Nape anajulikana wazi Katoka wapi na katumwa na nani! Sisi raia ni ngumu kujua lakini kwa cheo chako cha waziri wa mambo ya ndani itakuwa ni kichekesho na dhihaka ya mwaka kumuagiza IGP atamtafute huyo mtu na kuchukuliwa hatua!
Eti ATAFUTWE na aangaliwe Kama ni askari kweli... Ooh My God kuna raia anaweza kufanya vile kweli? Kwa uthubutu Kutoka wapi?
Please tupunguzieni drama zenu hizi, unafahamu vema organs zisizo chini yako zinavyofanya kazi, umekuwa nazo hata kabla hujawa waziri enzi zile za zile drama zako
Usituzuge sasa yule mtu ulichopaswa kufanya ni KUAGIZWA AKAMATWE MARA MOJA.... kwakuwa anajulikana vema alitoka kitengo gani..... Punguzeni siasa za kitoto mtuhumiwa yuko huru kwa pozi zote.... Alitumwa hakwenda mwenyewe pale.... Mojawapo ya Kanuni za askari ni kupokea amri na kutekeleza bila kuhoji... Mtafuteni aliyemtuma pale.....
We are living in the era of reasoning....
Mkuu inawezekana ikawa toyo gun ya watoto! Au walikuwa bongo movie
 
Yule Jamaa aliyemtolea Mhe.Nape bastola mbona hajatiwa nguvuni?. Hapa uzalendo utakosa.
 
~kwani kwa kuwa ni waziri anaweza kufahamu askari wote mmoja mmoja?....
~ok we differ!


Anatakiwa kuwa na mechanisms za kujua hilo. Mbona walimu wakuu shule zao zikiharibu wanafukuzwa na waziri? Kwani Ndalichako anajua walimu wote wa nchi hii? Ni mechanisms tu ndio zinamsaidia!
 
Mwigulu Kisu kimechoma ktk mfupa akigeuka kulia aliefanyiwa tukio ni best yake kushoto kuna mfalme juha sasa haelewi afanyaje maana kibarua anakipenda na pia anapenda kuishi muda mrefu..
 
Kwa nn na wale askari walio vamia clouds hakujitokeza na kumuagiza igp awafatilie au kwa kuwa walivaa uniform? Wao waliwatuma? Hawakupaswa kutafutwa? Mwigulu ni mnafiki na mshenzi pia.
Kwa nini unamtukana?? Hivi kweli ungekuwa uso kwa uso na Waziri Mwigulu ungemtukana hivyo?? Kwa nini usichangie thread kiungwana? Au kwa kuwa uko nyuma ya keyboard??
 
Kwanini Mwigulu hajatumbuliwa? Naona nayeye ni mzigo tu
 
Jina lako limenipa sababu ya kukudharau. Laanaa turkadiriiii.
Utakuwa unaumwa unagoma kunywa dawa wewe. Jina lako ama langu ni majina kama mengine. Sina laana niko huru kuliko wewe. Hivi ukisema nina laana ndo tayari inakuwepo?. Haaahaaahaaahaaa, kuwaza siyo sare usitake tuwaze sare wote hiyo itakuwa ajali.
Aliyekuponza ni huyo aliyekukaririsha hiyo elimu bila kukupa uhuru ktk kichwa chako.
 
Usiume na kupuliza, mtu aliyemtolea bastola Nape anajulikana wazi Katoka wapi na katumwa na nani! Sisi raia ni ngumu kujua lakini kwa cheo chako cha waziri wa mambo ya ndani itakuwa ni kichekesho na dhihaka ya mwaka kumuagiza IGP atamtafute huyo mtu na kuchukuliwa hatua!
Eti ATAFUTWE na aangaliwe Kama ni askari kweli... Ooh My God kuna raia anaweza kufanya vile kweli? Kwa uthubutu Kutoka wapi?
Please tupunguzieni drama zenu hizi, unafahamu vema organs zisizo chini yako zinavyofanya kazi, umekuwa nazo hata kabla hujawa waziri enzi zile za zile drama zako
Usituzuge sasa yule mtu ulichopaswa kufanya ni KUAGIZWA AKAMATWE MARA MOJA.... kwakuwa anajulikana vema alitoka kitengo gani..... Punguzeni siasa za kitoto mtuhumiwa yuko huru kwa pozi zote.... Alitumwa hakwenda mwenyewe pale.... Mojawapo ya Kanuni za askari ni kupokea amri na kutekeleza bila kuhoji... Mtafuteni aliyemtuma pale.....
We are living in the era of reasoning....

Kwani alikua nani yule
 
Back
Top Bottom